Acha Uvivu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 525
- 131
Jamani mimi nimekuwa nikifikiria kwa muda mrefu juu ya hizi imani zetu na waanzilishi wake. Kwa Uislam naamini Muhamad hakuanzisha haya madhehebu ya Suni, Shia, Kurdi n.k ambayo yapo katika uislam lakini yana misimamo tofauti hata kuweza kuuana km Iraq kaskazini. Vivo hivyo katika ukiristo kuna madhehebu ambayo hayaishi kupondana, mara eti wale kanisa la Shetani. Au Wakatoliki sio dini ya kweli ila Usabato. Tena eti kuwa Mpetekoste ndio sasa. Lakini yesu alileta Ukristo na hakuleta haya madhehebu na wala hakusema kupitia dhehebu fulani mtu ataenda peponi. Pia katika uislamu nadhani ni hivyo hivyo na hatuambiwi wateule wataishi katika makundi huko peponi. Sasa huu ni mtego ambao watu wenye akili za umimi na uroho ndio hutugawa kwa misingi ambayo ni kinyume cha misingi ya hizi imani mbili. Wana JF mnajiita Great Thinkers lakini bado mtu km Malari Sugu na wanaojibu hoja zake udini mnaingia kwenye mtego. Kwa kutambua hii siri mimi nitajitahidi tu kuwa msafi na sio nishabikie dini halafu mtenda dhambi. Hivyo natangaza nia ya kuoa muislam hadi nipate andiko takatifu litakalosema peponi tutaishi km Waislam (shia, suni kivyao) au Wakristo (wasabato, waluteri) kivyao. Siwezi kuukubali upuuzi mimi. Mwenye hoja ya msingi aseme na aeleze haya madhebu katika kila dini yana asili gani.