thanks kwa kwa kuwakumbusha lakini wamelala hawawezi kufanya ulicho kishauriKatika Maisha ya binadamu inafahamika na kujulikana kuwa kuna kuzaliwa kuishi na hatimae kifo kwa Mwanadamu yoyote yule.Kwenye bishara na shughuri nyingine kuna Mzunguko wa biashara kisayansi ambao unaitwa LIFE CYCLE [Yaani kama Mwandamu biashara nayo inapitia Mchakato uleule wa binadamu wa kuzaliwa kuisha na hatimae kufa kwa shughuri ama biashara husika].
Ilikufa TAA ikazaliwa TANU,Ikafa TANU NA ASP kikazaliwa Chama Cha Mapinduzi [CCM],sasa yapata miongo mitatu [3] toka kuzaliwa kwa CCM.Kwa kuwa zama [NEW ERA] hizi sasa ni mpya, zilizosimama kwenye dunia mpya yenye siasa zinazosuguana na UTANDAWAZI [Globarization] na hivyo kuifanya dunia kuwa kama kijiji kimoja na kuwafanya binadamu wa zama hizi kuwa na uelewa mkubwa sana wa mambo mengi haswa katika uwezo wa kuwasiliana na kupashana habari duniani.
Hivyo CCM kwa ujio huu wa UTANDAWAZI toka miaka ya tisini inaweza kuwa na tathimini ya kuijpima uwezo wake juu ya kukabiliana na mawimbi mapya ya kizazi kipya kisicho itaji kujua na kukalilishwa kuhusu AMANI na UMOJA,bali kufundishwa jinsi ya kulinda AMANI hiyo isipotee kupitia vyama vyovyote ama kupitia taasisi yoyote ile.
Kwa kuwa CCM inajijua na kutambua malengo ya kuanzishwa kwake,haina budi kukaa na kuona namna mpya ambayo kwa kuanzia kaurii mbiu ya kujivua gamba ni vyema wakaenda mbali mpaka kubadilisha jina na kusisi KATIBA MPYA na ITIKADI MPYA ya Chama cha Mapinduzi yenye maono [Vision] ya CCM MPYA yenye kukabidhi vijiti vya mbio kwa kizazi kipya [New Generation Dotcom].
Kwa kuwa kutokukabidhi mbio hizo za vijiti kwa kizazi kipya na kuondoa ndani ya CCM tabia ya huyu ni mwenzetu,na CCM ya wafanya biashara na wachumia tumbo,ni hakika CCM itakuwa imejichimbia KABURI kama chama husika na pia viongozi wake watakuwa ni wahanga wa kile walichokitenda na kukiasisi wenyewe na hivyo kulipia vibaya sana.
Sasa ni heri ya nusu shari kuliko shari kamili au ni heri zimwi likujualo kwa kuwa alikuli likakwisha.CCM wabadilike na kuasisi mabadiliko Wananchi wanayoyataka kwa dhati yao ya moyo.Tofauti na hayo na viongozi wapenda ubwana na utukuzwa wa kukubaliana na viongozi wajivuni na wapenda kuabudiwa kukubali kutayarisha vikwazo vya kuzuia ustawi wa demokrasia kama huo mpango unaotajwa wa kuundwa kwa sheria mpya inayohusu maandamano,wananchi watakapochua hatua dhidi ya askari mmoja kwa Wananchi elfu kumi ni risasi ngapi zitatoka kuwazuia wasiandamane.Hapa ni kuangalia Wananchi wanataka nini?Kisha kupitia CCM wananchi wapewa jibu sahihi na katika muda sahihi.Vinginevyo wakilikosa jibu hilo watalitafutia kupitia chama kingine.Na kwa dhahili hivi sasa inafahamika kuwa Wananchi wanaanza kupata imani na kutambua kuwa kumbe kupitia CHADEMA wanaweza kupata JAWABU sahihi la Matatizo yao.
CCM BADILISHENI JINA LA CHAMA,KATIBA YA CHAMA NA ITIKADI YENU MPYA ITAMBULIKE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Kama hamuamini endeleeni na jina hilo na katiba yenu na wananchi wasijue ITIKADI YENU,na hakika 2015 CCM itapasikia Magagoni kama KANU ilivyoisikia IKULU YA KENYA.
Nasilisha
Walianza kwa kunakili sera la ELIMU (kuifanya Dodoma kuwa Education Capital)