SnowBall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2011
- 3,054
- 2,840
WanaMMU heshima mbele.
Ni siku kadhaa hivi nilitupia uzi wenye kwenda kwa jina 'Namuanzaje mamamkwe'?. Kwa kweli naomba nishukuru kwa Mawaidha, Ushauri, Maonyo pamoja na Michango yote kiujumla. Baada ya kutafakari kwa kina niliamua kufuata ushauri wa kupiga simu ili niongee na mamamkwe kuhusu issue iliyokuwa inanitatiza. (Kwa wale ambao watakuwa hawafahamu nini kinaendelea wanaweza kujikumbusha HAPA ). Kilichonileta tena ni kuleta 'feedback' kulingana na mlivyonishauri. Kiukweli niliamua kuwasilaina na mamamkwe na mazungumzo yetu yalikuwa kama ifuatavyo:
Snowball: Hallow mama shikamoo!
Mamamkwe: Marhaba mwanangu..za siku..za huko?
Snowball: Nzuri tu mama..halaf pole na matatizo ya kazini kwenu mama..
Mamamkwe: (kama akastuka)..Ahsante mwanangu..si unajua tena mambo ya kazini..
Snowball: Sasa mama nilikuwa naomba majina yako kamili ili nikutumie japo kiasi kweye western union(nikafix ili kuona ukweli).
Mamamkwe: hapana baba..yale mbona yaliisha..hayakuwa makubwa..isitoshe kama ningehitaji pesa mbona ningekuambia mwanangu..yameisha baba!!
Snowball: (Nikashtuka)..Kweli mama??
Mamamkwe: Kweli mwanangu
(Nikajibaraguza na mengineyo kisha nikakata simu).
Kwa kuhofia labda mama kajivunga ili kuua soo..nikatulia kidogo ili kuona kama watawasiliana na binti yake na kwa vyovyote nikajua atanipigia. Hamadi baada ya kama lisaa hivi mchumbaangu akanipigia na kikubwa akaniambia mama alimuambia kuwa nimempigia simu na yeye mchumbaangu akaniuliza kama nilimulizia kuhusu pesa (inaonekana mamamkwe hakumgusia hii kitu) na mimi nikamdanganya kuwa sijamgusia chochote zaidi ya kumsalimia. Eti mchumbaangu akanipongeza kwa kutomuuliza mamamkwe habari za pesa zaidi akinisihi kuwa tumuache tu mama atazirejesha!!!Sikusema chochote zaidi tukaagana na nikakata simu.
Jamani huyu ndiye mchumbaangu ambaye Mungu kama atapenda baadaye mwaka huu eti tutafunga ndoa!!!..Kwa kweli tangu hapo nimeanza kuwaza vitu vingine tofauti!!!..Na pia nimeamini 'pesa mwanaharamu'.
Ahsanteni kwa waliochangia ule uzi....kwa kweli i am fed up!!..Ni laki tano tu but it has given me a lesson!!!!
Ni siku kadhaa hivi nilitupia uzi wenye kwenda kwa jina 'Namuanzaje mamamkwe'?. Kwa kweli naomba nishukuru kwa Mawaidha, Ushauri, Maonyo pamoja na Michango yote kiujumla. Baada ya kutafakari kwa kina niliamua kufuata ushauri wa kupiga simu ili niongee na mamamkwe kuhusu issue iliyokuwa inanitatiza. (Kwa wale ambao watakuwa hawafahamu nini kinaendelea wanaweza kujikumbusha HAPA ). Kilichonileta tena ni kuleta 'feedback' kulingana na mlivyonishauri. Kiukweli niliamua kuwasilaina na mamamkwe na mazungumzo yetu yalikuwa kama ifuatavyo:
Snowball: Hallow mama shikamoo!
Mamamkwe: Marhaba mwanangu..za siku..za huko?
Snowball: Nzuri tu mama..halaf pole na matatizo ya kazini kwenu mama..
Mamamkwe: (kama akastuka)..Ahsante mwanangu..si unajua tena mambo ya kazini..
Snowball: Sasa mama nilikuwa naomba majina yako kamili ili nikutumie japo kiasi kweye western union(nikafix ili kuona ukweli).
Mamamkwe: hapana baba..yale mbona yaliisha..hayakuwa makubwa..isitoshe kama ningehitaji pesa mbona ningekuambia mwanangu..yameisha baba!!
Snowball: (Nikashtuka)..Kweli mama??
Mamamkwe: Kweli mwanangu
(Nikajibaraguza na mengineyo kisha nikakata simu).
Kwa kuhofia labda mama kajivunga ili kuua soo..nikatulia kidogo ili kuona kama watawasiliana na binti yake na kwa vyovyote nikajua atanipigia. Hamadi baada ya kama lisaa hivi mchumbaangu akanipigia na kikubwa akaniambia mama alimuambia kuwa nimempigia simu na yeye mchumbaangu akaniuliza kama nilimulizia kuhusu pesa (inaonekana mamamkwe hakumgusia hii kitu) na mimi nikamdanganya kuwa sijamgusia chochote zaidi ya kumsalimia. Eti mchumbaangu akanipongeza kwa kutomuuliza mamamkwe habari za pesa zaidi akinisihi kuwa tumuache tu mama atazirejesha!!!Sikusema chochote zaidi tukaagana na nikakata simu.
Jamani huyu ndiye mchumbaangu ambaye Mungu kama atapenda baadaye mwaka huu eti tutafunga ndoa!!!..Kwa kweli tangu hapo nimeanza kuwaza vitu vingine tofauti!!!..Na pia nimeamini 'pesa mwanaharamu'.
Ahsanteni kwa waliochangia ule uzi....kwa kweli i am fed up!!..Ni laki tano tu but it has given me a lesson!!!!