TCRA tuelezeni wateja wa M-Pesa/Tigopesa wanapofariki warithi wanapataje haki zao?

Chereko

Member
Jul 20, 2009
54
16
Watu wengi kwa sasa hutunza pesa zao kwenye M-PESA, TIGO-PESA na kadhalika na kuifanya kama ndio benki (ingawa hakuna interest). Ni vema kwa kuwa unapotaka malipo ya haraka haraka au kumtumia mtu haraka ni bora sana. Sidhani kama tunafahamu juu ya risk zake:
  • Umeweka laki tano, ukachukua mzinga (Mola aepushilie mbali) na hukusema kwa mtu kuwa una laki tano kwenye M-pesa au Tigo Pesa, vibaka wakalamba ile simu wakanyofoa simcard wakaitupa wakabaki na simu, hivi ina maana kuwa hiyo pesa ndio imetoka hivo sio?
  • TIGO au VODACOM kuna siku watakaa waseme mteja mmoja aliwekeza kwetu laki tano miaka miwili imepita na simu haipo hewani hivyo tutafute ndugu zake?
Huo ni mfano tu lakini hali kama hiyo au inayofanana na hiyo pengine iko sana:

Ushauri:
  1. Weka pesa tu pale unapohitaji au uweke kiasi kidogo tu cha dharura au kwa ajili ya malipo ya bili au kununua vocha.
  2. Umtaarifu ndugu wa karibu kuwa simu yangu ina pesa kiasi fulani lolote likitokea kwangu fatilia urithi.
  3. Makampuni ya simu yaandae taratibu za urithi wa pesa za mtandao huu endapo baya limetokea
Wana JF mpo hapo?
 
nadhani RA anawezakuwa mrithi pekee kwenye matukio kama hayo..........
 
Kama benki zetu hazina huo utaratibu unadhani kampuni za simu zinaweza?

Hivi ni wewe umesema haya ama ni mwingine!
Mkuu benki taratibu zipi na hata kadi au kitabu cha benki kipo! Kuwa na akaunti benki hata mke ama mtoto anajua! Sio sawa na kuwa na hizi tigo, voda na nini cjui.
Hakika huu ni ushauri mzuri!
Big up broda
 
Kama benki zetu hazina huo utaratibu unadhani kampuni za simu zinaweza?

hakuna kitu kama hicho..pindi unapokufa au kufunga akaunti yako lazima benk wapewe taarifa nataratibu za mshiko wako znafuata kuhusiana na tigo na m-pesa na wao wanataratibu zao.
Tatizo ni moja watz wengi huwa hatuna utaratibu wakuso kanuni na sheria za vitu ni hayo tu.
 
Ushauri mzuri,kwa wanaotumia zap,m-pesa au tigo pesa kama benki,wanakosea zle zituaisidie 2 kuharakisha huduma.
 
safi umefikiria jambo muhimu sana,maana watu wengi siku hizi wamefanya mpesa,tigo pesa na airtel money ndio benki zao!
 
Hiyo ya kula leo na watoto sina, nitapata ya kuning'iniza hewani? Endeleeni wajameni. Ngoja nijaribu kuzungusha dagaa langu mie manake leo muuza matembele kaniwahi kapu langu bado zito! Wamedoda dagaa.
 
Hiyo ya kula leo na watoto sina, nitapata ya kuning'iniza hewani? Endeleeni wajameni. Ngoja nijaribu kuzungusha dagaa langu mie manake leo muuza matembele kaniwahi kapu langu bado zito! Wamedoda dagaa.


Hii ni kweli nashangaa ina maana mishahara yangu minne iwe kwenye simu?
 
Chereko,

Umesoma ile Customer Registration Form ya M-Pesa?

Kama bado geuza upande wa nyuma kuna maandishi madogo and I think that will answer a lot of your queries

Thanks!
 
nadhani usikurupuke kuwashauri watu kabla hujafanya research. kiujumla nakushauri ufanye utaratibu wa kuzijua hizo m-pesa,tigi,na kdhalika .
huduma yao ni nzuri tu wala haina matatizo sema ukitaka uwe na matatizo utakuwa nayo tuu. wangapi wana acount benki na hakuna yeyote anayejua na akifa inakuwa faida kwa mabenki.???!!!!!
 
Naweza kuzungumza juu ya Mpesa ambayo ndo naitumia mara kwa mara, wao utaratibu uko wazi wa kufuatilia mirathi ya marehemu. Watanzania tujifunze kusoma masharti na taratibu za huduma tunazozitumia kila siku. Binafsi naona M-pesa imeleta revolution kubwa sana kwenye kufanikisha transfer, safety ya vi-saving vidogovidogo pamoja na kusaidiana kwenye dharula za hapa na pale.

Guys siyo siri mabenki yetu yamekuwa very slow kuleta ubunifu katika sekta ya fedha. Leo hii ukipata tatizo na unahitaji pesa kutoka kwa jamaa yako haraka...Mpesa imekuwa ni mkombozi mkubwa. Una save time, ni fast na cost ni reasonable sana!!

Binafsi all small transactions nazifanya kupitia Mpesa such as kutuma allowances za vijana walioko mashuleni, kulipia bills such as Luku, DStv etc, kuwatumia ndugu na jamaa vipocket money vya hapa na pale hata walioko vijijini kabisa ambako hakuna mabenki n.k n.k!!

Last but not least inaepusha kutembea na pesa nyingi mfukoni ambapo unaweza kupoteza ama kuporwa na vibaka.

Kiukweli Mobile pesa zimeleta mapinduzi makubwa sana!
 
urithi kwa benki ni rahisi baada ya kukamilisha taratibu za mirathi bank account access haina tabu sana.wasiwasi wa mtoa mada ni kuhusu kupata inf ya m-pesa akaunti ya marehemu na statement ya account..hata kama zimeandikkwa katika form lakini bado elimu haijatolewa na uwazi haujawekwa
 
kipindi hiki watu wamependa sana kutunza pesa kwenye simu, tena wengi wanatunza kimya kimya pasipo kumwambia mtu yeyote. watanzania tunatabia pale tunapoona mtu katutoka cha kwanza ni kuzima simu simu ya marehemu... HIvi amuoni kua pesa za watanzania wengi zinapote kwenye aya makampuni tofauti na bank? ata kama hujazima simu za marehemu, hujuwi pin namba yake, hujuwi ana pesa kiasi gani......... wakuu amuoni kama kunamapungufu kwenye mobile money?
 
Back
Top Bottom