Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
WAKATI vyama mbalimbali vikijitokeza kuwania nafasi ya Urais, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema hakina papara ya kumtangaza mgombea wa nafasi hiyo mapema kwa kuhofia kuchafuliwa. Kaimu Katibu Mkuu CHADEMA Taifa, Victor Kimesera, ameliambia gazeti hili.
Amesema malengo ya chama hicho si kukurupuka na kumtangaza mapema mgombea, kwanza ni kujipanga ili kuweza kuongeza idadi ya majimbo na madiwani ambao wataweza kuwa nguvu ya kupambana na chama tawala.
Matarajio yetu ni kuongeza nguvu bungeni angalau kufikia robo tatu ya wabunge wote, amesema.
Kimesera amesema kabla ya kuweka wazi jina la mgombea urais, watatangaza majina ya wagombea ubunge na udiwani Agosti 9 na 10, mwaka huu. Amesema ifikapo Agosti 12, mwaka huu wanatarajia kumtangaza mgombea wao wa Urais.
Akifafanua kilichosababisha kuchelewa kuweka hadharani majina ya wagombea hao, amesema si kweli kuwa CHADEMA inasuasua kumtangaza mgombea kama ilivyovumishwa bali wanaendelea kupokea maombi ya wanachama ya kuwania nafasi mbalimbali, na hiyo imetokana na kujitokeza kwa wagombea zaidi ya mmoja katika nafasi moja.
Hata hivyo, kuna hasara na faida ya kuwahi kumtangaza mgombea, lakini kwa upande wetu tumeona hasara ni kubwa kuliko faida kwani anaweza kufuatwa na wapinzani wake na hatimaye kumchafua, amedai.
Akifafanua juu ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kugombea ubunge badala ya nafasi ya urais, amesema wameamua kufuata mfumo wa mataifa makubwa duniani kwa kumteua mgombea ambaye sio mwenyekiti wa chama.
HABARI NDIYO HIYO
Amesema malengo ya chama hicho si kukurupuka na kumtangaza mapema mgombea, kwanza ni kujipanga ili kuweza kuongeza idadi ya majimbo na madiwani ambao wataweza kuwa nguvu ya kupambana na chama tawala.
Matarajio yetu ni kuongeza nguvu bungeni angalau kufikia robo tatu ya wabunge wote, amesema.
Kimesera amesema kabla ya kuweka wazi jina la mgombea urais, watatangaza majina ya wagombea ubunge na udiwani Agosti 9 na 10, mwaka huu. Amesema ifikapo Agosti 12, mwaka huu wanatarajia kumtangaza mgombea wao wa Urais.
Akifafanua kilichosababisha kuchelewa kuweka hadharani majina ya wagombea hao, amesema si kweli kuwa CHADEMA inasuasua kumtangaza mgombea kama ilivyovumishwa bali wanaendelea kupokea maombi ya wanachama ya kuwania nafasi mbalimbali, na hiyo imetokana na kujitokeza kwa wagombea zaidi ya mmoja katika nafasi moja.
Hata hivyo, kuna hasara na faida ya kuwahi kumtangaza mgombea, lakini kwa upande wetu tumeona hasara ni kubwa kuliko faida kwani anaweza kufuatwa na wapinzani wake na hatimaye kumchafua, amedai.
Akifafanua juu ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kugombea ubunge badala ya nafasi ya urais, amesema wameamua kufuata mfumo wa mataifa makubwa duniani kwa kumteua mgombea ambaye sio mwenyekiti wa chama.
HABARI NDIYO HIYO