Nani kafumaniwa

hakunaga zaidi yangu mi na ww, hakunaga.......hahahahaha haka kawimbo kijana yule kajitahidi kukaimba.haya ngoja nirudi ktk mada hucka.kaka mi naomba utuambie wanaJF kwamba huyu mwanamke kwa mara ya kwanza kabisa ulikutana naye wapi.kuna mzee wangu mmoja alishawahi kunieleza kua mahala unapokutana na mwanamke kwa mara ya kwanza mkaanzisha uhusiano inaashiria tabia zenu nyie wote.mfano km mlikutana baa inajulikana hapo what next.pili mi nadhani we unajua sana tabia za huyu bint kuliko cc ndio maana machale yakakucheza wakat ambao ulishaagwa kua analala wakat ukiwa ofisini ukaamua kwenda club na kwa bahat nzuri ulimkuta akijirusha na walatino.ila la mwisho n kwamba km wote ni wa club ni bora mkae muongee kabla ya kuchukua uamuz wa kumwacha coz kwa nyie watu wa club mademu wako ndio hao hao so utajikuta unaacha halafu unakuja kuangukia kwa mtu wa aina hyohyo.ila km we c wa club na umetulia na heshima zako basi PIGA CHINI.
 
Mambo hya club bhana, eti wengine wanaanzia uchumba baada ya kukutana club, siku hizi hakuna ndoa kabisa, full ukicheche
 
uyo sio mwanamke kabisa..,unajua uaminifu ni k2 kikubwa sana.,kuwa makini na uachane nae mara moja.,uyo sio mwanamke wa kuoa ni malaya.,ucpoangalia atakuja kukuua mpk ww..hafaia katka jamii...
 
Mi sidhani kama kuna hoja hapa. Plz usikilize moyo wake; uifikirie roho yako. Kama una moyo mkubwa uliobebwa na mbavu nguvu PIGA CHINI ila kama un moyo mdogo uendelea kuumia kidogokidogo. Qangu napendelea maumivu makubwa ya mara moja.
 
Ni saa kumi na mbili jioni natoka kazini, nampita demu wangu ili nimpeleke kwake na mimi nirudi zangu kwangu.
Mara ananiambia nimpitishe mahala kuna club fulani karibu na kwake akachukue mzigo wake fulani kwa rafiki yake. Nafanya hivyo na tulipofika nje ya hiyo club nikapokea simu inayonilazimu nirudi ofisini. Hivyo tukakubaliane achukue mzigo na aende nyumbani maana mimi narudi ofisini. Nimekaa ofisini mpaka saa mbili usiku, akanipigia simu kuwa ameshalala na akanitakia usiku mwema. Nami nikamweleza kwamba ndo naelekea kwangu. Ila machale yakanicheza ikabidi nipite kwenye ile club, nika-paki gari mbali kidogo, nikaingia ndani ya hiyo club nikaagiza maji na kijichimbia kenye kona fulani ina kagiza.
Mtumeeeeee!!!, baada ya dakika kumi hivi sikuamini macho yangu kumuona demu huyohuyo anaingia akiwa ametinga pedo laini, mapaja yote nje. Akaenda kukaa meza moja walikaa mabrother men na baadhi ya mademu. Kilicho niuma ni brother men mmoja kumpokea kwa busu, wakakaa then demu akawaamemkumbatia huyo brother. kweli roho iliuma kinoma. Nikawaacha waendelee na mishemishe zao, mara wanyanyuke wasindikizane nje, waende kwenye gari kutafuta koti na mengine.
Ulipopigwa mziki wa hakunaga, meza yao wote alinyanyuka na kuanza kusakata rumba. At around saa nne na robo wakawa wameshakolea kilevi. sasa wakati anasakata rumba gafla demu kaniona nikiwa kona nimekaa nami namuangalia. Nguvu ya kucheza iliisha, akaangalia chini kwa aibu, akaja kunifuata. kuja tu nikamzuia asinifuate aendelee na starehe maana mimi sijamuita. then mimi nikaondoka zangu.
sasa najiuliza maswali yasiyo na majibu
1. Kuna haja ya kuendelea naye
2. ananiambia wale ni kaka zake, je kaka kwa staili ile, na alitegemea kulala wapi maana nyumba anayoishi geti linafungwa saa nne kamili.
3. nilikuwa namlipia masomo ya kuendeleza shule yake, je niendelee au ndo mwisho??
4. nyumba anayoishi nailipia mimi maana mimi kwangu nakaa na wadogo zangu na hatujaanza kuishi pamoja, je nitaendelea kulipa


Naomba ushauri,

Chimps
Nimempelekea mama Matesha uzi huu na kumtaka atoe ushauri, akaniuliza huyu aliyeanzisha hii thread ana umri gani?

Bila kumjibu niliporudia hizo bold hapo juu, nikajiondokea zangu kwenda bar. Nilikuwa nimeshamuelewa.
 
Ni saa kumi na mbili jioni natoka kazini, nampita demu wangu ili nimpeleke kwake na mimi nirudi zangu kwangu.
Mara ananiambia nimpitishe mahala kuna club fulani karibu na kwake akachukue mzigo wake fulani kwa rafiki yake. Nafanya hivyo na tulipofika nje ya hiyo club nikapokea simu inayonilazimu nirudi ofisini. Hivyo tukakubaliane achukue mzigo na aende nyumbani maana mimi narudi ofisini. Nimekaa ofisini mpaka saa mbili usiku, akanipigia simu kuwa ameshalala na akanitakia usiku mwema. Nami nikamweleza kwamba ndo naelekea kwangu. Ila machale yakanicheza ikabidi nipite kwenye ile club, nika-paki gari mbali kidogo, nikaingia ndani ya hiyo club nikaagiza maji na kijichimbia kenye kona fulani ina kagiza.
Mtumeeeeee!!!, baada ya dakika kumi hivi sikuamini macho yangu kumuona demu huyohuyo anaingia akiwa ametinga pedo laini, mapaja yote nje. Akaenda kukaa meza moja walikaa mabrother men na baadhi ya mademu. Kilicho niuma ni brother men mmoja kumpokea kwa busu, wakakaa then demu akawaamemkumbatia huyo brother. kweli roho iliuma kinoma. Nikawaacha waendelee na mishemishe zao, mara wanyanyuke wasindikizane nje, waende kwenye gari kutafuta koti na mengine.
Ulipopigwa mziki wa hakunaga, meza yao wote alinyanyuka na kuanza kusakata rumba. At around saa nne na robo wakawa wameshakolea kilevi. sasa wakati anasakata rumba gafla demu kaniona nikiwa kona nimekaa nami namuangalia. Nguvu ya kucheza iliisha, akaangalia chini kwa aibu, akaja kunifuata. kuja tu nikamzuia asinifuate aendelee na starehe maana mimi sijamuita. then mimi nikaondoka zangu.
sasa najiuliza maswali yasiyo na majibu
1. Kuna haja ya kuendelea naye
2. ananiambia wale ni kaka zake, je kaka kwa staili ile, na alitegemea kulala wapi maana nyumba anayoishi geti linafungwa saa nne kamili.
3. nilikuwa namlipia masomo ya kuendeleza shule yake, je niendelee au ndo mwisho??
4. nyumba anayoishi nailipia mimi maana mimi kwangu nakaa na wadogo zangu na hatujaanza kuishi pamoja, je nitaendelea kulipa


Naomba ushauri,

Chimps

Pole mzeya, hapo kwenye rangi, hivi kumbe bado kuna wanaume wa karne hii wanafanya hivyo vitu vyote kwa mwanamke ambaye haishi naye, mwambie amlete huyo kaka mbele yako, amtambulishe kwamba huyu ni shemeji yako, alikasirika kweli alivyotuona siku zile club, nimekuleta mbele yake ili nimthibitishie kuwa wewe ni kaka yangu, ingawa pia bado haitoshi kumwamini mia kwa mia, maana unaweza ukamwacha huyu akaja mwingine vituko vikawa afadhali vya huyu. Ingekuwaje kama angekuazima gari siku moja, halafu unakuta kaka ndo anaendesha, halafu ni jamaa yake. Yaani mapenzi haya mi sijui. Ingekuwa vipi kama watu ambao hawajaoa/olewa maisha yao ya kimapenzi wafanye kama ile nyimbo ya Ali Kiba, ya poa, poa, mapenzi ya kugandana yalikuwa zamani.

Eeee Mwenyezi Mungu naomba umsaidie baba "D" wangu asitapakanye mali za ndani kwa kuwapa wanawake, maana siwezi jua labda na yeye ni miongoni mwao. Kwa aliyefanikiwa kusoma mchango wangu aseme AMEEEEEEEEEEEEEEEEEEEN.
 
siku zote njia ya muongo ni fupi; hivi ulipomsindikiza huyo demu kuchukua 'mzigo' hapo club, ndiyo alienda kumcheki huyo jamaa yake nini? halafu alipoona ratiba yako iko favourable, akaamua ale bata fully
 
ikiwa ameanza kukudanganya wakati huu je mkimuoa unadhani ataacha tabia hiyo? huyo ni changudo Mungu kaamua kuonesha ili asije akakuletea maradhi bure ,. huyo anakutumia kama wasichana wa chuo kikuu ambao nasikia wengi wao wana wanaume hadi watano wenye mgawanyo ufuatao.

1. mwanaume mmoja kwa ajili ya vocha;
2. mwanaume wa pili kwa ajili ya nguo;
3. mwnaume wa tatu kwa ajili ya masomo hususani huwa mwenye uwezo mzuri darasani ili awe anamfundihsa na kumsaidia kujibu mtihani anaposhindwa;
4. mwanaume wa nne kwa ajili ya kumtoa out- kama huyo uliyemkuta na demu wako;
5. mwanaume wa tano ni yule anyempenda kwa dhati; anayejisikia kuwa naye

hivyo wewe na wenzake wanne mnapangiwa ratiba ya kuonana naye

Nakushauri achana naye , mwombe Mungu atakupa Mtu mwaminifu asiyenia makuu



kila la heri

sasa hizo kashfa usitoe ushauri wako kwa kutusi wengine mana hao wasichana wa chuo kikuu uliwaona wapi wakifanya huo uovu?ina mana huyo dada hapo sasa ni mwana chuo?...ni tabia ya mtu tu hiyo cha mana chimps aendelee na mambo yake tu hapo sio ridhiki
 
no need kuedelea na huyo dogo! sio muaminifu na siamin kama anaweza ku change coz it seems hata msaada unaompa hauthamini! ila 2012 DUNIA YAKO, CHAGUO LAKO.
 
unauliza nini hapa brother sioni swali naona majibu. Au mpaka ukute kitu juu ya kitu ndo uamini. Ni juu yako
 
Kwa koment zako mkuu kama huyu jamaa hajakuelewa naomba nishauri kuwa kwanza kama ni muumini wa dini yeyote aende akafanyiwe maombi au dua ya kuweza kumuepusha na huyo ibilisi aliyemvaa huyo binti na maombi au dua yenyewe yawe ya kumuachanisha nae, kama sio muumini basi akawaone wataalam wamsaidie dawa za kumfumbua macho na akili ili aweze kuachana na huyo binti! Kiukweli kwa mtu ambaye yuko timamu au mzima kabisa asingetuomba ushauri wana fj badala yake angekuwa anatusimulia jinsi alivyo mtoa nduki (alivyo mtaliki hata kama hakuwa amemuoa) huyo dada kwa mambo aliyomfanyia, then sisi tungekuwa tunafanya kumpongeza tu na si kumshauri!
 
Kwa koment zako mkuu kama huyu jamaa hajakuelewa naomba nishauri kuwa kwanza kama ni muumini wa dini yeyote aende akafanyiwe maombi au dua ya kuweza kumuepusha na huyo ibilisi aliyemvaa huyo binti na maombi au dua yenyewe yawe ya kumuachanisha nae, kama sio muumini basi akawaone wataalam wamsaidie dawa za kumfumbua macho na akili ili aweze kuachana na huyo binti! Kiukweli kwa mtu ambaye yuko timamu au mzima kabisa asingetuomba ushauri wana fj badala yake angekuwa anatusimulia jinsi alivyo mtoa nduki (alivyo mtaliki hata kama hakuwa amemuoa) huyo dada kwa mambo aliyomfanyia, then sisi tungekuwa tunafanya kumpongeza tu na si kumshauri!
 
Huyo alikuwa kakufanya ATM yake na ungeona matokeo yake! Hivi wanaume nani kawa ambia kuwa kulipia nyumba na masomo na pesa za matumizi ndio kumfanya mwanamke akupende zaidi! Ukipata mwanamke wa design hiyo ujue huyo ni mchimba chumvi tu atakutumia halafu atakuacha na utashangaa!
 
Asilimia 99 ya Wabeijing wamemtetea mwenzao................Kweli umoja ni nguvu.........LOL
Mkuu Kusamehe baada ya fumanizi ni jambo linalohitaji subira ya hali ya juu.............Umepokea ussauri mwingi sana hapa na mauzoefu kibao.................Mimi nasema akili mukichwa. Uamuzi unao wewe maana wewe ndio unamjua zaidi huyo mpenzi wako tofautu na sisi wachangiaji.
Mimi nakuomba umpe nafasi nyingine, kwani huenda alipitiwa na shetani..........
 
huyo hafai kua mke, wewe kakufanya kitega uchumi chake, wa kulipia skul fees, kodi ya nyumba na mengine yote, lakini starehe apewa mwingine. achana nae na songa mbele. atakusumbua, ikiwa hawezi kutambua fadhila zako kwa sasa, ukimuoa ndio atatambua? kwanza kakudanganya kuwa kalala kumbe yuko mtaani anavinjari, wanini mtu kama huyo, mwongo mzoefu, jiulize kesha kudanganya mangapi?
 
Back
Top Bottom