Nani Alitoka na Akatoka Bunge la Katiba?

1954tanu

JF-Expert Member
Jul 19, 2013
1,038
487
Kwenye moja ya kipindi cha Meza ya Busara kinachorushwa na WAPO radio wiki hii nili msikia mmoja kati ya wachangiaji akisema UKAWA na CCM hakuna aliyebaki bungeni wote walitoka. Mchangiaji huyo alisema hayo akichangia kwenye mada iliyokuwa ikisema," UKAWA wametoka, Je! Nini Kifanyike?".

Mchangiaji huyo alisema CCM ndio walioanza kutoka pale walipotoka nje ya mjadala kwa mujibu wa sheria iliyowaweka pale. Alisema ukawa wao waliamua kutoka kabisa nje ya jengo la bunge. Nikiyaangalia mawazo ya huyu mtu ni wazi kuwa CCM walishatoka siku nyingi kwenye njia kuu, walichepuka kitambo tangu Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipoanza kukusanya maoni. CCM ilikwaandaa watu na kuwaambia ni nini cha kuchangia.

Wakati wa Mabaraza ya Katiba hao CCM hawakujificha walionesha wazi kwamba wamechepuka. Kwa mantiki hiyo, UKAWA ndio walikuwa bungeni wakati CCM wamechepuka. Ukweli huu unajidhihirisha hata katika namna ya uchangiaji wa hoja. UKAWA walionesha dhahiri kwamba waliwafumbua macho na masikio wananchi waliowengi ambao hawakuwa wameisoma rasimu ya pili iliyowasilishwa. Na ni kutokana na hoja za UKAWA wananchi waliowengi wakaanza kuelewa katiba ni nini na inasema nini. Kwa kuwa CCM walikuwa wamechepuka basi hata hoja zao hazikuwa na mashiko. Na wakaamua kuzitia vibwagizo vya mipasho, matusi, kejeri na kila aina ya udhalimu walioweza kuuonesha.

Hata hivyo, kupitia radio WAPO siku hiyo watu waliochangia wengi takriban 80% waliunga mkono UKAWA kutoka nje. Wakasisitiza UKAWA wasirudi isipokuwa tu kama BMK litajadili rasimu iliyowasilishwa bungeni.
 
Ni kweli kabisa mkuu kwenye hoja yako...na ikiangalia lengo kuu la ukawa kutoka ni baada ya kuona hawadiscuss tena kilicho wapeleka pale..kwa hiyo kuingia kule ndani ilikua ni kupoteza muda tu..maana unakaa na watu wanaomdiscuss warioba badala ya katiba..
 
Kwenye moja ya kipindi cha Meza ya Busara kinachorushwa na WAPO radio wiki hii nili msikia mmoja kati ya wachangiaji akisema UKAWA na CCM hakuna aliyebaki bungeni wote walitoka. Mchangiaji huyo alisema hayo akichangia kwenye mada iliyokuwa ikisema," UKAWA wametoka, Je! Nini Kifanyike?".

Mchangiaji huyo alisema CCM ndio walioanza kutoka pale walipotoka nje ya mjadala kwa mujibu wa sheria iliyowaweka pale. Alisema ukawa wao waliamua kutoka kabisa nje ya jengo la bunge. Nikiyaangalia mawazo ya huyu mtu ni wazi kuwa CCM walishatoka siku nyingi kwenye njia kuu, walichepuka kitambo tangu Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipoanza kukusanya maoni. CCM ilikwaandaa watu na kuwaambia ni nini cha kuchangia.

Wakati wa Mabaraza ya Katiba hao CCM hawakujificha walionesha wazi kwamba wamechepuka. Kwa mantiki hiyo, UKAWA ndio walikuwa bungeni wakati CCM wamechepuka. Ukweli huu unajidhihirisha hata katika namna ya uchangiaji wa hoja. UKAWA walionesha dhahiri kwamba waliwafumbua macho na masikio wananchi waliowengi ambao hawakuwa wameisoma rasimu ya pili iliyowasilishwa. Na ni kutokana na hoja za UKAWA wananchi waliowengi wakaanza kuelewa katiba ni nini na inasema nini. Kwa kuwa CCM walikuwa wamechepuka basi hata hoja zao hazikuwa na mashiko. Na wakaamua kuzitia vibwagizo vya mipasho, matusi, kejeri na kila aina ya udhalimu walioweza kuuonesha.

Hata hivyo, kupitia radio WAPO siku hiyo watu waliochangia wengi takriban 80% waliunga mkono UKAWA kutoka nje. Wakasisitiza UKAWA wasirudi isipokuwa tu kama BMK litajadili rasimu iliyowasilishwa bungeni.


Katika maisha yangu, sijawahi kuona chama cha kipuuzi kama CCM! Sidhani kama nitaona kama hicho mpaka kufa kwangu. Kwamba wakati watu wengine wanapigania katiba kwa ajili ya uhai wa taifa, wao wanaona ni muda wao kuendesha hila ili jambo hilo likwame. Wakati watu wanaona katiba ya sasa ime-outlive its usefulness wao wanaona kila jambo la mabadiliko ni tatizo kwao. Watu wa ajabu kabisa.

Pamoja na hila zote za kwenye mabaraza ya katiba mpaka bungeni, bado kukaa tu kama watu wazima wakajadili rasimu ili basi walau washinde kwa hoja, hilo nalo gumu. Na baada ya kuzidiwa hoja wakaona matusi, vijembe na kudhalilishana ndiyo ustaarabu. Kama haitoshi UKAWA wamekuwa waungwana tena. Kuliko kuendelea na mijadala ya matusi badala ya kujadili rasimu wao wameona watoke, wakawaelimishe wananchi kuhusu madhara ya mchezo wa CCM. Ajabu CCM nao kuendelea na kujadili rasimu hata wakiwa peke yao bado imewashinda. Wamekaa wanajadili UKAWA wiki nzima na nusu. Kama walitoka makwao kuja bungeni kujadili UKAWA!

Kwamba ndani ya wiki na nusu katika chama kizima, wakiongozwa na waziri Mkuu, amekosekana hata mtu mmoja mwenye busara wa kuwaambia wenzake tujadili rasimu siyo watu binafsi! Halafu tukisema CCM ni hopeless mnasema tunakashifu chama. Sasa hawa ni watu wa aina gani? Na mnataka nikubali kuwa kwa hali hii tuna viongozi wa kutuongoza? Viongozi wa aina hii wanatupeleka wapi? Mimi siyo muumini mzuri wa bahati, lakini ni wazi kuwa hata hapa tulipo tupo kwa bahati tu. Siyo kwa sababu tuna viongozi. Siyo kwa uongozi huu ambapo Rais ndiyo kiongozi wa vitisho, kejeli na vijembe, tena mpaka kwa watu aliowateua mwenyewe!

Narudia, sijawahi kuona chama cha kipuuzi kama CCM! Sitegemei kuona kingine kama hicho mpaka nakufa!
 
Katika maisha yangu, sijawahi kuona chama cha kipuuzi kama CCM! Sidhani kama nitaona kama hicho mpaka kufa kwangu. Kwamba wakati watu wengine wanapigania katiba kwa ajili ya uhai wa taifa, wao wanaona ni muda wao kuendesha hila ili jambo hilo likwame. Wakati watu wanaona katiba ya sasa ime-outlive its usefulness wao wanaona kila jambo la mabadiliko ni tatizo kwao. Watu wa ajabu kabisa.

Pamoja na hila zote za kwenye mabaraza ya katiba mpaka bungeni, bado kukaa tu kama watu wazima wakajadili rasimu ili basi walau washinde kwa hoja, hilo nalo gumu. Na baada ya kuzidiwa hoja wakaona matusi, vijembe na kudhalilishana ndiyo ustaarabu. Kama haitoshi UKAWA wamekuwa waungwana tena. Kuliko kuendelea na mijadala ya matusi badala ya kujadili rasimu wao wameona watoke, wakawaelimishe wananchi kuhusu madhara ya mchezo wa CCM. Ajabu CCM nao kuendelea na kujadili rasimu hata wakiwa peke yao bado imewashinda. Wamekaa wanajadili UKAWA wiki nzima na nusu. Kama walitoka makwao kuja bungeni kujadili UKAWA!

Kwamba ndani ya wiki na nusu katika chama kizima, wakiongozwa na waziri Mkuu, amekosekana hata mtu mmoja mwenye busara wa kuwaambia wenzake tujadili rasimu siyo watu binafsi! Halafu tukisema CCM ni hopeless mnasema tunakashifu chama. Sasa hawa ni watu wa aina gani? Na mnataka nikubali kuwa kwa hali hii tuna viongozi wa kutuongoza? Viongozi wa aina hii wanatupeleka wapi? Mimi siyo muumini mzuri wa bahati, lakini ni wazi kuwa hata hapa tulipo tupo kwa bahati tu. Siyo kwa sababu tuna viongozi. Siyo kwa uongozi huu ambapo Rais ndiyo kiongozi wa vitisho, kejeli na vijembe, tena mpaka kwa watu aliowateua mwenyewe!

Narudia, sijawahi kuona chama cha kipuuzi kama CCM! Sitegemei kuona kingine kama hicho mpaka nakufa!
Bravo broda!Sijawahi kuona chama cha kipuuzi kama CCM!Sitegemei kuona kingine kama hicho mpaka nakufa!
 
Bravo broda!Sijawahi kuona chama cha kipuuzi kama CCM!Sitegemei kuona kingine kama hicho mpaka nakufa!

Na hakitatokea kimgine cha kipuuzi kitakachotokea zama hizi kama hichi si Tanzania tu hata jamhuri ya Africa ya kati ambako kuna vita na vurugu
 
Back
Top Bottom