Namna ya kumkamata mwanaume!!

Nimekukubali. Problem yetu ni desperado! Nna dadangu akiambiwa na mkaka ntakutoa jioni, anaulizia pa kupata gauni la harusi!
Kila la kheri mama

aah hiyo kali halafu hapo aliposema mwingine anapigiwa tu simu na wanaume hata wasiojulikana ndo nimekubali
 
I was single once, but now i'm a wife and a mother. Nimekaa nikaona sio vibaya iwapo nta-share tips kadhaa zilizonisaidia kumuweka baba Ashrat sawa na mpaka leo hii sijawahi kuhisi wala kugundua kwamba anatoka nje ya ndoa yetu, japo matatizo ya hapa na pale hayakosekani ila tumedumu na bado tunaendelea na safari.

Unapokutana na mwanaume akakutongoza/mwanamke akakukubalia kuna uwezekano mkubwa kuwa amevutiwa na wewe kweli au kakutamani tu. Kitu ambacho watu hua wanasahau ni kwamba hata mtu aliyekutamani tu unaweza ukampa mwongozo/sababu mpaka mwenyewe akajikuta anakupenda kuliko ambavyo angeweza kutarajia kwamba angewahi kupenda. Ndio maana hata wale waitwao 'bad girls/boys' hua wanajikuta wamenaswa na kunasika at some point.

1. Usiigize.
Maigizo waachie wasanii wetu, kuwa vile ulivyo kweli kimaisha/kitabia (isiwe mbaya)/mazoea n.k

2. Don't move too fast/act desperate.
Usitumie ule muda wa mwanzo kabisa wa mahusiano yenu kutaka kujua "una malengo gani na mie?" "utanioa?" "Kanitambulishe/nataka nikakutambulishe." n.k Mpe nafasi ya kukusoma na kupata kujua wewe ni mtu wa aina gani, je unafanania na mwanamke ambae angependa kuwa nae kwa muda mrefu, possibly hata ndoani? Na wewe nawe tumia muda huo kufanya kitu hicho hicho.

3.Don't be too demanding.
Huyo sio baba yako wala sio mume just yet, hivyo chochote atakachokufanyia kinatokana na yeye kutaka/kupenda kufanya hivyo na sio kwakulazimika. Haki hiyo hauna.

4. Kuwa na shukurani.
Learn to appreciate all that he does for you, that way ataona umuhimu wa hayo anayokufanyia, yawe makubwa au madogo.

5. Be real.
Badala ya kufika kwake na kuanza kushangaa anaishije bila ya mfanyakazi wa ndani huku ukitamba kuwa wewe huwezi, shangaa anawezaje weka nyumba yake katika hali nzuri mwenyewe bila ya msaada. Hii itaonyesha fika wewe utakua mke wa aina gani hapo baadae, kama ni wale wakukaa miguu juu huku wakiagiza hata maji waliyoombwa na mume au la.

6. Learn to cook if you don't know how to.
Waliosema "the way to a man's heart is through his stomach" hawakukosea. Ukiachilia mbali wale watu wachache wanaokula ili kushiba wengi hua wanajali ladha. Hiyo ndio hua inawaongezea hamu ya kula na kuwarudisha nyumbani mapema pia kuwafanya wakumiss pale inaposhindikana kula chakula chako . Kwakumwonyesha mwanaume kwamba hata tumbo lake unaweza kuliridhisha unamwongezea sababu za kukuweka kwenye maisha yake.

7. Mheshimu.
Mpe heshima yake kama mwanaume wako ila usimwogope. Wengine wote usiwape nafasi kumfanya ajisikie kwamba haheshimiki.

8. Kuwa ngao yake.
Inapotokea anakumbwa na matatizo yoyote yale onyesha utayari wa wewe kuwa pamoja naye kwa hali na mali mpaka yatakapoisha. Pia usikose kumjali kumpa moyo pale unapoona inahitajika.

9. Kuwa muwazi.
Kama kuna mambo ambayo unajua moja kwa moja yatakuwa sehemu ya mahusiano yenu (watoto/X mkorofi .nk) mweleze mapema ili aamue kama yuko tayari kudeal nayo au la.

10. Usiwe na chuki.
Kikifika kipindi cha yeye kukutambulisha kwa ndugu na rafiki zake onyesha ushirikiano. Usionyeshe chuki wala kujiona kana kwamba wewe ndio wewe.

11. Give your all.
Kama na nyie mtaamua kuonjeshana tunda kabla (kama ambavyo wengi wanafanya karne hii) basi kuwa mbunifu, mtundu na usiwe mvivu.

12.Pendeza.
Vaa/onekana vizuri unapokuwa nje hata ndani pia. Usisahau kuzingatia/jali hisia zake kuhusu mavazi yako.

13. Onyesha interest kwa yale ayapendayo yeye.
Usiwe mbinafsi kila siku unataka kusikilizwa wewe tu na story/mambo utakayo wewe. Uliza/jua kuhusu yale anayopenda yeye mf. mpira/siasa.

14.Kuwa mtulivu.
Usiwe mtu ambae kila saa simu yako inapigwa pigwa na wanaume wasio ndugu wala marafiki wakaribu na wanaoeleweka. Discpline ni muhimu sana.

15.Usimzonge.
Usiwe mmoja wa wale watu wanaofuatilia wenzi wao masaa yote wanapokuwa hawapo pamoja. Mpe nafasi ya kuwa na marafiki zake bila kuhitaji kuzima simu ama ku-ignore simu/text zako.

16. Mfurahishe/chekeshe.
Joke around sio muda wote yeye ndio awe wakukufurahisha wewe.

17. Jifunze kusamehe.
Mambo madogo madogo yanapoombewa msamaha samehe na uache yapite.

18. Mshirikishe Mungu wako.
Ukishaona kwamba huyo ndie basi mshirikishe yule unayemwamini ili upate mwongozo wa kiroho.

Mama Ashrat.



on point mama ashrat..hasa iyo ya 14,kina nakusalimia,waharibif sana..
 
Kwanza napinga kabisa kama mme wako hajaenda nje ya ndoa, sababu ni hii hapa quote yako nummber 11 ni ushahid tosha kabisa.....Nauliza nini mana ya ndoa? wewe ume sexi kabla ya ndoa mana unasema mnapo amua kufanya sex usiwe mvivu hapo kabla ya ndoa...sa ndoa yako iko wapi wewe mama Ashraf?

Hebu nipe kitabu gani cha dini kiancho ruhusu ufanye sex kabla ya ndoa :A S shade:


Mpe heshima afu hapo hapo unasema usimuogope hapo ni kuelewe vipi?

fazaa

Kuna mengi dini isiyoruhusu ila at some point tunajikuta tunafanya kwasababu tunaona tunatakiwa/hitaji kufanya hivyo. Ndio maana kukawa na kutubu, tunakosa kila siku na tunatubu na kuachana na hayo makosa. Hata wewe inawezekana hukushiriki/bado hujashiriki nje ya ndoa ila haina maana huna makosa mengine, pia usisahau kuwa kwa Mungu hamna mizani.

Tukirudi kwenye kuheshimu na kuogopa.
Kwanza kumuogopa mtu sio kumheshimu. Naweza nikakuogopa wewe kwasababu hii au ile ila nisikuheshimu, hiyo inaiywa nidhamu ya woga maana hutoona kwamba sikuheshimu. Pili, kumwogopa mwanaume/mwanamke wako kutakunyima uhuru/wepesi wa kuwa karibu nae kimawasiliano na hata kihisia kwasababu unamwogopa.Ndio maana wapo watu wapo kwenye ndoa miaka na miaka ila hata siku moja hamna anaeweza mkalisha mwenzie chini akamweleza hisia zake au akamkosoa kiutu uzima. Matokeo yake ndo hao wahusika kwenda kutafuta unafuu sehemu nyingine.
 
Last edited by a moderator:
Sijakataa kama utakuwa katika point zingine sio kwa mke na mme....Tukizungumzia point ya mke kama hamuogopi mme wake, lazima kuna ukosefu tu waheshima hapo....Mana anaweza kwenda popote bila ya kumuaga mme wake, na mengi tu anaweza kufanya sababu hamuogopi mme wake.

Heshima ndio itakayozuia hayo yasitokee.
Ukishamheshimu mtu (heshima ya kweli na sio ya kushinikizwa) utamtii automatically. Kila kitu kitaenda kwa maelewano.

charmingirl, nafurahi kusikia hivyo mwaya.

BAK na UmkhontoweSizwe
Asanteni sana kwa nyongeza zenu, kila mlilosema linaongeza mambo muhimu sana.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
BAK umeongea kitu muhimu sana. Sio ex tu ama watoto, kuna issue ya wanafamilia wakorofi pia. Hii tabia (hasa ya wadada) ya kujifanya unatokea familia takatifu is really disgusting. Hata kama babako mchawi muambie mwenzio, ajue u don't side with mambo yake. Ili hata huko mbele ya safari akikusakama nao umuambie the loss is his asiwacheke ndugu zako manake nao ni sehemu yenu.
Asante rafiki.
...Nimeupenda sana mchango wako na hii hapa ni kweli kabisa, ". Kuwa muwazi.
Kama kuna mambo ambayo unajua moja kwa moja yatakuwa sehemu ya mahusiano yenu (watoto/X mkorofi .nk) mweleze mapema ili aamue kama yuko tayari kudeal nayo au la."

Napenda kuongezea kama atapenda kujua mahusiano yako ya nyuma na kwanini yalivunjika basi kuwa muwazi. Ila siyo maswali ya huyu A alikuwa na size gani mlikuwa mnananihii kwa style zipi. Unapokuwa muwazi na kueleza mambo muhimu ambayo mwenzako angependa kuyafahamu basi fanya hivyo ukaleta za kuleta na kuficha mambo muhimu ambayo mwenzio angependa kuyajua basi itakula kwako. Unapokuwa muwazi inajenga imani kubwa kwa mwenzi na hivyo kuanza kukuamini mapema katika mahusiano yenu.


 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Heshima ndio itakayozuia hayo yasitokee.
Ukishamheshimu mtu (heshima ya kweli na sio ya kushinikizwa) utamtii automatically. Kila kitu kitaenda kwa maelewano.

charmingirl, nafurahi kusikia hivyo mwaya.

BAK na UmkhontoweSizwe
Asanteni sana kwa nyongeza zenu, kila mlilosema linaongeza mambo muhimu sana.


...Nilishawahi kuweka mfano hai hapa wa rafiki yangu mpenzi ambaye baada ya kumpata kimwana na kutoamini bahati yake kwamba kimwana yule alikuwa hana mtu ikabidi amuweke kiti moto kuulizia mahusiano yake ya nyuma na kwanini mahusiano yake ya mwisho yalivunjika. Kimwana akawa muwazi kuelezea kila kitu bila kuficha chochote, na jamaa akafuatilia ili kuhakikisha aliyoambiwa yalikuwa kweli na akathibitisha kwamba ni ukweli mtupu. Binti naye akataka kujua mahusiano ya nyuma ya mwenzie basi njemba haikuwa na hiana ikaelezea kila kitu. Mapenzi yakapamba moto sasa ni mume na mke.


Vaislay
 
Last edited by a moderator:
BAK umeongea kitu muhimu sana. Sio ex tu ama watoto, kuna issue ya wanafamilia wakorofi pia. Hii tabia (hasa ya wadada) ya kujifanya unatokea familia takatifu is really disgusting. Hata kama babako mchawi muambie mwenzio, ajue u don't side with mambo yake. Ili hata huko mbele ya safari akikusakama nao umuambie the loss is his asiwacheke ndugu zako manake nao ni sehemu yenu.
Asante rafiki.

Ahsante sana King'asti kwa mchango wako muhimu.
 
Last edited by a moderator:
Safi sana mama ashrat, tatizo wake wa karne hii wanapenda waonekane wao ndio wao, mume kama pambo tu ndani ya nyumba la kumuwezesha nae aonekane ameolewa. Maadili ya wake kwa waume zao yameporomoka sana

Mke unakuta yeye kazi yake kubwa ni kukuwinda tu aone wapi umeteleza hata kama ni kwa ishu ndogo ndogo ambazo sometimes na yeye anakuwa amechangia. Baada ya hapo ni ugomvi kwa kwenda mbele na kumjibu mume kwa maneno machafu.

Inasikitisha sana.
point,,,,hakika na kweli
 
dah, shule mwanana sana hii... si mbaya siku nyingine ukishuka kwenye jukwaa la kule chini kabisa kutugawia dondoo zinazohusiana na department ile pia...
 
Mke mwema hutoka kwa Bwana; kwa akili zetu si rahisi kumtambua mke mwema

unamtaka mke mwema atokaye kwa mungu,sawa,wewe ni mwema,,,,,,,,,yaan mungu amtoe mtu wake mwema ampe haramia,,,,,,,,jaman,jamii imeharibika na wanawake hao gibiligibili ni zao lake,,,,,zaa kusanya watoto lea somesha,,,kuoa tunaolea mazoea tu,,,ila moto,,tunakufa kwa presha tunawaacha wanadunda,,,wanafurahi hao hasa umeacha vimali,,kaburi lako atajengea hata kwa marumaru na kuwasha mishumaa kumbe ukiwa hai alikuuuumiza,,,,achana nao:yo:
 
Hii sredi imetulia sana kwa wadada, ubarikiwe mama.
Ufafanuzi : Lawyer nikisema sredi imetulia basi ujue ina hazi ya kimataifa
 
...Mie natofautiana nawe katika hili. Kuna Wanawake ambao ndani ya ndoa wanawaogopa waume wao kutokana na vipigo wanavyovipata toka kwa hao waume zao. Mume kama hayuko nyumbani mama aliye nyumbani anakuwa na raha na mara mume akirudi tu basi wasiwasi mtindo mmoja akijua kosa dogo tu basi litaishia kwa yeye kupata kipigo kitakatifu.

Hakuna sababu yoyote ya mke kumuogopa mumewe ila kuna kila sababu ya mke kumuheshimu mumewe na vice versa. Waliomo ndani ya ndoa au hata mahusiano kabla ya ndoa inabidi waheshimiane lakini si kuogopana.
Aisay mimi na wewe tuko tofoutii sana wewe unadhani mke kumuogopa mme ni sababu ya vipigo anavyo pewa.

Mwanaume anaye piga mwanamke naye ni mwanaume...hao sio wanaume, hao ni walevi, vichaa, yani sijui niseme nini...Yani wewe unadhani wanaume wote ni walevi au vichaa au hawajui mwanamke katokea wapi?

Ndo naona mawazo yako na mimi yako tofouti sana, wewe unaona wanao piga wake zao ni wanaume :A S shade:
 
mama asharat ni noumeeer...umegusa 95% ya mambo aliyokua ananifanyia wife wakati tukiwa wachumba,tena umesahau.....hard working pia ni mpango mzima,leo hii ni mme na mke na mtoto mmoja....
 
fazaa

Kuna mengi dini isiyoruhusu ila at some point tunajikuta tunafanya kwasababu tunaona tunatakiwa/hitaji kufanya hivyo. Ndio maana kukawa na kutubu, tunakosa kila siku na tunatubu na kuachana na hayo makosa. Hata wewe inawezekana hukushiriki/bado hujashiriki nje ya ndoa ila haina maana huna makosa mengine, pia usisahau kuwa kwa Mungu hamna mizani.

Tukirudi kwenye kuheshimu na kuogopa.
Kwanza kumuogopa mtu sio kumheshimu. Naweza nikakuogopa wewe kwasababu hii au ile ila nisikuheshimu, hiyo inaiywa nidhamu ya woga maana hutoona kwamba sikuheshimu. Pili, kumwogopa mwanaume/mwanamke wako kutakunyima uhuru/wepesi wa kuwa karibu nae kimawasiliano na hata kihisia kwasababu unamwogopa.Ndio maana wapo watu wapo kwenye ndoa miaka na miaka ila hata siku moja hamna anaeweza mkalisha mwenzie chini akamweleza hisia zake au akamkosoa kiutu uzima. Matokeo yake ndo hao wahusika kwenda kutafuta unafuu sehemu nyingine.
Yeap kuna kutubu mengi tu lakini sio ya kuoa mwanamke umeisha sex naye, afu unaendelea naye eti ni wife wako...wakati kwa mungu wewe kila ukisex na huyo mme wako/mke wako ambaye mliona bada ya sex ni dhambi tu, sababu mungu hatambui ndoa yenu.

Mtu ana tubu harudii makosa yake tena...sa we unategemea kutubu lini? ikiwa mme uliye naye umefanya naye sex kabla ya ndoa...sijui niseme nini hapo...Hivi kuna toba hapo.

Mtu anatubu kama vile ka sex nje ya ndo afu haendelee na makosa tena ukiolewa na mtu ume sex naye ina mana hujatubu bado , sasa wewe sijui niseme nini sijui lini unategemea kutubu afu hapo hapo unashangilia wengine watoe matunda ili waolewe hahaha...kweli kuna vichekesho duniani...najua wengi mtanichukia sababu mmo katika huo mfumo...lakini huo ni ukweli, mtake msitake ndoa zenu hazikubaliwi na mungu :A S shade:
 
Aisay mimi na wewe tuko tofoutii sana wewe unadhani mke kumuogopa mme ni sababu ya vipigo anavyo pewa.

Mwanaume anaye piga mwanamke naye ni mwanaume...hao sio wanaume, hao ni walevi, vichaa, yani sijui niseme nini...Yani wewe unadhani wanaume wote ni walevi au vichaa au hawajui mwanamke katokea wapi?

Ndo naona mawazo yako na mimi yako tofouti sana, wewe unaona wanao piga wake zao ni wanaume :A S shade:

...Niliyoyaandika hapa ni maneno ambayo nimeyasikia kwa akina mama ambao wanapata vipigo ndani ya ndoa zao wengine ni ndugu wa karibu kabisa kwamba wanawaogopa waume zao kutokana na vipigo na wanapokuwa hawapo nyumbani wanajiona wako huru zaidi lakini waume wakirudi tu basi uoga huwajaa kwa kujua kosa dogo linaweza kusababisha kipigo.

Kutofautiana hakuna tatizo lolote au vinginevyo tungekuwa tunakubaliana kila kitu basi hili jamvi lingekuwa halina mvuto kabisa. Bado msimamo wangu ni ule ule kwamba hakuna sababu yoyote ya mke kumuogopa mumewe bali anatakiwa kumuheshimu. Ukiona mke anamuogopa mumewe basi ujue kuna walakini wa namna moja au nyingine.
 
Hii sredi imetulia sana kwa wadada, ubarikiwe mama.
Ufafanuzi : Lawyer nikisema sredi imetulia basi ujue ina hazi ya kimataifa

Hahaha asante klorokwini au lawyer kama unavyoitwa/jiita.

fazaa
Wewe ndio msemaji wa Mungu? Hayo unayoongea umeyapata wapi? Kama ni maoni yako tu basi yabaki kama yalivyo, ila kama una uhakika kwamba Mungu ndivyo anavyofanya kazi naomba vilelezo vya uhakika.

majany
Hilo nalo linahusika kwakweli.Mwanamke kujituma na sio kubweteka.
 
Last edited by a moderator:
Nimekubali point nyingi hasa za wale wanaotaka kuolewa; ila kwa wenye ndoa maisha ni more complicated na wengi tu wenye heshima kwa waume zao ndoa zao ziko ndivyo sivyo. Na huwezi sema kuwa mumeo achiti ni siri ya moyo wake; ila ni vizuri ku think positive na kujipa moyo.

Inategemea na mume ulo nae; wengine hata walambwe hawakamatiki. Hence it takes two.
 
58 Reactions
Reply
Back
Top Bottom