Namuanzaje mamamkwe-mrejesho

SnowBall

JF-Expert Member
Sep 13, 2011
3,054
2,840
WanaMMU heshima mbele.

Ni siku kadhaa hivi nilitupia uzi wenye kwenda kwa jina 'Namuanzaje mamamkwe'?. Kwa kweli naomba nishukuru kwa Mawaidha, Ushauri, Maonyo pamoja na Michango yote kiujumla. Baada ya kutafakari kwa kina niliamua kufuata ushauri wa kupiga simu ili niongee na mamamkwe kuhusu issue iliyokuwa inanitatiza. (Kwa wale ambao watakuwa hawafahamu nini kinaendelea wanaweza kujikumbusha HAPA ). Kilichonileta tena ni kuleta 'feedback' kulingana na mlivyonishauri. Kiukweli niliamua kuwasilaina na mamamkwe na mazungumzo yetu yalikuwa kama ifuatavyo:

Snowball: Hallow mama shikamoo!
Mamamkwe: Marhaba mwanangu..za siku..za huko?
Snowball: Nzuri tu mama..halaf pole na matatizo ya kazini kwenu mama..
Mamamkwe: (kama akastuka)..Ahsante mwanangu..si unajua tena mambo ya kazini..
Snowball: Sasa mama nilikuwa naomba majina yako kamili ili nikutumie japo kiasi kweye western union(nikafix ili kuona ukweli).
Mamamkwe: hapana baba..yale mbona yaliisha..hayakuwa makubwa..isitoshe kama ningehitaji pesa mbona ningekuambia mwanangu..yameisha baba!!
Snowball: (Nikashtuka)..Kweli mama??
Mamamkwe: Kweli mwanangu
(Nikajibaraguza na mengineyo kisha nikakata simu).

Kwa kuhofia labda mama kajivunga ili kuua soo..nikatulia kidogo ili kuona kama watawasiliana na binti yake na kwa vyovyote nikajua atanipigia. Hamadi baada ya kama lisaa hivi mchumbaangu akanipigia na kikubwa akaniambia mama alimuambia kuwa nimempigia simu na yeye mchumbaangu akaniuliza kama nilimulizia kuhusu pesa (inaonekana mamamkwe hakumgusia hii kitu) na mimi nikamdanganya kuwa sijamgusia chochote zaidi ya kumsalimia. Eti mchumbaangu akanipongeza kwa kutomuuliza mamamkwe habari za pesa zaidi akinisihi kuwa tumuache tu mama atazirejesha!!!Sikusema chochote zaidi tukaagana na nikakata simu.

Jamani huyu ndiye mchumbaangu ambaye Mungu kama atapenda baadaye mwaka huu eti tutafunga ndoa!!!..Kwa kweli tangu hapo nimeanza kuwaza vitu vingine tofauti!!!..Na pia nimeamini 'pesa mwanaharamu'.
Ahsanteni kwa waliochangia ule uzi....kwa kweli i am fed up!!..Ni laki tano tu but it has given me a lesson!!!!
 
Asante kwa mrejesho mdau....Hapo sasa..!!!kwa kweli i really feel your dilemma..!!TO BE OR NOT TO BE....
 
tatizo unachunguza mno na wewe.busara ni kuongea na huyo ,keo ,tarajiwa taraatibu muelewana akueleze ukweli. huwez pata mwanamke malaika hata siku moja
 
Snowball - achana na hii laki tano kaka. Hata kama utamuuliza tena na akijua dili limebumburuka, anaweza kuja na kamba nyingine. Katika dunia hii ya sayansi na teknolojia bado unamuachia mtu kadi yako ya bank??. Ni hivi...Fanya mpango uchukue kadi yako fasta kaka - bank nyingi sasa hivi wana huduma ya internet banking. Mfungulie account kwenye bank yako na uwe unamtumia pesa online when necessary. Mimi ndo utaratibu wangu huo!

Tena mwambie hizo pesa amuachie mama tu - ukizidi ku-push sana, anaweza kutumia njia ''haramu'' kuitafuta hiyo pesa.
 
tatizo unachunguza mno na wewe.busara ni kuongea na huyo ,keo ,tarajiwa taraatibu muelewana akueleze ukweli. huwez pata mwanamke malaika hata siku moja

Kama ni wa barabarani hapo sawa, ila kama ni yule ambaye aliwekwa maalumu kwa ajili yako, malizia.
The unseen is illustrated by the seen.
 
tatizo unachunguza mno na wewe.busara ni kuongea na huyo ,keo ,tarajiwa taraatibu muelewana akueleze ukweli. huwez pata mwanamke malaika hata siku moja

Dadaangu nilishindwa kuishi na dukuduku moyoni mwangu..at least now i know the type of a person i am intending to live with...
 
Kuna jambo ambalo unatakiwa ufikirie,hizo hela kafanyia nini?Na kwanini hajakuambia?
 
Snowball - achana na hii laki tano kaka. Hata kama utamuuliza tena na akijua dili limebumburuka, anaweza kuja na kamba nyingine. Katika dunia hii ya sayansi na teknolojia bado unamuachia mtu kadi yako ya bank??. Ni hivi...Fanya mpango uchukue kadi yako fasta kaka - bank nyingi sasa hivi wana huduma ya internet banking. Mfungulie account kwenye bank yako na uwe unamtumia pesa online when necessary. Mimi ndo utaratibu wangu huo!

Tena mwambie hizo pesa amuachie mama tu - ukizidi ku-push sana, anaweza kutumia njia ''haramu'' kuitafuta hiyo pesa.

Nadhani ndo kilichobakia bro..
 
ahsante kwa feedback,ila bora umeyajua mapema.fedha,fedheha.inaweza ikambadilisha mtu.ila wadada wa sasa ki ukweli,kumpata mwenye mapenzi hasa bila ya kujali unacho au huna ni wachache sana.ingawa na wadada nao wanasemwa,wanaume wa sasa wanapenda kulishwa.sijui yupi anafaa
 
SnowBall, bila samahani nachelea kukutusi kwa kuwa kanuni za JF haziruhusu.

Hivi, ulipomwachia hawara yako ku operate akaunti yako ya benki ulikuwa unamuonesha kuwa unazo pesa au ni "umwanjo-mwanjo"?

Isiwe huu ni mchakato katika kutaka kuwatapeli wadada wa JF. maana nahisi nyuzi inayofata utasema umeshampiga chini huyo demu wako na upo njiani kurudi na unataka urafiki na demu wa kukuliwaza.
 
SnowBall, bila samahani nachelea kukutusi kwa kuwa kanuni za JF haziruhusu.

Hivi, ulipomwachia hawara yako ku operate akaunti yako ya benki ulikuwa unamuonesha kuwa unazo pesa au ni "umwanjo-mwanjo"?

Isiwe huu ni mchakato katika kutaka kuwatapeli wadada wa JF. maana nahisi nyuzi inayofata utasema umeshampiga chini huyo demu wako na upo njiani kurudi na unataka urafiki na demu wa kukuliwaza.

Mkuu sidhani kama at the first place nilifanya makosa kumuachia acc huyu 'hawara' yangu..ni vigumu sana kueleza humu kila kitu. Itoshe tu kusema 'nimemjua ni mtu wa aina gani'. Na kuileta humu ni kuwasaidia wengine ambao pengine wangeingia kwenye huu mtego nilionasa!. Kuhusu wa dada wa JF nadhani huitaji kuwasemea wewe kama wataona nawatega hope watazungumza wenyewe!..But i made it public, so that we can all learn from this saga!..Otherwise kama nimekukera nipotezee tu mkuu!!!!
 
SnowBall bora ulifuatilia hilo suala (nimeipenda technique uliyoitumia)...Anayesema laki tano ni ndogo suala hapa ni ukweli na uaminifu tena kwenye haya mambo tunayoyaona ni madogo yanaweza kuonyesha mienendo ya watu tuwapendao na kutaka kujenga nao maisha.

Chukua ATM card yako mapema maana hata mama mkweo mhasibu zile laki 5 hakupatiwa!..pesa majaribu!

Now the ball is in your hand!!
 
Last edited by a moderator:
snowball!kuchunguza ni muhimu sana,hiyo laki tano ni kubwa,lkn kubwa zaidi ni kujua uaminifu wa huyo mtarajiwa!!haimaanishi uachane naye ila utajua namna ya kuishi naye kwa tahadhari hususan yanapokuja masuala yanayo husisha mshiko!!chunguza kaka!
 
Dadaangu nilishindwa kuishi na dukuduku moyoni mwangu..at least now i know the type of a person i am intending to live with...

anyway si busara kumuacha ila pia talk to her ili asije akarudia tena kwa upendo sana na siyo ka jazba kama ilivyo desturi ya wababa
 
SnowBall, inabidi ufanye maamuzi yenye busara na ambayo hayatakuja kukuletea tabu huko mbeleni. Huyo mchumba wako, kabla hujamuoa inabidi ujiridhishe na uaminifu wake kwenye mambo yanayohusiana na pesa. Hiyo scenario yako imerise some "red flags" ambazo unawezakuwa hukuwahi kuziona kwenye relatioship yenu.

:coffee:
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom