Nani Mhusika Mkuu wa Mauaji 2001?

Calipso

JF-Expert Member
Mar 25, 2009
284
15
Ktk harakati za wazee wa znz za kumfungulia mashitaka Rais mstaafu wa jamhuri ya muungano Mh Benjamin Mkapa,yapo masuala mengi na fununu nyinyi zimejitokeza miongoni mwa wananchi wa znz kuhusu nani hasa Mhusika mkuu wa mauaji hayo ya tarehe 26-27 ya 2001.. Miongoni mwa fununu hizo na masuala ambayo yamejitokeza ni haya..


  • Je nani mhusika mkuu? - Mwananchi mmoja alisema Mkapa ndio alikuwa Amiri jeshi mkuu na yeye ndie anaehusika na mauaji yale pamoja na kuwa alikuwa yupo nje ya nchi. Afisa mwandamizi mmoja wa serikali ya smz naye alisema ni kweli Mkapa ndie anaehusika kwani tayari alikuwa ameshasaini,na kuacha maagizo yote kuwa ikiwa yatafanyika maandamano basi watu wauawe,na kweli ikafanyika. " Makamu wa Rais Marehemu Dr Omar alikuwa hana wadhifa wa kuamua chochote,kwani tayari amri ilikuwa ishatoka,na hata wakati alipoulizwa baada ya mauaji yale alisema Muulizeni Mkapa atakujibuni" Alisema mdau mwengine.

  • Kwanini Makamu wa Rais hakuzuwia amri ile? Baadhi ya wananchi nao walikuwa wakihoji kwanini Makamu wa Rais hakuzuwia amri ile,mwananchi mmoja alisema Marehemu Dr omar alikuwa na uwezo wa kuzuwia amri ile kwa sababu yeye ndie alikuwa anashika nafasi ya urais kwa wakati ule wakati Mkapa alipokuwa nje. Mwengine alisema ni kweli inawezekana Mkapa alitoa amri lkn nani hasa alietekeleza amri? na kwanini atekeleze amri ambayo ni haramu. wananchi wengi hapa walijaribu kumuingiza Makamo lkn wakisema amri emepewa na Rais ila wanahoji iweje atekeleze amri ile?

  • Waziri Mkuu alikuwa wapi? Pamoja na kudadisiwa kina Mkapa na Dr Omar lkn baadhi ya watu wengine wao walihoji Sumaye alikuwepo nchini? Mwananchi mmoja alisema je kama alikuwepo kwa nini tusiseme kama yeye ndie muhusika kwani yeye ndie mtendaji mkuu wa serikali,na ukiangalia jeshi lilitumika na polisi ni wa Muungano. mwengine alisema Sumaye anahusika kwa kuwa alitekeleza amari ya bosi wake ili kulinda cheo chake lkn akijua kuwa si amri sihihi.

  • Kikwete je? baadhi ya wadau amabao walikuwa ktk vijiwe vya kahawa wanasema amri zote zilikuwa zinatoka kwa Aliekuwa waziri wa mambo nje Mh kikwete. Mnywaji kahawa mmoja alisema hivi,Huyu kikwete ndie anaehusika kwani yeye ndie alikuwa anaelekeza nini la kufanya kwa wakati ule,na ndio maana utaona hivi sasa wanalindana hawa jamaa kwani wote hawa wamehusika. nae mtu mwengine alisema,si unakumbuka maneno ya Mh Rais alivokuja hapa juzi tu akafanya mkutano kibanda maiti alisemaje? alisema tutayalinda mapinduzi yetu kwa njia yoyote na yule atakaechezea mapinduzi atakiona,sasa si unaona kauli zake,huyu kama Mkapa,na huyu ana tabia ya kutafuna huku anapuliza.
Pamoja na masuala mengine yanayoumiza hivi sasa wananchi wa znz ni sababu ya kutafakari uchaguzi unaokuja kwani kuna habari ambazo zimezagaa znz kuwa baadhi ya viongozi wa Cuf pemba wamekamatwa na jeshi na kupelekwa kambini huku wakioneshwa Silaha nzito nzito na kuambiwa kuwa mnaziona hizi,basi sisi hatupo tayari nyinyi mtugombanishe na mabosi wetu,kwa hiyo hizi tutazitumia safari hii kikamilifu ikiwa hamtaacha kushabikia Cuf.
 
Wacha watumie hata nyuklia kwa Pemba wasahau huko hakuna wanachokiogopa wanasema wanalinda haki yao hivyo kufa kwa ajili ya kuitetea haki yao hawaoni muhali kwani na hao watakaobakia au wanaotekeleza udhalimu huo nao watakufa tu ,hawataishi milele ,hivyo kifo chao kama kimeandikwa kwa ajili ya kutetea nchi yao na uzalendo wao basi hakuna binadamu wa kukiepusha.
 
mhusika mkuu wa mauaji ya 2001 ni aliyekuwa amiri jeshi mkuu wa Tanzania sema ipo siku haki itapatikana. Wanasiasa waiache zanzibar huru na vugu vugu za kuelekea uchaguzi mkuu mwakani sirikali ya muungano ikubali iliua raia wasiokuwa na hatia.
 
hata mimi kwa mawazo yangu ni aliekuwa amiri jeshi mkuu Mr clean..
 
ktk kutafakari hilo,juzi moja limetokea jengine baada ya karibu boti zote kupakia majeshi wakielekea zenji,na baadhi ya meli kupakia silaha nzito nzito pamoja na vifaru,ambapo baada ya kushushwa tu bandarini znz,wananchi waliokuwa karibu na hapo wakishuhudia ushuhswaji huo walizomea saana harakati hizo huku wakikejeli Serikali ya Muungano
 
Muhusika mkuu Mkapa na hamna chochote kitakachofanyika chini ya serikali ya CCM. Zambia wameshindwa kumfunga Chiluba huko na wao wana historia ya kutotaka upuuzi, itakuwa Tanzania?
 
Muhusika mkuu Mkapa na hamna chochote kitakachofanyika chini ya serikali ya CCM. Zambia wameshindwa kumfunga Chiluba huko na wao wana historia ya kutotaka upuuzi, itakuwa Tanzania?
Mkuu, kwa tz haiwezekani nakubaliana na wewe,lkn je mahakama ya kimataifa haitowezekana na wakati tayari mambo yapo njiani?
 
Mhusika mkuu ni Polisi aliyefyatua risasi zikawaua watu. Wamtafute huyo.
 
Mbabe na Mhusika mkuu ni mkapa,alisema muungano hauwezi kuvunjwa kwa namna yoyote ile aliapa kuulinda.Akiwa amiri jeshi mkuu aliamuru matumizi ya nguvu kubwa ya jeshi zenji alikataa msemo usemao wengi wape wakapeleka mamluki wanazenji wakataa.2010 mhusika mkuu atakuwa kikwete kwa mazingira anayoyalea kwani mpaka sasa katuma majeshi ya ulinzi na usalama kuizunguka zenji.Hatutaki kusubiri maafa,tuchukue hatua viongozi waepushe migogoro kama hii iliyowazi......
pengine tutafika..............
 
Sijasema Mahita. Nimesema mhusika mkuu ni yule Polisi aliyefyatua risasi. (Rejea kesi ya Zombe. Aliyeua ni yule aliyefyatua risasi. huyo ndiye wa kutafuta.)
Nimekupata mkuu,lkn wakati kulikuwa na tetesi kuwa Mahita mwenyewe alikuwa akimwaga risasi,wakati akiwa na Chopa yake angani..
 
Mhusika mkuu ni Polisi aliyefyatua risasi zikawaua watu. Wamtafute huyo.

nakubali mkuu, vinginevyo itakuwa kama kesi ya zombe.........mkapa, Dr. Omar, Amani karume ni accessories tu, hakuna aliyefyatua risasi kati yao na kuua...kweli watanzania ni wasahaulifu...
 
Ukweli ni huu... wazanzibari waliuana wenyewe. Mkapa wala hakuagiza mauaji yafanyike. Pale watu wanapoamua kuwakabili polisi na mawe bila kujua kuwa polisi wana risasi kwanza za moto, walikuwa wanafikiria nini? Aliyewaambia wananchi wawapige polisi au wakatae kutii amri, anahusika moja kwa moja na hao si wengine bali viongozi wa CUF. Kama ushindi umeporwa na ushahidi upo si wangefungua kesi mahakamani badala ya kuwa na porojo kuwa tumeshinda na hakuonyeshwi kwamba wameshinda vipi? Mahakamani unaweza ukatoa vielelezo vyote na kuonyesha ukweli wako uko wapi. Hivyo kwa ujumla....watu wamekuwa wakifa wengi tu kwa kupigwa risasi na polisi pale wanapowashambulia polisi..kumbuka mauaji ya mwembachai,n.k.
 
..Mkapa alikuwa nje ya nchi.

..IGP Mahita alikuwa likizo.

..someni ripoti uchunguzi ya Brig.Gen.Hashim Mbita kuhusu mauaji hayo mnaweza kupata majina ya wahusika waliokuwa on the ground wakati vurugu zile.
 
Back
Top Bottom