Nampendekeza Phiri

ELNIN0

JF-Expert Member
Nov 26, 2009
4,161
1,458
Soccer fun's

Tunataka kupata kocha wa timu yetu ya taifa kuchukua nafasi ya Maximo ambaye muda wake unamalizia - sasa basi:--

Ni bora kufanya kazi na mtu unayemjua na unajua uwezo wake na ndiyo maana kila ofisini wakitaka kuajiri mtu huwa kwanza wanafanya internal advert wakikosa mtu mwenye sifa then wanafanya external.

Napendekeza tutumie njia hii kwamba TFF watoe kwanza internally then tukikosa ndiyo waanze kusaka nje ya nchi. Tusipofanya hivi tutakuwa tunawatenga hawa makocha wetu wa ndani na kuwavunja mioyo, na hawatakuwa na ari ya kuweka michango yao kwenye soka endapo hamtawapa nafasi kujaribu kupata nafasi hii ya juu kabisa ya uongozi wa soka wa nchi yetu.

Binafsi naona huyu Mzambia (Patrick Phiri) ambaye yupo nchini na Simba anaweza kushika timu yetu vizuri tu, ni kocha mzuri na CV yake ipo juu. Sasa kwa nini tuhangaike na watu hawa wapo na tunafahamu uwezo wao.

Natoa hoja......
 
shida ya vyama vya soka vya Afrika haviwalipi mishahara vizuri makocha wazawa ama weusi wenzao, tofauti na weupe wanaotoka ulaya ama America. makocha wazawa hawapewi mazingira mazuri ya kazi kama wapewayo wazungu kutoka ulaya. hivyo hata PHIRI akipewa timu hatapewa marupurupu kama ya Maximo, hatapewa mazingira bora ya kazi KAMA ya huyo maximo
 
Binafsi naona huyu Mzambia (Patrick Phiri) ambaye yupo nchini na Simba anaweza kushika timu yetu vizuri tu, ni kocha mzuri na CV yake ipo juu.

CV yake ipo juu kivip kaka.....ameshinda nini katika ngazi ya kimataifa!? - coz that's where we wanna go....

Tumechoka na hizi sera kwamba ukiifunga Yanga, basi wewe upo juu
 
CV yake ipo juu kivip kaka.....ameshinda nini katika ngazi ya kimataifa!? - coz that's where we wanna go....

Tumechoka na hizi sera kwamba ukiifunga Yanga, basi wewe upo juu
PHIRI , amewahi kuingoza Chipolopolo kwenye fainali ya maifa ya Afrika miaka miwili nyuma akiwa na CHIPOLOPOLO, KWANI maximo kabla ya kuja DSM aliwahi kutwaa taji lolote kimataifa ?
 
Phiri yes, lakini hatapewa ushirikiano na Tff, serikali na mashabiki wa yanga!
 
Kwa hali ilivyo sasa anaweza kupewa ushirikiano coz mshahara unalipwa na serikali labda kama serikali ijiondoe coz hapo kwenye mshahara ndio kuna tabu, wadhamini wapo for now wamejitokeza kusupport vya kutosha, so kama ataomba nafasi hiyo na akiwa na vigezo vilivyowekwa na TFF then atapata ajira.Hilo ni kwa wote hata wazawa, kinachotakiwa ni kutimiza vigezo vilivyowekwa na sio kujulikana au umaarufu, inabidi tukumbuke hata mshahara pia ni kigezo kimojawapo coz kuna wanaotaka kulipwa pesa nyingi na kuna wanaotaka kidogo ila kiwango hakilidhishi kupewa timu ya taifa. Kwa maoni yangu mi napendelea kocha atoke nje ili tupate challenge nyingine mpya kama aliyoleta maxi, hawa wazawa waendelee kujenga vijana kitaalamu na sio kimazoea.
 
Mie pia namkubali Phiri. Huyu ni kocha mwenye mafanikio kwa sababu anaweka malengo na anahakikisha yanatekelezeka.
 
Hakuna tafiti zinazoonyesha kwamba Tanzania ina matatizo ya makocha wa football, kocha akiwezeshwa anafanya kazi, tatizo la Tanzania ni investment kwenye timu ya Taifa, kwa jinsi nijuavyo akipewa mswahili tu misaada yote inasitishwa, timu inarudi salvation army!!!
 
napinga straight away phiri kupewa timu ya taifa.

kabla ya yote napenda nikurekebishe ndugu yangu si kweli kazi zote za ofisini zinaanza na internal vacancy advert, kuna kazi zinaitaji mtu wa nje moja kwa moja.

pili, unapotaka kupata mtu wa kuchukua nafasi ya mtu mwingine kigezo kikubwa tutachokiangalia ni uwezo wa anayekuja awe na qualification na uwezo wa iyo kazi zaidi ya yule anayetoka.

phiri hana distignuishable achievement yoyote ktk ukocha wake zaidi ya kuipeleka zambia afcon ambayo kwa zambia si kipya ni kitu they are used to do unlike maximo ametupeleka internal afcon ambayo haikua kawaida yetu then that is achievement.

tanzania tunataka kocha wa kutupeleka afcon na world cup na kocha phiri is unlike to do that, hata iyo simba kwani ni lipi kubwa aliloifanyia hadi awe mtu sahihi kuchukua nafasi ya maximo?

tunataka kocha ambaye ashawai kuipeleka timu afcon, world cup, copa america au euro na ktk klabu level awe amefanikisha timu kubeba africa champions league, ashafundisha bundesliger, uk barlays premier league, serie a, league 1 in france, spain only kama hayupo nje ya hao hafai
 
Phiri mwenyewe nilimuona anahojiwa akasema hayuko tayari kwanza mkataba wake na simba bado kwisha
 
tumsubirni kwanza amalize msimu na simba alafu tutajaribu kumuangalia vizuri na pia sio mbaya ni pendekezo zuri lakini tunahitaji majina mengine zaidi hili yafanyiwe kazi alafu tutachagua aliye bora.tusifanye maamuzi haraka haraka tuchukue mda wetu na process ianze sasa hivi.
 
napinga straight away phiri kupewa timu ya taifa.

kabla ya yote napenda nikurekebishe ndugu yangu si kweli kazi zote za ofisini zinaanza na internal vacancy advert, kuna kazi zinaitaji mtu wa nje moja kwa moja.

pili, unapotaka kupata mtu wa kuchukua nafasi ya mtu mwingine kigezo kikubwa tutachokiangalia ni uwezo wa anayekuja awe na qualification na uwezo wa iyo kazi zaidi ya yule anayetoka.

phiri hana distignuishable achievement yoyote ktk ukocha wake zaidi ya kuipeleka zambia afcon ambayo kwa zambia si kipya ni kitu they are used to do unlike maximo ametupeleka internal afcon ambayo haikua kawaida yetu then that is achievement.

tanzania tunataka kocha wa kutupeleka afcon na world cup na kocha phiri is unlike to do that, hata iyo simba kwani ni lipi kubwa aliloifanyia hadi awe mtu sahihi kuchukua nafasi ya maximo?

tunataka kocha ambaye ashawai kuipeleka timu afcon, world cup, copa america au euro na ktk klabu level awe amefanikisha timu kubeba africa champions league, ashafundisha bundesliger, uk barlays premier league, serie a, league 1 in france, spain only kama hayupo nje ya hao hafai

Huyu ni mmoja wa watu nilosema wanatoka ktk kundi la yanga family wasiomkubali Phiri.
 
Phiri ana mpinzani kama akiomba nafasi hiyo.leo si mshasikia mechi ya kampiga mtu 3-1 mechi 13 bila kupoteza.huyu anafaa.
 
napinga straight away phiri kupewa timu ya taifa.

pili, unapotaka kupata mtu wa kuchukua nafasi ya mtu mwingine kigezo kikubwa tutachokiangalia ni uwezo wa anayekuja awe na qualification na uwezo wa iyo kazi zaidi ya yule anayetoka.

Qualifications za namna gani? vyeti? Track record? Tacit knowledge? Ability to blend in and/or settle?

phiri hana distignuishable achievement yoyote ktk ukocha wake zaidi ya kuipeleka zambia afcon ambayo kwa zambia si kipya ni kitu they are used to do unlike maximo ametupeleka internal afcon ambayo haikua kawaida yetu then that is achievement. tanzania tunataka kocha wa kutupeleka afcon na world cup na kocha phiri is unlike to do that, hata iyo simba kwani ni lipi kubwa aliloifanyia hadi awe mtu sahihi kuchukua nafasi ya maximo?

Mtake radhi huyu bwana wa Zambia. Katika dunia hii nothing should be taken for granted regardless of how good or potentially good a team or an individual is. Mifano hai iko mingi tu, angalia Morocco, Senegal na Afrika Kusini, walikuwepo Angola? Je na kama si kuna wenyeji wa mashindano, Afrika Kusini wangefuzu kucheza fainali hizo?

Hii internal Afcon, tumecheza na nani? Ikiwa kombe la Gosage lenyewe tu latushinda itakuwa huko?


tunataka kocha ambaye ashawai kuipeleka timu afcon, world cup, copa america au euro na ktk klabu level awe amefanikisha timu kubeba africa champions league, ashafundisha bundesliger, uk barlays premier league, serie a, league 1 in france, spain only kama hayupo nje ya hao hafai

Dau la kocha kama huyo mtaliweza? Hao unaowataka wameshazoea madau makubwa, $10,000 inaweza kuwa ni mshahara wa wiki kwao. Halafu pili unajua makocha wengi vijana (i.e under the age of 60) hupendelea kufundisha vilabu na si timu za taifa maana huko ndio kwenye action na masilahi zaidi.

Vile vile pia kuwa na kocha mwenye pedigree kubwa sio kigezo kuwa timu ya taifa itapata mafanikio, wewe angalia akina Carlos Alberto, Paul Le Guen, Roger Lemerre etc.

Binafsi kama mdau wa Msimbazi nisengependa kuona kocha wetu anaenda Stars, mtatuyumbisha tu katika project yetu na pia Watanzania msivyokuwa na dogo mtaanza kuchonga tu from day one.

Matatizo ya timu ya taifa ni ya tactical discipline. Timu haina shape, defence iko all over the place na wachezaji wengine wanashindwa kujipanga.
Tunahitaji kocha kutoka nchi za Ujerumani, Uskochi, Uingereza au Italia. Huko tactical discipline na uwezo wa timu kucheza kimfumo na kuushika mfumo katika mechi nzima uko katika damu.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom