Namna ya ku-unhide mafaili ambayo hayaonekani kwenye flash disk kwa kutumia command

MAHENDEKA

JF-Expert Member
Jul 9, 2010
308
153
NAMNA YA KU-UNHIDE MAFAILI AMBAYO HAYAONEKANI KWENYE FLASH DISK KWA KUTUMIA COMMAND LINE(DOS)
KWA WINDOWS OPERATING SYSTEM

Wakati mwingine unaweza ukasave mafaili au mafolder kadhaa kwenye flash disk lakini baadae ukija kuifungua flash disk kwenye computer unakuta flash haina kitu,yaani iko empty..Maana yake ni kwamba mafaili hayo yapo humohumo kwenye flash disk lakini yamekuwa hidden usiyaone..Sasa kama unataka kuyaona tena(kuya-unhide) fuata maelekezo yafuatayo:

1.click startbutton iliyopo kwenye desktop, then click run, halafu andika neno cmd au command,baada ya hapo press enter..{black screen itafunguka hii kitaalamu huitwa DOS au Disk Operating System)
Hapo kwenye black screen andika Drive letter ya Flash disk yako kama inavyosomeka kwenye computer kabla hujaifungua au baada yaku-click mycomputer{mfano flash yangu inasomeka hivi (F:)MAHENDEKA },

2.Ntaandika F: halafu nita-press enter { NOTEHapo mbele ya F kuna full colon:)) na sio semi colon(;)}

3.Andika maneno attrib -r -a -s -h /s /d halafu press enter

4.Baada ya hapo nenda kaifungue tena flash yako mafaili yote ambayo yalikuwa hidden yataonekana!!!!

NAMNA YA KU-HIDE LOCAL DISK ISIONEKANE KWA KUTUMIA COMMAND LINE{DOS}

Unapo-click icon ya Mycomputer kwenye computer yako utaona screen ambayo ina icon zifuatazo
(C:)Local Disk , (D:)Local Disk , na (E:)Local Disk .Unaweza ku-hide(kuficha) local disk D, na local disk E isionekane pindi mtu mwingine atapofungua computer yako.Lakini huwezi ku-hide local disk C kwa sababu program zote zinazoload wakati computer inawake hukaa kwenye local disk C ,na endapo utajaribu kui-hide command hazitakubali.Sasa kama unataka kuhide local disk D,isionekane fuata maelekezo yafuatayo

1.click startbutton iliyopo kwenye desktop, run, halafu andika neno cmd au command,baada ya hapo press enter..{black screen itafunguka hii kitaalamu huitwa DOS au Disk Operating System)

2.Andika neno Diskpart halafu press enter

3.Andika maneno Show diskpart halafu press enter

4.Andika maneno select volume D halafu press enter {pia unaweza kuandika select volume E kama unataka ku-hide local disk E badala ya local disk D}

5.Andika maneno remove letter = D halafu press enter{ hapa pia unaweza kuandika remove letter= E kama unataka ku-hide local disk E badala ya local disk D}

6.Baada ya hapo restart computer.Itakapowaka tena local disk D HAITAONEKANA ,ITAKUWA HIDDEN TAYARI

NA ENDAPO UTATAKA KU-UNHIDE LOCAL DISK AMBAYO UMEI-HIDE FUATA MAELEKEZO YAFUATAYO

1. 1.click startbutton iliyopo kwenye desktop, run, halafu andika neno cmd au command,baada ya hapo press enter..{black screen itafunguka,screen hii kitaalamu huitwa DOS au Disk Operating System)

2.Andika neno Diskpart halafu press enter

3.Andika maneno Show diskpart halafu press enter

4.Andika maneno select volume = 2 halafu press enter{Hapa tunatumia namba badala ya herufi, namba 1.inawakilisha local disk C,namba 2.inawakilisha local disk D,namba 3.Inawakilisha local disk E…mimi nataka ku-unhide local disk D ambayo nilii-hide mwanzoni ndio maana nimetumia namba 2}

5.Andika maneno assign letter = D halafu press enter

6.Baada ya hapo restart computer yako.Pindi itakapowaka local disk D ambayo ilikuwa hidden itaonekana tena kama zamani!!!


……………………THE LITTLE I HAVE I SHARE WITH OTHERS………………………
 
Hongera..sana na asante sana....tuwe makini...twaweza potezaa kabsaa kila kitu..ni mtazamo tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom