Naliona anguko la Kibanda

Kwa kazi hii uliyomfanyia Mbowe(Mkurugenzi wako) ya kummaliza Zitto sidhani kama deni alilokukopesha atakudai tena.

swali jee makala haya ya kumchafua Zitto kabwe na kina KITILA ndio ulikuwa unataka huruma ya MKURUGENZI WAKO juu ya deni alilokukopesha?

KIBANDA umewahi kuandika makala kwenye Tanzania Daima juu ya siasa za Mbeya na Makundi yaliyopo kumsakama Mwandosya naomba ubishe hili?
jana hukuonekana hapa jamvini au ulikuwa kwenye PARTY ya kupongeza ya kamati ya Mbowe?

Childish!
 
Hivi jamani huyu Kibanda ni Mpiga kura wa Chadema? Maana kama kweli zito alikuwa anadhamira ya kweli na sio kutafuta kurudi ulingoni hapakuwa na sababu ya kutoa jina. Angeacha demokrasia ifuate mkondo wake na alikuwa na support ya ndani na nje ya Chama.

Kibanda alitumia uhuru huo huo alioutumia Zito kutoa maoni yake kupitia makala zake za Tuendako. Labda ningewaomba sana wachangiaji twende mbali zaidi ya hizi tuhuma kwa kuangalia nani alimshawishi Zitto Kugombea nafasi hiyo. Pia Tujiulize kwamba tangu Zitto alipoingia kwenye tume ya kupitia upya mikataba ya Madini, amebakia yuleyule au kawa na mtazamo tofauti na alivyokuwa mwaka 2007?

Katika kwenda mbali zaidi tutamsaidia hata kumjenga kijana mwenzetu Zitto Kabwe kwa miaka ijayo. Zitto anasema hakuwa na mpango wa kugombea isipokuwa alifuatwa na wazee na ndio maaana hata fomu za Uongozi alijaza akiwa uwanja wa Ndege.

Hii ni kauli ya ajabu sana kwamba mwenyekiti wetu anayetaka kuongoza chama hajawahi kuwa na vission ya muda mrefu mpaka afuatwe na kundi fulani la watu ambalo kwaza hatujui lina maslahi ghani na limetumwa na nani.

Imekuwa ni tabia ya viongozi wetu kudai ooh niligombea kwa sababu niliombwa na wananchi ili niwatumikie! Huu ni Mzaha. Lakini pia ni kwa kiasi ghani Zito anaijua vizuri Chadema? Uongozi wa juu unapatikanaje? Wabunge wa viti maalumu wanapatikanaje? Kwa demorasia? Ukanda? Ukabila? Kuachiana au la?

Kama tunataka kuijua vizuri Chadema turudi nyuma tangu 1992 then tutapata namna unavyoweza kuwa kiongozi wa juu katika Chama hiki. Zitto ni Kiongozi anayeinukia lakini yuko too ambitious, anataka kukimbia pale anapotakiwa kutembea kwanza.

Lazima akae chini atulie wakati utafika atakuwa huko juu ila asitumie ghiliba za marafiki toka CCM, maana wengi wa hao wanaojiita vijana, wameshajua udhaifu wake uko wapi na wanampango Mahsusi.

Sio siri, Kumbe haya ya Zitto tumeyaona tangu NCCR, na yanaendelea sana tu, na wahusika wengine wanatoka hata idara za usalama. Mambo haya ni Zaidi ya huyu Mswahili Kibanda, yana mapana na marefu.
 
Tatizo lako kibanda ni kwamba umeonyesha dhahiri kumshambulia zitto kwa sababu kaamua kupambana na mkurugenzi wako.
Kwenye makala zako uliandika kuwa mmekuwa mkishauriana sana na zitto katika mambo mengi lakini hilo la kuchukua fomu za kugombea uenyekiti wa chadema ili achuane na mkurugenzi wako hakuwahi kukushirikisha.
Yaani unataka tuaminu kwamba wewe ndo unamuamlia nini cha kufanya?
Halafu jinsi usivyo na aibu unawashambulia watu wengine wengi tu kwa sababu ya maslahi yako binafsi.Au ndio tuamini kwamba kama mbowe hatokuwa mwenyekiti wa chadema gazeti la tanzania daima haliwezi kujiendesha?inawezekana ruzuku ya chadema ndiyo inaliendesha gazeti kwahiyo usingetaka kuona kwa namna yoyote ile mirija ya ulaji inakatwa hivi hivi ukishuhudia.
badala ya kuzungumzia mambo ya msingi, sababu za msingi za kushauri kwanini zitto asigombee uenyekiti umeishia kupiga majungu tu.
Kwa jinsi ulivyomshambulia zitto sishangai maneno ya watu kwamba uko kwenye pay roll ya mafisadi. Sasa vijana wa chadema unawatukana bila aibu?hivi wewe kibanda unaweza kusema una credibility ya kumfikia zitto? au kumfikia Dr. Kitila?yaani sashivi umekuwa mhariri wa hovyo kabisa.


Swadakta! hapo kwenye blue umegonga ikulu! Kibanda anafahamu kuwa ustawi wa gazeti la TanzaniaDaima unaenda sambamba na uwepo wa Mbowe kwenye nafasi ya uenyekiti and vice versa.

Baada ya uchaguzi wa mkuu wa mwaka 2005 Mbowe alikuja madai eti anakidai chama mamilioni ya shilingi alizowakopesha kwenye kampeni kama nukuu ifuatayo;

Mwenyekiti kasema na matumizi mabaya huku ufisadi ukikitafuna chama kwa matumizi hewa na kwa kigezo eti wanajilipa madeni ya kampeni za mwaka 2005.
Alisisitiza kuwa madeni hayo hayatambuliki katika mfumo wa chama kwani Mbowe alikuwa anakopa hizo pesa mwenyewe, anatumia mwenyewe bila kuingiza kwenye mfumo wa chama na analeta madeni kwenye chama ili alipwe.

Lakini Mh. Wangwe alimweleza kuwa kila mtu aliyegombea mwaka 2005 alikuwa ametumia pesa je kila mgombea aliyeshinda au kushindwa aje kuleta madeni ya fedha alizotumia katika kampeni ili alipwe.

Na baadae ilidhihirika kuwa sehemu kubwa ya madeni anayodai kutaka kulipwa na chama ilikuwa ni michango ya wapenzi ili kufanikisha kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Kwa hiyo anapewa michango ya watu wanaokitakia mema chama, anasema amekikopesha na baada ya uchaguzi anadai kusamehe sehemu ya pesa hizo na kudai arudishiwe zingine.

Kwa kutumia mbinu hiyo watu waliona huyu ndio anafaa kuwa kiongozi wao kwani anaweza kujitolea katika chama kumbe mara nyingi anafanya usanii na watu wanaaminishwa usanii wake huo.

Haishangazi kuona Kibanda akimtetea "Mkurugenzi" wake kwani hakuna alie tayari kukata tawi alilo kalia!
 
KUMBE HATA HUMU KUNA MAFISADI SIFA.kwamaba wanafanya kitu ili wakashikwe mkono na spika wa bunge!!!!!!!
Yote tisa lakini ukweli unabaki palepale kwamba katika mambo ambayo chadema wameyumba,basi hili la kuinyima democracy nafasi ya kufanya kazi ni anguko kwa chama hiki.
Huenda wakawa wamemdhibiti ZITTO LAKINI UKWELI NI KWAMBA FIKRA ZA WATU bado hazijadhibitiwa wala haziwezi kudhibitiwa na hapo ndipo palipo na mzizi wa anguko la CHADEMA.uchaga uliokithiri ndani ya chama hiki ni pigo kubwa kwa taifa hili na wanademocrasia kwa ujumla.na hii kansa ya wachaga katika taifa hili sijui nani atakayefanikiwa kuiondoa kama wameweza kumdhibiti mwanasiasa mjanja na upeo mkubwa kama ZITTO.
 
Kwa mujibu wa KIBANDA kasema kuna wageni wa ajabu ajabu Chadema ambao Chadema inabidi iwachunguze sana. unajua kama na wewe mmoja wapo? toka umepewa kadi hata miezi mitatu haijafika, KIBANDA yuko makini hata ujikombe kwake.unaibu katibu mkuu huwezi kupewa.hujawahi kuhudhuria mkutano wa Chadema huu ndio mara yako ya kwanza, unawafanya Chadema wajinga wakupe cheo kienyeji? umefulia Chadema ina wenyewe.
Hamna shida kanda mbili,
Naomba uniambie kwanza cheo chako chama cha majambazi na kisha unambie wewe ndiye mgawa kadi za chadema?
Mimi niko juu mkuu jambo hili lisikuumize.
Chadema iko juu mkuu wala ujinga unaoandika hapa si kwamba haujajulikana.
Subiri kichapo 2010.
Kelele mlipiga kuanzia enzi za Wangwe mkashindwa wewe na mshikaji wako Makamba sasa mnaanza hadithi za zamani ngoja kipigo ndipo utajua kwamba ni Chadema tu chama kisichoyumba kwa propaganda mbuzi.
 
If this is the case then who should wee trust? Mbowe is accused of using Kibanda as well as free media for his personal interests, and so does Reginald Mengi; Rostam Aziz is also accused of using his media outlets for political gains and so does His Highness Aghakan etc.

Sasa tusome nini? Maana sasa inachanganya zaidi kwa mujibu wa yanayozidi kuandikwa kila siku kuhusu wahariri wetu japo sijui kama yana ukweli kiasi ghani.
May be kasome Uhuru gazeti lizilo na habari zaidi ya propaganda za kijani/#1
Bila shaka mhariri wake ni kanda mbili.
 
Mimi binafsi naamini Zitto ni genuine na aliamini anaweza kuisaidia Chadema kulivua koti la Uchagga na kuivisha mavazi ya ................
Pasco kama hii ndio ilikuwa ni ajenda yake then nilipoweka dots jazia waha. Na hivyo basi hakuwa mtu genuine.
 
Kwa kazi hii uliyomfanyia Mbowe(Mkurugenzi wako) ya kummaliza Zitto sidhani kama deni alilokukopesha atakudai tena.

swali jee makala haya ya kumchafua Zitto kabwe na kina KITILA ndio ulikuwa unataka huruma ya MKURUGENZI WAKO juu ya deni alilokukopesha?

KIBANDA umewahi kuandika makala kwenye Tanzania Daima juu ya siasa za Mbeya na Makundi yaliyopo kumsakama Mwandosya naomba ubishe hili?
jana hukuonekana hapa jamvini au ulikuwa kwenye PARTY ya kupongeza ya kamati ya Mbowe?

Kanda 2 tangu ulipospin thread yako kwamba namsakama Zitto na kisha nikaona michango yako mbalimbali ndani ya thread hiyo mara moja nilibaini kwamba wewe ni miongoni mwa vijana wajinga niliokuwa nimewataja ambao waliamua kumuunga mkono Zitto.

Jana Zitto amethibitisha uchanga wake katika JF. Your chairman material anatamba kwa kusema kuna vijana ndani ya Chadema kama Mnyika na Mrema wanamuonea wivu kwa sababu ya umaarufu wake. Hiki ni kichekesho na utoto wa mwaka ambao unaweza kushangiliwa na wajinga kama wewe kandambili peke yako na wajinga wenzako.

Endelea na kejeli zako za Kigoma lakini ujue kwamba hatua ya kwanza ya Anguko la Zitto imeshatokea, amezuiwa kuibeba ajenda ya kuwanufaisha maadui wa Chadema. Amethibitishiwa tu kwamba kumbe umaarufu si kila kitu katika siasa. Wazee wametumia busara na kwa taarifa yako katika kikao cha hao wazee mchagga ni Mzee Mtei mnayemsakama.

Tulishagundua ujinga wenu kwamba mnatumiwa pasipo ninyi wenyewe kujua. I'm a man of principles, sina sababu ya kushangilia ujinga na utoto kama huu ambao mnaufanya wewe, Zitto na wenzako. Mmeangushwa na sasa mnaona haya.

Kupewa mkopo ni haki yangu ya msingi na ninastahili lolote la zaidi hata kama ni huo msamaha. Kwa taarifa yako kwa kufanikiwa kumzuia Zitto na wapambe ambao hamumtakii mema yeye binafsi na ambao mko tayari kuua mafanikio makubwa ya Chadema chini ya uongozi wa Mbowe, tumeinusuru Chadema na tumewakaba koo ninyi mawakala wa CCM na wa idara yenu ya makachero.

Kweli wewe kilaza, kumbe unaandika mambo ambayo hujayafanyia utafiti. Sijapata kuandika makala ya kumsakama Mwandosya bali niliandika makala dhidi ya Kikwete na kumuuliza ana nini na mkoa wa Mbeya? Nikamhoji ni kwa nini ameamua kuteua mawaziri wawili kutoka wilaya moja (Mwandosya na Mwakyusa?)

Mwenzako aliyeweka thread hii amenisakama kwa kuendelea kulia na kumuombolezea Mwandosya tangu alipoangushwa na Kikwete na wewe unaandika nimemsakama Mwandosya. Upuuzi mtupu. Ninyi ni vijana ambao uwezo wenu wa kufikiri umepwaya endelea kujianika JF, mwisho tutaacha kusoma kila aina ya upuuzi unaotuwekea.

Kidogo kidogo ujinga wenu unajifunua. Ole wenu upumbavu unaelekea kuwakumba kwa sababu mmekumbatia upuuzi.
 
Kibanda, hili la kutumiwa kumshambulia Spika Sitta vipi? Nalo limevuma sana.


MzeePunch sina sababu hata moja ya kumshambulia Spika Sitta. Siku zote nimeepuka kushambulia watu. Kama mwandishi naandika makala za kukosoa ambazo kwa wengi tafsiri yake imekuwa ni kushambulia. Labda nielezwe tofauti ya 'criticism' (ukosoaji) and 'attacking' (kushambulia).

Nimeruhusu kuchapwa kwa makala za watu waliokuwa wakimkosoa Sitta nikiamini kwamba wanafanya hivyo kutimiza wajibu wao. Ni bahati mbaya sana kwamba kumbe sikujua kwamba Sitta alikuwa na anaendelea kuwa mtu anayepaswa kusifiwa kila siku na si kuguswa na mashabiki wake wakatokea kupinga makala zile.

Makala zile zilipoendelea, na habari mbili au tatu zikaandikwa na waandishi wa habari dhidi ya Sitta, basi spika huyo akaibuka bungeni na kulitaja Tanzania Daima kuwa moja ya magazeti yanayotuhumiwa kumchafua.

Baada ya tuhuma hizo dhidi ya Tanzania Daima nikaandika makala ya kumjibu spika nikikosoa utamaduni wa kudhani kwamba watu huwa hawawezi kuandika fikra zao pasipo kutumiwa. Ugonjwa huu wa kutilia shaka kila jambo badala ya kufikiri umekuwa ukininyima raha sana.

Majibu yangu ya kumshangaa Sitta ndiyo yakawapa makuwadi wa mwanasiasa huyo na wale wanaodai wanapambana na ufisadi mlango wa kusema eti ninamshambulia spika.
 
Kibanda,
Mkuu wangu nikuulize.. wewe unasema ni mwandishi wa habari au sio? inakuwaje wewe huyo huyo unakuwa mtetezi wa Mnyika na Mrema dhidi ya Zitto wakati sidhani kama unaelewa hisia za hao watu.
Kama mwandishi mzuri kwa nini suikimbilie kwa Mnyika na Mrema ukawasikiliza wao wenyewe wanasema nini badala ya wewe mkuu wangu kuendeleza tungo zako ambao hazimsaidii mtu yeyote yule. Mkuu enough! unachosha sana yaani kama mimi ningekuwa Mbowe au mhariri wa Daima basi huna kazi!..
Reporter siku zote huandika maelezo ya watu na sio yake yeye kwa jinsi anavyojishirikisha ktk scandal kisha anakuwa mwandishi.. Haya ni matumizi mabaya sana ya madaraka sawa na Fisadi ambaye anatumia vibaya madaraka yake. Kama wewe ni mwandishi bakia kuwa mwandishi na kama unaandika kama Kibanda zungumza kama Kibanda mpinzani wa Zitto na ukubali kukosolewa pia.
 
Jana Zitto amethibitisha uchanga wake katika JF. Your chairman material anatamba kwa kusema kuna vijana ndani ya Chadema kama Mnyika na Mrema wanamuonea wivu kwa sababu ya umaarufu wake. Hiki ni kichekesho na utoto wa mwaka ambao unaweza kushangiliwa na wajinga kama wewe kandambili peke yako na wajinga wenzako.

Endelea na kejeli zako za Kigoma lakini ujue kwamba hatua ya kwanza ya Anguko la Zitto imeshatokea, amezuiwa kuibeba ajenda ya kuwanufaisha maadui wa Chadema. Amethibitishiwa tu kwamba kumbe umaarufu si kila kitu katika siasa. Wazee wametumia busara na kwa taarifa yako katika kikao cha hao wazee mchagga ni Mzee Mtei mnayemsakama.

Tulishagundua ujinga wenu kwamba mnatumiwa pasipo ninyi wenyewe kujua. I'm a man of principles, sina sababu ya kushangilia ujinga na utoto kama huu ambao mnaufanya wewe, Zitto na wenzako. Mmeangushwa na sasa mnaona haya.

Kupewa mkopo ni haki yangu ya msingi na ninastahili lolote la zaidi hata kama ni huo msamaha. Kwa taarifa yako kwa kufanikiwa kumzuia Zitto na wapambe ambao hamumtakii mema yeye binafsi na ambao mko tayari kuua mafanikio makubwa ya Chadema chini ya uongozi wa Mbowe, tumeinusuru Chadema na tumewakaba koo ninyi mawakala wa CCM na wa idara yenu ya makachero.

Kidogo kidogo ujinga wenu unajifunua. Ole wenu upumbavu unaelekea kuwakumba kwa sababu mmekumbatia upuuzi.

Kibanda, nimependa ukweli wako na daring yako kaka!! wasiwasi wangu ni:
Je hauoni wewe kuja kushambuliana na kusutana na watu humu jamvini kuhusu mambo yenu ya ndani ni hatari kwa chama chenu?
Hamuoni mnaanza kuanika personalities zenu humu??
Sasa kwa staili hii, inawezekana kweli ukatoa fair appraisal au article that will be positive to Zitto na wenzake??
Where is the party protocol in addressing leaders issues?
Kwa jinsi ulivyoongea humu, it is deffo that Zitto has no place in CHADEMA, na umeshangilia anguko lake!! Who do you represent in all this??

Siri za ndani, bakizeni ndani!!! Haya mngeachia wakuu waje wayaweke smooth, not sure you were the right person to come up and expose things

 
Kibanda, nimependa ukweli wako na daring yako kaka!! wasiwasi wangu ni:
Je hauoni wewe kuja kushambuliana na kusutana na watu humu jamvini kuhusu mambo yenu ya ndani ni hatari kwa chama chenu?
Hamuoni mnaanza kuanika personalities zenu humu??
Sasa kwa staili hii, inawezekana kweli ukatoa fair appraisal au article that will be positive to Zitto na wenzake??
Where is the party protocol in addressing leaders issues?
Kwa jinsi ulivyoongea humu, it is deffo that Zitto has no place in CHADEMA, na umeshangilia anguko lake!! Who do you represent in all this??

Siri za ndani, bakizeni ndani!!! Haya mngeachia wakuu waje wayaweke smooth, not sure you were the right person to come up and expose things
Thank U..yaani sina la kuongezea. Hii ndio taabu ya vijana wadogo kuchukua madaraka makubwa wasijue wajibu wao..
 
Kanda 2 tangu ulipospin thread yako kwamba namsakama Zitto na kisha nikaona michango yako mbalimbali ndani ya thread hiyo mara moja nilibaini kwamba wewe ni miongoni mwa vijana wajinga niliokuwa nimewataja ambao waliamua kumuunga mkono Zitto.

Jana Zitto amethibitisha uchanga wake katika JF. Your chairman material anatamba kwa kusema kuna vijana ndani ya Chadema kama Mnyika na Mrema wanamuonea wivu kwa sababu ya umaarufu wake. Hiki ni kichekesho na utoto wa mwaka ambao unaweza kushangiliwa na wajinga kama wewe kandambili peke yako na wajinga wenzako.

Endelea na kejeli zako za Kigoma lakini ujue kwamba hatua ya kwanza ya Anguko la Zitto imeshatokea, amezuiwa kuibeba ajenda ya kuwanufaisha maadui wa Chadema. Amethibitishiwa tu kwamba kumbe umaarufu si kila kitu katika siasa. Wazee wametumia busara na kwa taarifa yako katika kikao cha hao wazee mchagga ni Mzee Mtei mnayemsakama.

Tulishagundua ujinga wenu kwamba mnatumiwa pasipo ninyi wenyewe kujua. I'm a man of principles, sina sababu ya kushangilia ujinga na utoto kama huu ambao mnaufanya wewe, Zitto na wenzako. Mmeangushwa na sasa mnaona haya.

Kupewa mkopo ni haki yangu ya msingi na ninastahili lolote la zaidi hata kama ni huo msamaha. Kwa taarifa yako kwa kufanikiwa kumzuia Zitto na wapambe ambao hamumtakii mema yeye binafsi na ambao mko tayari kuua mafanikio makubwa ya Chadema chini ya uongozi wa Mbowe, tumeinusuru Chadema na tumewakaba koo ninyi mawakala wa CCM na wa idara yenu ya makachero.

Kweli wewe kilaza, kumbe unaandika mambo ambayo hujayafanyia utafiti. Sijapata kuandika makala ya kumsakama Mwandosya bali niliandika makala dhidi ya Kikwete na kumuuliza ana nini na mkoa wa Mbeya? Nikamhoji ni kwa nini ameamua kuteua mawaziri wawili kutoka wilaya moja (Mwandosya na Mwakyusa?)

Mwenzako aliyeweka thread hii amenisakama kwa kuendelea kulia na kumuombolezea Mwandosya tangu alipoangushwa na Kikwete na wewe unaandika nimemsakama Mwandosya. Upuuzi mtupu. Ninyi ni vijana ambao uwezo wenu wa kufikiri umepwaya endelea kujianika JF, mwisho tutaacha kusoma kila aina ya upuuzi unaotuwekea.

Kidogo kidogo ujinga wenu unajifunua. Ole wenu upumbavu unaelekea kuwakumba kwa sababu mmekumbatia upuuzi.

Kibanda,

Hivi kweli wewe ni mhariri mkuu wa gazeti linalosomwa nchi nzima? Kama ni kweli basi nchi iko kwenye matatizo makubwa sana kimaadili na kiuwezo.

Naona umeshindwa hata kuelewa alichoandika Kanda2 kuhusu siasa za Mbeya; sijaona aliposema wewe ulimsakama prof. Mwandosya na badala yake uliandika habari za makundi yanayomsakama Mwandosya.

Unavyomwelezea Zitto ni kama una chuki kubwa sana, why? Pia kama mwajiriwa wa Mbowe ulitakiwa ukae kimya kabisa katika mjadala huu kwasababu issue ya conflict of interest iko wazi mno.

Tulieni vinginevyo mtakichana chana hicho chama chenu. Tanzania inahitaji upinzani wenye nguvu hasa katika kipindi hiki. Sasa kama wenyewe mnaanza kuraruana tena mbele ya kadamnasi inakuwa balaa na aibu kubwa kwa chama na taifa. Please stop washing you dirty, stinky running laundry in public.
 
Thank U..yaani sina la kuongezea. Hii ndio taabu ya vijana wadogo kuchukua madaraka makubwa wasijue wajibu wao..

Actually kwa jinsi Kibanda alivyojieleza na considering his relation with Mbowe... He has just smeared Mbowe more than himself!!!

Enough with bootlicker!!
 
Ndugu yangu Kibanda, baada ya 'Anguko la Zitto', nimekusoma tena kwenye 'Kibiriti Kimejaa', endelea kuutumia uhuru wako wa kutoa maoni kwa maandishi ya moto yenye kuchoma mithili ya ndimi za moto, huku ncha ya kalamu yako ikiendelea kumwaga makali ya mithili ya upanga wa makali kuwili.Tanzania Daima Jumatano, lilikuwa gazeti langu la tatu baada ya Mwanahalisi na Raia Mwema, sasa ndilo la kwanza mengine yakifuatia, ila kwa ushauri tuu, baada ya hii seke seke ya Chadema kuisha, nakushauri uuvue Uchadema wako, vaa tenas vazi lako la taaluma ya uandishi mahiri, rudi ulingoni uendelee kutuchapia kazi kwa misingi ya impartiality na objectivity ambayo kwa sasa umeicompromise na comflict of interest ya mwajiri wako, mmiliki wa gazeti lako na ndio mwenyekiti wa chama unachokiamini kwa sasa.Kwa lugha nyingine, Waandishi hatutakiwa kufungamana na upande wowote, wewe umeamuamua kufungamana na upande wa Mbowe at the expense ya upande mwingine wa Zitto. Japo hili ni kinyume cha maadili ya uandishi lakini sio kinyume cha uhuru wako wa kutoa maoni yako.Naungana na wewe, mwandishi unapofikia mahali ukaona kuna hatari ya tishio la umani, uhuru na ustawi wa jambo unaloliamini, unaruhusiwa to take sides kwa lengo la kuepusha shari ama kunusuru jahazi lisizame, jahazi likishakaa sawa, basi Kibanda, rejea ngamani kama mwenda tezi na homo.
 
Kazi kweli kweli naona watu mnaumia sana na CHADEMA muwaache jamani wakijenge chama kuliko kuanza kuwasakama na kuwanyooshea vidole. Kweli mafisadi wanatisha yaani wamepeleka akili za wapiganaji wote CHADEMA na kuwaacha wao wakipumua.
 
Personal attack zinanoga sana katika masikio ya watu weusi, Mbowe, Zitto na Kibanda ni watu zaidi na wanapita kutokana na wakati lakini kanuni na taratibu je?. Kwa mfano mfumo wa Chadema unaruhusu mwenyekiti aliye madarakani kushindanishwa na wagombea wengine katika kinyang'anyiro cha kulinda kiti? Kama jibu ndio woga wa wapambe na wazee unatoka wapi kiasi cha kushawishi wagombea wajitoe, ni bora wazee na wapambe wakatumia ushawishi wao kubadilisha kanuni ili mwenyekiti asimame peke yake. Kama demokrasia ipo basi msingi wake watu washindane na sio kupenda ubwete.

Kuhusu taaluma ya uwandishi wa habari bongo ni tatizo kubwa sana sema limekosa msemaji mzuri ambaye anaweza kulidadavua kwa upana wake manake waandishi wa bongo wengi sio na wanafungamana sana na upande mmoja hasahasa wamiliki wa vyombo vyao na hawako huru kabisa lakini kusakama serikali ni rahisi zaidi kuliko wamiliki wa vyombo vya habari. Kibanda ni sehemu tu ya mfumo mzima usiofaa kwa maslahi ya watanzania na Tanzania kwa ujumla labda hili ndio limewagusa zaidi kama mtadurusu kazi zao za nyuma mtagundua jamaa ni makasuku tu, unaweza ukawatumia kufanya chochote manake wengi kama sio wote wamechoka na kazi zao si za uwakika.
 
Pili nimesikitishwa na uongo wa wazi unaoenezwa na baadhi ya wanajamvi kwamba eti nimenunua magari matatu. Habari hizi si za kweli hata kidogo. Mwaka huu nimenunua gari mtumba kwa fedha zangu kidogo na nyingine za kukopeshwa na mkurugenzi wangu.

Kibanda,

Hivi huo mkopo wa mkurugenzi wako unalipa riba gani? Kama hakuna riba inatakiwa TRA wakufuate na ulipie kodi.

Tushukuru Tanzania haifuati sheria hasa kwa wenye vyeo kama wewe. Kwa kutaja hapa huu mkopo wako, ingekuwa sehemu zingine wajanja wangefuatilia mpaka wakute makosa makubwa hasa upande wa kodi.

Nakushauri nyamaza tu maana ni kama unajiharibia bure. Alipoandika Masatu kwamba anguko la Kibanda nilicheka nikafikiri utani, lakini kwa yanakoenda haya naona kama unajiangusha mwenyewe.
 
Unajua Kibanda hapa naona unafaidisha wabaya wako wengi kwa kumwaga mboga bora unyamaze wengi wamezoea kudanganywa na kudanganya unapo ongea ukweli unawanufaisha kukujua in and out.
 
Back
Top Bottom