Nani anambeba Profesa Kapuya?

Well said Zak. Mimi ni mzaliwa wa na natoka jimboni mwake, yanayoitwa ''maendeleo" jimboni kwake ni umasikini mkubwa wa wananchi wake ambao husubiri tu hongo na T-shirts, capello (bila bottoms) wakati wa uchaguzi. Sure, kuna umeme sasa na huduma za simu za mkononi -- huduma ambazo ni wachache mno (0.000001%) wa wakazi wanafaidi. Lakini haya yametokana zaidi na taasisi husika kupanua biashara zao muliko jitihada zake.
 
Tushike lipi?mara kaoa nyumba moja na JK.MARA ALILIA SANA WAKATI WA MSIBA WA DR.OMAR ina maana alilia kuwa refarii wake kafariki,hapo hapo unauliza nani anambeba Professor Kapuya?mara anaonekana sana Mlingotini,jee huko Mlingotini ndio kuna mbeba?

nadhani nyinyi na huyu Mwandishi aliyeandika huko Mwanahalisi wote mnazua tu.Mara alimconvince JK kwenye Kampeni,mara Uprofessor na dini yake.vyote mnaongea ni pumba tupu.
Mwandishi wa makala ile kawa straight. Shida ni shule yako ndogo na uelewa mdogo pia.
 
dada haitwi kapuya ni professor kapuya.mwandishi mzima unashindwa kuweka hiyo title?

simba,professor kapuya na malima hawajafeli.nenda jimboni kwa professor watu wake ndio watakwambia kama amefeli au laa,hizi hapa ni propaganda na uchaguzi.mwandishi mwenzio aliyeandika ameshindwa kufikisha ujumbe,

mara anamtaja dr.omar na kilio cha kapuya ina maana dr.omar ndio alikuwa refarii wake?kama alilia sana kwa refarii wake kufariki mbona anapeta?refarii wake ni elimu yake.nawe kasome uwe professional,vinginevyo utaendelea kuwa kanjanja tu.


Kanda2 wasomi wa aina ya kapuya ndio wametufikisha hapa tulipo. Nahisi ni kati ya wasomi waliobebwa tu politically na ukisoma cv yake lazima ukute anasema alikuwa fulani fulani katika chama cha mafisadi Tanzania. Hii nadhani ndio imemfikisha hapa. Na aina hii ya wasomi ndio wameiweka pabaya nchi hii.
 
Kanda2 wasomi wa aina ya kapuya ndio wametufikisha hapa tulipo. Nahisi ni kati ya wasomi waliobebwa tu politically na ukisoma cv yake lazima ukute anasema alikuwa fulani fulani katika chama cha mafisadi Tanzania. Hii nadhani ndio imemfikisha hapa. Na aina hii ya wasomi ndio wameiweka pabaya nchi hii.

Nadhani umepigilia msumari kichwani. Nchi hii imejaliwa na watu wa ajabu kabisa -- watu wanaoamini giza ndiyo mwanga, na kinyume chake! Watu wanaotetea uovu wa waziwazi! Kama Muungwana wetu, watu wasiojua sababu ya nchi hii kuwa masikini! Ni usenge-senge tu ndiyo unaoendelea hapa nchini!
 
Soma vizuri rafiki yangu - hakuna mahala wachangiaji wamesema Prof Kapuya kafel ubunge. Kinachosemwa hapa ni kwamba kafeli uwaziri. Inawezekana kafanya vizuri jimboni mwake, lakini nahisi hiyo ni kutokana na kuwa waziri, tena katika wizara nono -- kama vile hii ya usitawi wa jamii ambayo mifuko yote ya hifadhi za jamiui (pension funds) iko chini yake. Tusisahau kwamba ile kashfa ya magodown ya Ubungo ilifanyika wakati yeye ndiyo waziri wa wizara hiyo.

Mimi nafikiri angekuwa ni mbunge tu bila ya uwaziri, asingeweza kufanya chochote jimboni kwake.

Yeah -- nakumbuka ile kashfa iliyomhusu Manji na kupigiwa debe na Mzee wetu Mengi. Sijui iliishaje ile! Bila shaka Profesa alivuta mzigo mnene katika deal ile
 
Miaka michache nyuma jimboni I mean kijijini kwake kulikuwa HAKUNA UMEME. Anachoeza yeye huyu 'Prof.' ni kudanganya watu kuhusu ajira mil 1 na kumdanganya Rais kuhusu wafanyakazi, na kumiliki BENDI YA MUZIKI WA DANSI. Huyu ndo 'profesa' na waziri ktk sirikali yetu tukufu, halaf eti tunaketi kitako hapa tunasubiri miracle workers like this clown eti watuongoze kufikia nchi ya maziwa na asali..looool
 
Professor asiyekuwa na kitu kichwani professor gani huyu?
Unajua kisomo kina maana pale kinapokuwa apllicable kwa manufaa ya jamii lakini ukisoma ukawa kama mtu ambaye hakwenda skuli wewe msomi gani bwana? Ndio maana nchi haiendi. Na hapa ndipo watanzania tumeliwa kwa kupigia magoti wasomi uchwara hawa simply kwa sababu eti anaitwa professor. Wanavijiji wakisikia tu professor wanaweka tick kumbe ni professor ambaye kichwa kiko wazi. aghrrrrrrrrrr
 
Pedesheeee Juma Kapuya , Mfadhili na mwenyekiti wa Akudo impact .

Nakala kwa Chakaza
 
Soma vizuri rafiki yangu - hakuna mahala wachangiaji wamesema Prof Kapuya kafel ubunge. Kinachosemwa hapa ni kwamba kafeli uwaziri. Inawezekana kafanya vizuri jimboni mwake, lakini nahisi hiyo ni kutokana na kuwa waziri, tena katika wizara nono -- kama vile hii ya usitawi wa jamii ambayo mifuko yote ya hifadhi za jamiui (pension funds) iko chini yake. Tusisahau kwamba ile kashfa ya magodown ya Ubungo ilifanyika wakati yeye ndiyo waziri wa wizara hiyo.

Mimi nafikiri angekuwa ni mbunge tu bila ya uwaziri, asingeweza kufanya chochote jimboni kwake.
ametajwa pia kwenye mabasi ya mwendokasi , akishirikiana na Kisena , Idd Simba , Masaburi na mwingine namhifadhi kwa sasa , ni mtu anayejipigia hela za nchi hii kimya kimya , wanasema kwenye kuhonga akina dada hana hiyana , kumpa mtu nyumba au benz ni kitu kidogo sana
 
ametajwa pia kwenye mabasi ya mwendokasi , akishirikiana na Kisena , Idd Simba , Masaburi na mwingine namhifadhi kwa sasa , ni mtu anayejipigia hela za nchi hii kimya kimya , wanasema kwenye kuhonga akina dada hana hiyana , kumpa mtu nyumba au benz ni kitu kidogo sana
Kwa umri huo kwani aliruka stage

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom