sasa wewe unampotosha mwenzio,yeye nae alienda kuwinda club soma heading ya thread. WAMEFUMANIANA.piga chini huyo
sasa wewe unampotosha mwenzio,yeye nae alienda kuwinda club soma heading ya thread. WAMEFUMANIANA.piga chini huyo
Asipolielewa hili, hatoelewa kitu kingine chochoteMchumba hafumaniwi!!!!
hana ubavu wa kuacha......angekuwa na uamuzi huo saaa hizi ingekuwa siku nyingiiiiiiiii kila mtu kivyake.usikilize moyo wako,kwani wewe ndio unaeweza kutoa msamaha,na ndio ulieona kwamacho yako vitendo alivyovifanya, kama umeona anastahili kusamehewa sawa ....
kitu gani kilikufanya hadi ukapatwa na machale ukaamua kurudi pale club? humwamini mtu wako??
Ni saa kumi na mbili jioni natoka kazini, nampita demu wangu ili nimpeleke kwake na mimi nirudi zangu kwangu.
Mara ananiambia nimpitishe mahala kuna club fulani karibu na kwake akachukue mzigo wake fulani kwa rafiki yake. Nafanya hivyo na tulipofika nje ya hiyo club nikapokea simu inayonilazimu nirudi ofisini. Hivyo tukakubaliane achukue mzigo na aende nyumbani maana mimi narudi ofisini. Nimekaa ofisini mpaka saa mbili usiku, akanipigia simu kuwa ameshalala na akanitakia usiku mwema. Nami nikamweleza kwamba ndo naelekea kwangu. Ila machale yakanicheza ikabidi nipite kwenye ile club, nika-paki gari mbali kidogo, nikaingia ndani ya hiyo club nikaagiza maji na kijichimbia kenye kona fulani ina kagiza.
Mtumeeeeee!!!, baada ya dakika kumi hivi sikuamini macho yangu kumuona demu huyohuyo anaingia akiwa ametinga pedo laini, mapaja yote nje. Akaenda kukaa meza moja walikaa mabrother men na baadhi ya mademu. Kilicho niuma ni brother men mmoja kumpokea kwa busu, wakakaa then demu akawaamemkumbatia huyo brother. kweli roho iliuma kinoma. Nikawaacha waendelee na mishemishe zao, mara wanyanyuke wasindikizane nje, waende kwenye gari kutafuta koti na mengine.
Ulipopigwa mziki wa hakunaga, meza yao wote alinyanyuka na kuanza kusakata rumba. At around saa nne na robo wakawa wameshakolea kilevi. sasa wakati anasakata rumba gafla demu kaniona nikiwa kona nimekaa nami namuangalia. Nguvu ya kucheza iliisha, akaangalia chini kwa aibu, akaja kunifuata. kuja tu nikamzuia asinifuate aendelee na starehe maana mimi sijamuita. then mimi nikaondoka zangu.
sasa najiuliza maswali yasiyo na majibu
1. Kuna haja ya kuendelea naye
2. ananiambia wale ni kaka zake, je kaka kwa staili ile, na alitegemea kulala wapi maana nyumba anayoishi geti linafungwa saa nne kamili.
3. nilikuwa namlipia masomo ya kuendeleza shule yake, je niendelee au ndo mwisho??
4. nyumba anayoishi nailipia mimi maana mimi kwangu nakaa na wadogo zangu na hatujaanza kuishi pamoja, je nitaendelea kulipa
Naomba ushauri,
Chimps
Samehe mara sabini msonge mbele na maisha. Ukiamua kumuacha utaacha wangapi?