MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Baada ya kifo cha Waziri wa fedha Dk. william mgimwa mengi yamesemwa ndani na nje ya jukwaa letu la JF. Kwa wastani threads nyingi zimeonyesha kuwa wengi wamehuzunishwa na kifo chake jambo linaloonyesha kuwa Marehemu alitimiza wajibu wake.
Hata hivyo tumesahau wajibu wetu wa kutoa maoni yetu juu ya mtanzania atakayeweza kutosha kuziba pengo lake bila kujali kuwa Mtanzania huyo atatoka bungeni (bunge) au nje ya bunge (asiye bunge) ambaye akitosha atateuliwa kuwa bunge. Tushiriki kutabiri/kubashiri kama watanzania si kama watoa maamuzi.
Wengi wetu tutapenda kufanya dhihaka/mzaha au kuipuuza thread hii. Taifa hili ni letu sote ubashiri wetu hapa JF kama utakuwa makini unaweza kushabihiana na watoa maamuzi ndilo tunalojaribu kulifanya hapa. Tunataka kuona kama tunaowawazia ndio watakaochukua mikoba ya Mgimwa?
Hata hivyo tumesahau wajibu wetu wa kutoa maoni yetu juu ya mtanzania atakayeweza kutosha kuziba pengo lake bila kujali kuwa Mtanzania huyo atatoka bungeni (bunge) au nje ya bunge (asiye bunge) ambaye akitosha atateuliwa kuwa bunge. Tushiriki kutabiri/kubashiri kama watanzania si kama watoa maamuzi.
Wengi wetu tutapenda kufanya dhihaka/mzaha au kuipuuza thread hii. Taifa hili ni letu sote ubashiri wetu hapa JF kama utakuwa makini unaweza kushabihiana na watoa maamuzi ndilo tunalojaribu kulifanya hapa. Tunataka kuona kama tunaowawazia ndio watakaochukua mikoba ya Mgimwa?