Nani anaandikaga subtitles za movies za Bongo?

carmel

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
2,836
262
Mwenzenu sikuwahi kuwa na mazoea ya kuangalia movie zetu za hapa nyumbani kwa maana mara nyingi huwa actors wana overdo hadi nikawa naboreka. sasa last weekend kwa kufuata ushabiki wa watoto nikakaa kuangalia, kwa kweli nilikuwa shocked na nikawa nashindwa kuelewa. Kwani ni nani anayewaandikia zile subtitles za kiingereza, halafu it seems ni myu mmoja ndiye huwa anapelekewa kwa jinsi zilivyo.

Ni aibu jamani, kama bado hamjafikia level hiyo ya lugha, acheni tu, wekezeni zaidi kwenye kiswahili basi ieleweke tu kwamba movie ni ya kiswahili. Au kama mnataka mpate soko la kimataifa, hebu mu-invest sana mpate professionals wanaoweza kuwaandikia lugha ya kueleweka, otherwise mnajiabisha na kuiabisha nchi hii, can you imagine unaeangalia movie ndo unaona aibu kwa niaba yao. Maana ile lugha inayoandikwa pale si english, bali direct translation from kiswahili inaishia kuwa pigini, au mnajaribu kutengeneza lugha ingine? Mi sijaelewa jamani.

Kama vipi muwe mnaniletea japo nina uelewa mdogo wa hii lugha naamini i can do better than that. Ni ushauri tu, najua kina Kanumba sijui Ray huwa mnapita humu, next time kwenye baraza lenu la wasanii hebu wekeni hii kama agenda, naamini wapo watu kibao ambao hata kwa kuvolunteer wanaweza ku edit na kusaidia kutoa lugha inayoeleweka.
 
Mama kama unavyoshangaa ndio ninavyoshangaa sijui nani anafanya kazi hii kweli.
Kwani kwenye ulimwengu wa movie Tanzania hakuna actors walionda shule ????
 
[, halafu it seems ni myu mmoja ndiye huwa anapelekewa kwa jinsi zilivyo.
Unachosema ni kweli ila umekosea pia, hizo filamu zinatoka kama 50 mpaka 100 kwa mwezi mtu mmoja atazifanyaje?mimi ni mmojawapo wa wanaofanya nafanya za game 1st quality, kama vile village pastor, fake smile nk lakini siamini kwamba zote ni mbovu kiasi hicho kuna vizuri na vibaya just like vitu vingine, penye credit mjaribu ktoa
 
... huwa nami hutumbukia kwenye mtego wa kuangalia DSTV kwenye channel 114, 115 na 116. Humo huwa nakumbana na Movie za kibongo... Hata kama movie iwe nzuri namna gani, nikiona subtitle mbovu nabadilisha channel fasta.

hawa jamaa wajaribu kuinvest kwenye wakarimani (translators) nahisi wako wengi tu. Movie industry ina upana mkubwa wajamani... Tusipende kuvuna bila kupanda.

Tunapata aibu wa Tz kwakweli. Nadhani BASATA wanahitaji kuingilia kati hapa! Vinginevyo hili suala litakuwa na "multiplier effect" kwenye sekta nyingine ambazo watanzania tunajumuishwa na mataifa mengine.
 
hawa wasanii wetu wanajifanya kila kitu.wao wenyewe wanashoot, wanaedit,na kuandika subtilles wenyewe sasa imagine wakati wao wenyewe english ndio hivyo tena cha maimuna.....so madudu na madudu yataendelea.baraza la kiswahili ndilo lenye jukumu la kukemea hili
 
Mi huwa siangalii chuya hizo...........movie za Bongo ujinga mtupu...bora hata kusikiliza maigizo ya akina mzee Jangala na Onyango
 
hahaha ni kweli jamani, mimi sio mtazamaji mzuri wa hizi movie zetu za kibongo lkn ukweli ni kwamba hizi movie ni balaa I mean ni hatari kwa maendeleo nasema hivyo cuz cjui watoto wetu wakiangalia wanajifunza nini zaidi ya kuvaa uchi, kingine ni kwamba matukio mengi yaliyomo ktk filamu hizi hayaendani na uhalisia uliopo ktk jamii zetu, na kikubwa kuliko yote nadhani wanaandaa bajet finyu ili wapate wabakiwe na donge nono kwa ajili ya matanuzi, tatizo linakuja hata hao wanaodirect hizo filamu pia nao ni 0! km wameenda shule hawawezi kukubali kudirect hiki ambacho tunakiona nakukijadili kila leo. Hata hivyo napenda kuwaambia kwamba wasikate tamaa kwani mwanzo ni wowote ni mgumu ila wasibaki nyuma ktk kujifunza km kweli wanataka maendeleo na wameamua kufikisha ujumbe kwa njia ya sanaa.
 
Ndugu yangu mimi hizo movie siziangaliagi kabisa. Toka nione michezo yao ya kuigiza mibovu mibovu, below standard na sijui niseme........sipotezi muda wangu hata. Kama niko aido bora nikalale, kupumzisha mwili wangu kulikoni hayo mavituko utakayo yaona humo kwenye hizo movie.
 
Tafsiri ya Kiswahili kwenda Kiingereza inaonekana huwa ni kama ngumu hata kwa wasomi wa Kiswahli wa BAKITA...ukichukua Kamusi ya Kiswahili kwa Kiingereza ya TUKI utata mwingi.....tunafikiri kiswahili ili kutamka au kuandka kiingereza (UKANUMBA).
 
Nani anaandikaga subtitles za movies za Bongo?

MASANILO NA XSPIN
 
Wangekua wanaishia kwenye subtitles ingekua afadhali. Kuna igizo moja linaitwa The image Ray anamwambia binti, ''naomba tuwe just a friends'' binti nae ''just a friends ehhh''?. Sasa hiyo 'a' sijui ni ya nn. Na kwanini walazimishe kuonge kiingereza wasichoweza kukinyoosha wakati angesema '' naomba tuwe marafiki tu'' ingeleta maana na wasingejiaibisha.

Na hizi comment sijui hua hawasomi au labda wanapuuza, either way wakinamama wa uswahilini wanaofagilia maigizo yao ipo siku nao watajanjaruka ndo hapo watakapokosa soko.
 
sure ni tatizo kweli...well wadau ...kuna mbili nimezimaliza majuzi za game 1st quality..the hero of the church na saturday morning i think zipo sokoni na hazina subtitles so nilizofanya ni za kwenda magic plus...hope tofauti itaonekana...
 
[, halafu it seems ni myu mmoja ndiye huwa anapelekewa kwa jinsi zilivyo.
Unachosema ni kweli ila umekosea pia, hizo filamu zinatoka kama 50 mpaka 100 kwa mwezi mtu mmoja atazifanyaje?mimi ni mmojawapo wa wanaofanya nafanya za game 1st quality, kama vile village pastor, fake smile nk lakini siamini kwamba zote ni mbovu kiasi hicho kuna vizuri na vibaya just like vitu vingine, penye credit mjaribu ktoa

basi kama wewe ndo unaandikaga hongera, lakini hakuna haja ya haraka unapokuwa unataka kufanya kazi inayoonekana na watu katika ulimwengu huu, kama lengo ni kupata market ya afrika fanyeni kazi ya maana tusiishie kufanya vitu vya aibu na watanzania wote kuonekana majuha. Hizo haraka za kuproduce movie 100 kwa mwezi ndio lack of seriousness na ndo maana badala ya kwenda mbele mnarudi nyuma na kupoteza market. Na hata kama mnataka kuproduce movie nyingi, outsource kazi hizo kwa watu tofauti wenye uelewa wa lugha kwaa hali ya juu wafanye kazi ya maana.
 
Mi huwa siangalii chuya hizo...........movie za Bongo ujinga mtupu...bora hata kusikiliza maigizo ya akina mzee Jangala na Onyango

hahaaa laaziz!!!

Nani anaandikaga subtitles za movies za Bongo?

MASANILO NA XSPIN

my my my!!!

Wangekua wanaishia kwenye subtitles ingekua afadhali.
Kuna igizo moja linaitwa The image Ray anamwambia binti,
''naomba tuwe just a friends'' binti nae ''just a friends ehhh''?
sasa hiyo 'a' sijui ni ya nn.Na kwanini walazimishe kuonge kiingereza
wasichoweza kukinyoosha wakati angesema '' naomba tuwe marafiki tu''
i

nyie watu mmenichekesha kweli, n akunipa sababu ya kuendelea kusubiri msafara wa WEF upite ndo niondoke....lol!!!
 
[, halafu it seems ni myu mmoja ndiye huwa anapelekewa kwa jinsi zilivyo.
Unachosema ni kweli ila umekosea pia, hizo filamu zinatoka kama 50 mpaka 100 kwa mwezi mtu mmoja atazifanyaje?mimi ni mmojawapo wa wanaofanya nafanya za game 1st quality, kama vile village pastor, fake smile nk lakini siamini kwamba zote ni mbovu kiasi hicho kuna vizuri na vibaya just like vitu vingine, penye credit mjaribu ktoa

kwenye red mnakimbilia nini?? its about quality and not quantity!!! ulafi wa kipuuzi ndo unawafanya muishi hapa mlipo......'just a friends'

kwenye red nikiona panastahili credo ntatoa!!!
 
Sio subtitles tu...hata jinsi wanavyo-perform ni aibu..yaani hakuna uhalisia kabisa kama m2 umezoea kuangalia movie za hollywood hizi za kibongo hutaweza maana utaona hakuna ki2 kabisa...yaani mtu ana-potray scenes tofauti na inavyokuwa hakuna element ya reality kabisa..........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom