Ktk harakati za wazee wa znz za kumfungulia mashitaka Rais mstaafu wa jamhuri ya muungano Mh Benjamin Mkapa,yapo masuala mengi na fununu nyinyi zimejitokeza miongoni mwa wananchi wa znz kuhusu nani hasa Mhusika mkuu wa mauaji hayo ya tarehe 26-27 ya 2001.. Miongoni mwa fununu hizo na masuala ambayo yamejitokeza ni haya..
- Je nani mhusika mkuu? - Mwananchi mmoja alisema Mkapa ndio alikuwa Amiri jeshi mkuu na yeye ndie anaehusika na mauaji yale pamoja na kuwa alikuwa yupo nje ya nchi. Afisa mwandamizi mmoja wa serikali ya smz naye alisema ni kweli Mkapa ndie anaehusika kwani tayari alikuwa ameshasaini,na kuacha maagizo yote kuwa ikiwa yatafanyika maandamano basi watu wauawe,na kweli ikafanyika. " Makamu wa Rais Marehemu Dr Omar alikuwa hana wadhifa wa kuamua chochote,kwani tayari amri ilikuwa ishatoka,na hata wakati alipoulizwa baada ya mauaji yale alisema Muulizeni Mkapa atakujibuni" Alisema mdau mwengine.
- Kwanini Makamu wa Rais hakuzuwia amri ile? Baadhi ya wananchi nao walikuwa wakihoji kwanini Makamu wa Rais hakuzuwia amri ile,mwananchi mmoja alisema Marehemu Dr omar alikuwa na uwezo wa kuzuwia amri ile kwa sababu yeye ndie alikuwa anashika nafasi ya urais kwa wakati ule wakati Mkapa alipokuwa nje. Mwengine alisema ni kweli inawezekana Mkapa alitoa amri lkn nani hasa alietekeleza amri? na kwanini atekeleze amri ambayo ni haramu. wananchi wengi hapa walijaribu kumuingiza Makamo lkn wakisema amri emepewa na Rais ila wanahoji iweje atekeleze amri ile?
- Waziri Mkuu alikuwa wapi? Pamoja na kudadisiwa kina Mkapa na Dr Omar lkn baadhi ya watu wengine wao walihoji Sumaye alikuwepo nchini? Mwananchi mmoja alisema je kama alikuwepo kwa nini tusiseme kama yeye ndie muhusika kwani yeye ndie mtendaji mkuu wa serikali,na ukiangalia jeshi lilitumika na polisi ni wa Muungano. mwengine alisema Sumaye anahusika kwa kuwa alitekeleza amari ya bosi wake ili kulinda cheo chake lkn akijua kuwa si amri sihihi.
- Kikwete je? baadhi ya wadau amabao walikuwa ktk vijiwe vya kahawa wanasema amri zote zilikuwa zinatoka kwa Aliekuwa waziri wa mambo nje Mh kikwete. Mnywaji kahawa mmoja alisema hivi,Huyu kikwete ndie anaehusika kwani yeye ndie alikuwa anaelekeza nini la kufanya kwa wakati ule,na ndio maana utaona hivi sasa wanalindana hawa jamaa kwani wote hawa wamehusika. nae mtu mwengine alisema,si unakumbuka maneno ya Mh Rais alivokuja hapa juzi tu akafanya mkutano kibanda maiti alisemaje? alisema tutayalinda mapinduzi yetu kwa njia yoyote na yule atakaechezea mapinduzi atakiona,sasa si unaona kauli zake,huyu kama Mkapa,na huyu ana tabia ya kutafuna huku anapuliza.