Sabi Sanda
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 409
- 31
Wakuu,
Kutokana hali halisi iliyopo nchini mwetu, natumaini wote tunakubaliana kuwa Rushwa ni tatizo kubwa sana nchini na kimsingi tatizo hili linastahili kuitwa JANGA LA KITAIFA.
Pamoja na juhudi na njia nyingine ambazo zinatumika katika kutatua tatizo hili kama kuboresha mishahara na kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya Rushwa, naomba mliruhusu kupendekeza njia ifuatayo ili kukomesha Rushwa nchini.
Njia inayopendekezwa ni kufanya marekebisho ya sheria ili adhabu kwa mtu ambaye atatiwa hatiani na mahakama kwa tuhuma za Rushwa iwe ni KIFUNGO CHA MAISHA. Kifungo hiki kiambatane na VIBOKO 30 SIKU YA HUKUMU NA VIBOKO KUMI KILA MWEZI KWA MUDA WOTE MUHUSIKA ATAKAOISHI GEREZANI. Adhabu hii ya Kifungo cha Maisha na VIBOKO itolewe pia kwa wale wote wanaofuja fedha na rasilimali za taifa (Rejeeni Reports za CAG za kila mwaka) na wale wanao tumia madaraka yao vibaya na kulitia hasara taifa letu.
Naomba kuwasilisha.
Kutokana hali halisi iliyopo nchini mwetu, natumaini wote tunakubaliana kuwa Rushwa ni tatizo kubwa sana nchini na kimsingi tatizo hili linastahili kuitwa JANGA LA KITAIFA.
Pamoja na juhudi na njia nyingine ambazo zinatumika katika kutatua tatizo hili kama kuboresha mishahara na kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya Rushwa, naomba mliruhusu kupendekeza njia ifuatayo ili kukomesha Rushwa nchini.
Njia inayopendekezwa ni kufanya marekebisho ya sheria ili adhabu kwa mtu ambaye atatiwa hatiani na mahakama kwa tuhuma za Rushwa iwe ni KIFUNGO CHA MAISHA. Kifungo hiki kiambatane na VIBOKO 30 SIKU YA HUKUMU NA VIBOKO KUMI KILA MWEZI KWA MUDA WOTE MUHUSIKA ATAKAOISHI GEREZANI. Adhabu hii ya Kifungo cha Maisha na VIBOKO itolewe pia kwa wale wote wanaofuja fedha na rasilimali za taifa (Rejeeni Reports za CAG za kila mwaka) na wale wanao tumia madaraka yao vibaya na kulitia hasara taifa letu.
Naomba kuwasilisha.