Namzimikia sana Faizafoxy!

fuatilia mistakes za matamshi katika kiswahili cha huyo mama mrekebishaji wa wenzie
 
Ushungi unahusiana nini na kuongea?

Nioneshe nilichokukwaza hata unishambulie bila mpango. Unanshangaza! wengi wenu huwa hampendi ukweli na mfumo dume unawafanya muone kuwa wanawake ni watu wa kukaa kimya na hawajui kitu, hiyo inatokana na malezi uliyolelewa nayo.

Wanawake wa Kiislaam tuna rights zetu kwa zaidi ya miaka 1400 leo. Usione ushungi kuwa ni kitu cha ajabu hata ma nun wanauvaa huo, kwanini?
Kwa lugha za vijana wa sasa USHUNGI ni behind ya mwanamke. napita na zangu
 
Kigarama, una hamu na Mandi?
Sisi watu wazima mambo yetu tunayamaliza kimya kimya. Ushawahi kuusikia wimbo wa "kijana acha kupiga mayowe" unajua nani alikuwa anaimbwa? Muulize Faiza ndiye anayajua mambo ya Kilwa jazz na Jamhuri Jazz!
 
Mzimikie FF ipo siku atakufikiria japo kazi ya kusafisha mabanda ya Nguruwe nyumbani kwake...
 
Mimi naweza kuwa Kilaza lakini FF unamuonea. Level yake ni juu sana kuliko wengi wetu hata kama sikubaliani naye kwenye mambo mengi!!

Ntakubaliana na wewe kama utasema ni standard gani unazitumia kusema mtu fulani yuko juu. Kule kwetu kuna waendesha baiskeli wengi sana,kwahiyo ukionekana na pikipiki unaheshimika kama uko juu. Ila kwa jiji lenu la Darn hali ikoje?
 
anawafanyaga = anawafanya

neno sahihi ni huwafanya na si anawafanya!!!!anawafanya ni hali ya sasa wakati huwafanya ni hali endelevu!NITONYE ametumia anawafanyaga kumaanisha hali endelevu!!!kwahiyo neno sahihi ni huwafanya
 
Back
Top Bottom