Namuheshimu mama yangu lakini simpendi

wakuu nina tatizo nimekaa nalo muda mrefu sana moyoni mwangu'
tumezaliwa wanne kwenye familia yetu' sisi ni wachaga na tumekulia na kulelewa na kusoma uchagani'
lakini kwa kadri tulivyokuwa tunaendelea na maisha niligundua mama yangu mzazi anamthamini mtoto mwenye mali peke yake'
baada ya kugundua hilo niliamua kunyamaza kimya japo nilikuwa na uchungu moyoni'
lakini hicho kitendo kilijidhiirisha hata kwa watu wanaotufahamu kijijini kwetu na ilileta matatizo makubwa'
kwa kweli kutoka moyoni mwangu nimejikuta simpendi kabisa mama yangu lakini bado namweshimu kama mzazi wangu'
nikienda nyumbani mara moja kwa mwaka sijisikii kabisa hata kukaa naye hata kwa dakika 10 inakuwa ngumu sana,
niliumia sana kwa kuwa mimi ndiye maskini kabisa na ndiye ambaye sipewi heshima kabisa
naombeni kujua kama kuna mtu mwenye matatizo kama haya na naombeni kujua kama kunaweza kutokea matatizo yoyote katika maisha yangu kwa hilo

nawakilisha.

episodes pole sana kwa kweli ni maisha magumu haya ila mshukuru MUNGU kwa yote. ... chukulia ni kitu cha kawaida .(Si nasikia wachaga wanahusudu sana wenye pesa hadi wanawaamkia..shikamoo mwanangu!!- kama ni kweli ). Hii post yako imenigusa sana but amini unapoweka 'grudges' juu ya mama yako Moyoni mwako ndivyo unavyozizuia baraka za Mwenyezi Mungu katika maisha yako. Tumeambiwa tuwaheshimu wazazi wetu ili siku zetu zipate kuwa nyingi humu duniani lakini pia ziwe za mafanikio. Huwezisema unamheshimu wakati unamchukia!! hebu kaa na utafakari hiyo heshima yako ikoje----- heshima ni zaidi ya shikamoo mama; aksante mama e.t.c. Heshima ni ule m-package mzima wa shukrani, thamani na appreciation- Sasa kama unasema unamheshimu lakini humpendi- kutokumpenda kunawezakukuzuia kumthamini na hata kuappreciate anayokufanyia au malezi alokupa.

Funguka..........kama unaweza jenga ukaribu naye kisha mweleze..Mama najua sina uwezo kiasi cha kukuriddhisha, but mama jinsi unavyotutreat mimi na mdpgp wangu nakwazika..............mweleze unavyojisikia pengine ye anafikiri hujagundua au hujui. Mweleze kuwa unajua, wamama tuna huruma na huumia sana pale tunapowakosea wenetu (hatunaga ile pride ya mimi ni mzazi wako -so sistahili kukuomba msamaha) unawezashangaa akawa karibu nawe zaidi.

Funguka moyo ili upate kuachia baraka za MUNGU zimiminike kwenye maisha yako na kuyafungua madirisha ya baraka na mafanikio nyumbani kwako. Kila la khheri
 
Kuna somo moja alifundisha alifundisha Mwalimu wa neno la Mungu Mwakasege, linalosema LANGO LA MZALIWA WA KWANZA, ungepata kitabu au CD, ungejifunza kitu kikubwa. Hata hivyo kaka huna option, nikunyenyekea tu, kutubu kwa Mungu, nakuomba hicho kiambaza kiondoke kati yako na mama yako.
 
Pole kwa yote yanayokukuta.......
Ila kama ni mkristo naomba zingatia amri ya Mungu isamayo...."waheshimu baba na mama yako siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na bwana MUNGU wako.". Muache akufanyie ubaya usilipize, mpende na msikilize...just do your part.
 
Kuna somo moja alifundisha alifundisha Mwalimu wa neno la Mungu Mwakasege, linalosema LANGO LA MZALIWA WA KWANZA, ungepata kitabu au CD, ungejifunza kitu kikubwa. Hata hivyo kaka huna option, nikunyenyekea tu, kutubu kwa Mungu, nakuomba hicho kiambaza kiondoke kati yako na mama yako.

Kweli kabisa LD..nimekisoma kitabu chake.
 
  • Thanks
Reactions: LD
Mungu hawezi kukunyima vyote, Yeye ni mwaminifu kwao wamchao na hakika siku moja atasikia sala yako atakuinua kwa wakati wake

Jina la Bwana lihimidiwe

Pengine nisingeweza kutoa ushauri mzuri zaidi ya wa Miss Judith!
Labda kwa nyongeza tu ni kuwa MAMA hata waweje, hata wawe na tabia gani, bado watabaki kuwa ni mama zetu, tuwapende na tuwaheshimu.
Kupenda kwake kwa wanawe walio na uwezo kusikufanye wewe usimpende yeye kwani "Ukweli ni kuwa na wewe anakupenda". Kama angelikuwa hakupendi, sidhani kama angejisumbua kubeba ujauzito wako na kukulea hadi umefika ulipo.

Kitu kinachokusumbua ni kukosa kwako mali, kwa maneno mengine, chuki zako kwa mama yako zimeanzia kwa kaka zako walio na uwezo, na kuanzia hapo kila analofanya mama au ndugu zako unahisi ni manyanyaso kwako. Sio hivyo. Ikiwa wamepata kwa juhudi zao, nawe fanya juhudi kutafuta chako. Ikiwa Mungu amewapa na wewe kukunyima, uelewe kuwa Mungu humpa na kumnyima amtakaye, hugawa kwa mujibu wa kiasi na stahili zetu. Kama ushauri, "Usitumai cha ndugu".

Nisingependa kutumia maneno "wivu na choyo" lakini kumbuka kuwa vitu hivi ni kama kensa katika nafsi zetu. Nina wasiwasi kuwa hata hii hali ulinayo inaweza kutokana na wivu na choyo chako. Natamani niwe nimekosea kufikiri hivi na ninakuomba samahani ikiwa nmekosea. Kumbuka tu kuwa "Anayejitahidi hufanikiwa". Nawe Jitahidi!

Kama neno la mwisho nikitilia mkazo yale ya mwanzo, MPENDE NA MHESHIMU MAMA YAKO. Hili si ombi, ni amri toka kwa Mungu kwani ni wajibu wako.
Kila la Heri Mkuu!
 
wakuu nina tatizo nimekaa nalo muda mrefu sana moyoni mwangu'<br />
tumezaliwa wanne kwenye familia yetu'<br />
sisi ni wachaga na tumekulia na kulelewa na kusoma uchagani'<br />
lakini kwa kadri tulivyokuwa tunaendelea na maisha niligundua mama yangu mzazi anamthamini mtoto mwenye mali peke yake'<br />
baada ya kugundua hilo niliamua kunyamaza kimya japo nilikuwa na uchungu moyoni'<br />
lakini hicho kitendo kilijidhiirisha hata kwa watu wanaotufahamu kijijini kwetu na ilileta matatizo makubwa'<br />
kwa kweli kutoka moyoni mwangu nimejikuta simpendi kabisa mama yangu lakini bado namweshimu kama mzazi wangu'<br />
nikienda nyumbani mara moja kwa mwaka sijisikii kabisa hata kukaa naye hata kwa dakika 10 inakuwa ngumu sana,<br />
niliumia sana kwa kuwa mimi ndiye maskini kabisa na ndiye ambaye sipewi heshima kabisa<br />
naombeni kujua kama kuna mtu mwenye matatizo kama haya na naombeni kujua kama kunaweza kutokea matatizo yoyote katika maisha yangu kwa hilo<br />
<br />
nawakilisha.
<br />
<br />
Nahisi huu ndo ukweli, wachaga walio wengi huwa hawana mapenzi ya utu, bali wana mapenzi ya pesa. Pole sana.
 
hiyo tabia ya mama yako imekuwa kawaida tu siku hizi kwa wazazi wengi. nakushauri msamehe huyo mama kwani naye ni binadamu kama wengine. endelea kumheshimu hivyohivyo na ikibidi uongeze heshima lakini pia uwe na bidii kutafuta kujitegemea kwanza na kisha kama ni mapenzi ya Mungu uwe na mali ya ziada na hata uwezo wa kuwasaidia wengine akiwemo mama yako huyo. &lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
kumbuka kuwa kama hujajitegemea, hilo ndo kikwazo cha kwanza cha wewe kuheshimiwa na watu. jitahidi ujitegemee kwanza. kama tayari unajitegemea, ni vyema lakini usiwe unaomba kusaidiwa na ndugu zako au kupeleka mashitaka nyumbani kwenu kuwa ndugu zako hawakusaidii. jitahidi kupigana peke yako na ikiwezekana shirikiana kwa karibu na marafiki wema ili kuangalia namna ya kunyanyuka kimaisha kwani siku utakaponyanyuka, utaheshimiwa na wote.&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
mwisho usipuuze haja ya kujiendeleza kwa kutafuta elimu kubwa zaidi. wengi walishindwa kupata maisha mazuri kwa kuyatafuta mitaani, wakayapata kirahisi kupitia darasani. kuna mtu namfahamu ana zaidi ya miaka kumi (10) hajafika kwao kwa sababu kama hizi zako, heri wewe unakwenda kila mwaka! ila yeye alijikita katika elimu na hata sasa yuko nje akipasua kitabu na hiyo imemletea tena heshima katika familia kwani kila mtu anakubali kuwa his future is brighter!&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Mungu hawezi kukunyima vyote, Yeye ni mwaminifu kwao wamchao na hakika siku moja atasikia sala yako atakuinua kwa wakati wake&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Jina la Bwana lihimidiwe
&lt;br /&gt;<br />
<br />
<br />


UMEJAA HEKIMA NA UZOEFU WA MAISHA MISS JUDITH,ANA HERI YEYE ALALAYE AU ATAKAYELALA KWENYE KIFUA CHAKO!!<br />
Such a Wonderful Woman!!
 
Mkuu hilo ni kwa watu wengi sana na hii ni kwa sababu wazazi wanathamin pesa kuliko ki2 kingine ....La muhimu msamehe bure coz hajui alitendalo
 
Pole sana Episodes kwa kufikiria hivyo..Labda kweli na kwa asilimia kubwa labda si kweli.<br />
<br />
Michango mizuri imetolewa hapo juu na utakuwa umemsoma &quot;Boss, na pia wengine. Kwanza kabla hujamuhukumu mama yako tafakari vigezo unavyochukua kumuhukumu mama yako. Kuna uwezekano wewe ndiye tatizo au jamii inakufanya uamini mama yako ni tatizo.<br />
<br />
Asilimia 98% bila kujali kabila, utaifa, rangi, au unatoka machame upendo wa mama ni wa pekee. Kumbuka moyo wa mama unauwezo wa kutoa machozi ndani kwa ndani kwa miaka mingi..Asilimia kubwa ya kina mama wanashindwa kuwahukumu hata wale watoto wao waliowasaliti..wanawakubatia.lakini mioyo yao inaendelea kulia kwa kushindwa kuwapa furaha. Asilimia kubwa ya kina wanishia kubeba machungu ya maisha ya watoto wao..&quot;mtoto hakuwi kwa mama&quot; kina mama wanajiona wao ndio tatizo kwa jinsi watoto wao wanavyoteseka. <br />
<br />
Kuna nafasi kubwa kubwa mama yako anasikitika sana na maisha yako kiasi cha kutoweza kukwambia. Kuna uwezekano mkubwa mama yako hapati usingizi kwa ajili yako akiona wadogo zao wana maisha mazuri..Je wewe unawezaje kujua hili? Kwa kumwangalia jinsi anavyotabasamu wakija wadogo zako? <br />
<br />
Kabla hujakata tamaa na kumuhukumu mama yako..<b>Jaribu kujirudi..Mpende mama yako hata kama unajihisi yeye akupendi..ukiweza kujishusha kwa hilo utaweza kusikia kilio cha moyoni cha mama yako na siyo kile kinachotoka mdomoni kwake. </b>
<br />
<br />



Hakika hizi ni Hekima za Suleiman,Episode,sikikia sauti hii ya Mtu aliye nyikani,ukasawazishe hicho kilima kati yako na Mama yako!!
Be Strong,Inawezekana kabisa akawa na yeye anaugua Moyoni mwake Juu yako,go speak to her!! Inawezekana Mazingira aliyokulia hayakumfunda kusema hisia zake!!
Mara chache sana akina Mama kuwa vichaa,tatizo huwa ni sisi akina Baba!!
 
Na isimlaumu sana mama yako.....<br />
Huwezi jua maisha yame mfunza kitu gani...<br />
Inawezekana life haikuwa kind kwake.....<br />
Life was so cruel......so na yeye anatoa kile ambacho life imempa....<br />
Hakuheshimika labda na society kwa umasikini...<br />
So na yeye kwa kuuchukia umasikini,anawachukia mpaka watoto masikini..
<br />





Sawasawa Kaka,na kwa kawaida mtu hawezi kutoa kitu ambacho hana,atatoa alichonacho tu!! Kama amekulia katika familia ambayo thamani ya mtu hupimwa kwa Fedha ni dhahari na yeye atatoa hichohicho kwa Watoto wake!!!
 
watanzania ni watu wenye upendo sana
nashukuru wote mnaochangia hili,na kila wakati ninapata kitu kipya kutoka hapa
nilimtembelea rafiki yangu mmoja na kuona jinsi mama yao anavyoongea nao vizuri japo wao sio matajiri nikatamani ningekuwa ni mimi
ndugu zangu elimu niliyo nayo inanisaidia sana kwenye kazi zangu lakini mimi ni mtu mwenye maisha ya kawaida kabisa na sina mpango wowote wa kutafuta utajiri ili mzazi wangu aniheshimu
mimi namwamini mungu mkuu na ninaamini ninaishi na kumtegemea yeye
huyu mungu akipenda kunipa mali atanipa na hakuna wa kupinga
kila nikisoma comment zenu ninalia machozi
nimeamua kuchukua likizo labda kwenye mwezi wa kumi na nitakwenda kukaa na mama yangu nione kama naweza hili
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
watanzania ni watu wenye upendo sana
nashukuru wote mnaochangia hili,na kila wakati ninapata kitu kipya kutoka hapa
nilimtembelea rafiki yangu mmoja na kuona jinsi mama yao anavyoongea nao vizuri japo wao sio matajiri nikatamani ningekuwa ni mimi
ndugu zangu elimu niliyo nayo inanisaidia sana kwenye kazi zangu lakini mimi ni mtu mwenye maisha ya kawaida kabisa na sina mpango wowote wa kutafuta utajiri ili mzazi wangu aniheshimu
mimi namwamini mungu mkuu na ninaamini ninaishi na kumtegemea yeye
huyu mungu akipenda kunipa mali atanipa na hakuna wa kupinga
kila nikisoma comment zenu ninalia machozi
nimeamua kuchukua likizo labda kwenye mwezi wa kumi na nitakwenda kukaa na mama yangu nione kama naweza hili

Episode, Pole sana ndugu yangu.

Kuna msemo mapenzi ya pesa si mapenzi, ila mapenzi ya roho ni ya maisha.
Ninalokushauri, mweke mama yako kwenye maombi. Mkumbuke kwenye dua zako.
Mama yako anakupenda, ila labda hajaweza kukupa mapenzi vile weye unavyoyatafsiri.
Kumbuka, miezi tisa tumboni, ukazaliwa akakulea tangu ukiwa huna uwezo wa kujifanyia lolote mpaka
pale ulipokuwa na mamuzi yako.

Hakuna kama mama, iwe tulizaliwa mmoja au zaidi ya mmoja.
Endelea kumuombea kila lililo na heri mama yako.
Upendo unazaa upendo, na utu ni bora kuliko mali.
Hakuna haja ya kushindania Upendo wa mama.
Nyote mnapendwa, kila mtu kwa nafasi yake.

Ni yangu hayo machache, kila la heri.
 
Mzazi ni mzazi tu naye shida zake ndo zilimfanya ajisahau aegemee upande mmoja, mpe heshima yake kwani maisha ya duniani ni mafupi, ogopa adhabu utakayoikuta kutokanana kuvunja amri ya MUNGU ya kutokuwaheshimu wazazi.
 
mpendwa nimekutafutia huu wimbo ukusaidie kutafakati ukuu wa Mungu maishani mwako. i hope utaupenda:

JF Senior Expert Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png


icon1.png
Re: kumbukumbu ya siku CHOZI LA DAMU lilipochuruzika
jamani, machozi yananibubujika kwa fadhili hizo kuu za Mungu wetu. hakika jina la Bwana ni la kusifiwa sana.napenda niwashirikishe wimbo wa NITAMHIMIDI BWANA ulioimbwa na kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama. wimbo huu umetokana na Zaburi ya 34.

ni wimbo mzuri sana wa sifa na kwa habari ya mtu huyu, sikiliza kwa akini ubeti wake wa pili, hakika utabubujikwa na machozi jinsi Bwana anavyotenda ajabu na ishara nyingi, lol, asante sana Akili Kichwani kwa kumtukuza Mungu kupitia ushuhuda wa rafiki yako. ubarikiwe sana

wimbo: NITAMHIMIDI BWANA
kwaya: Uinjilisti Kijitonyama
Albam: sina hakika

1.
Nitamhimidi Bwana kila wakati, mimi ii,
sifa zake zi kinywani mwangu daima X 2

Katika Bwana nafsi yangu itajisifu,
wanyenyekevu wasikie wakafurahi,
mwimbieni Bwana ninyi pamoja nami,
na tuliadhiishe jina lake pamoja X 2

Kiitikio
Nalimtafuta Bwana akanijibu, milele
Akaniponya na hofu, Milele X2
Onjeni muone,
onjeni, ooh omjeni
onjeni muone, Bwana Yu mwema X2

2.
Nitamhimidi Bwana kila wakati,
sifa zake zi kinywani mwangu daima X 2

Masikini alimuita, Bwana akajibu,
Akamuokoa kwenye tabu, akawa huru,
malaika wa Bwana aja fanya kituo,
Kumzunguka kumuokoa,
Mtu wa Mungu X2

Nalimtafuta Bwana, milele &#8230;&#8230;&#8230;&#8230;&#8230;

Glory to God

wimbo wenyewe unapatikana hapa:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...-ya-siku-chozi-la-damu-lilipochuruzika-2.html

ni vizuri ukisoma na ushuhuda wa yule kaka ili uone Mungu anavyotupenda.

ubarikiwe sana mpendwa

Glory to God!
 
mkuu mimi ni mwanaume na ni wa kwanza kuzaliwa,wadogo zangu wana uwezo lakini mimi sina uwezo sana ila mungu amenisaidia kuridhika na hali niliyo nayo

Hutakiwi kuridhika ili uendelee, u have to fight ili ufike pale panapostahili. pole sanan haya ndo maisha ya mwisho wa dunia, vituko kila kukicha. Mungu ni mwema atakuinua ukikazana.
 
Wapo wamama wa hivyo, i hate them kwa tabia kama hiyo, wote ni watoto wake, kama hawana uwezo yeye kama mama anatakiwa kuwaombea ili wafanikiwe na kuwahimiza watoto wake wenye uwezo wamsaidie mwanzao ambaye uwezo wake ni mdogo! Ila msamehe kwani ibilisi anaweza kumtumia mtu yeyote ili kukufarakanisha na ndugu na hatimaye ukose amani maishani mwako
 
Hebu kajifunze upya tafsiri na maana ya usemi huu.............what goes around comes around!
 
mkuu nafikiri mimi ni mtu mwenye moyo laini sana
mtu akishaniudhi inakuwa tabu sana kusahau,lakini nafikiri uwezo nilio nao ni mungu peke yake anaweza kuniongezea
namtegemea muumba wangu najua siku moja nitakuwa na mali kama wanavyotaka lakini kamwe sitaweza kulazimisha hilo

Haya mambo yapo sana tuu mkuu na sidhani suluhisho kwako ni kumchukia mama yako kw aaliyokutendea na anayokutendea. Nafikiri suluhisho kwako ingekuwa kumuonyesha mama kuwa wewe ni mpambanaji na unapambana na bado hutaki hali uliyo nayo iendelee hata kwa watoto wako. Nafikiri Mama akishaona hayo atafurahi sana maana nafikiri kama wachangiaji wengine walivyosema inawezekana mama alinyanyaswa sana na jamii kutokana na umaskini wake so hataki mtoto wake awe maskini au anyanyasike kama yeye. Kaa na mama wala usiwe na ile hali ya kinyongo na mwambie wazi malengo yako na mategemeo yako na tekeleza hayo malengo yako kwa kiwango na kiasi then muonyeshe mama na mama akiona hayo atajua kuwa unafight kutoka katika hali uliyo nayo. Usiridhike wala usimwonyeshe mama kuwa umeridhika na hali uliyo nayo maana wewe ni mwanaume onyesha mapambano na onyesha kuwa wewe ni mtoto wa kwanza kwa kuontgoza mapambano ya kuistawisha familia yako.
 
Na mimi nakubaliana na maneno ya wahenga kuwa hilo kabila wengi wana roho za kipalestina. I wish angekuziba pua zako kwa manyonyo yake wakati uko kachanga ndo ingekuwa suluhu ya upuuzi wako.
 
Back
Top Bottom