Maseto
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 944
- 545
Pamoja na kumuunga mkono JK kwa maoni yake aliyotoa jana kuwa muungano ubaki,pia nawaunga mkono CHADEMA kwa suala la kugawanya Tz kimajimbo.napendekeza kuwa kuwe na serikali moja yenye majimbo kadhaa, Zanzibar ipewe upendeleo wa kuwa jimbo kamili,ingawa majimbo mengine yanaweza kutokana na muungano wa mikoa kadhaa kwa upande wa bara.JK alichofanya jana ni kuanza kutoa maoni yake kama mwananchi,siyo kukataza kujadili muungano.natumaini jaji Warioba alirekodi kwa maoni ya JK yalitolewa baada ya Tume kuapishwa.