Wanauelewa mpana sana kuhusu maisha ya familia na majukumu yake, wanataka kuwa na uhakika kama una-uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya maisha ya TZ ili muweze kuwa na maisha mazuri kiuchumi kwa faida ya familia na jamii. Kumbuka maisha ya kawaida ndani ya ndoa yanachukua muda mwingi kuliko mapenzi. Mafanikio ya kimaisha yanamchango mkubwa sana katika furaha unayo ihitaji, stress za kuwaza nitakula nini au nitaishi wapi au nitasomeshaje watoto nk zinaweza changia kupunguza upendo ndani ya nyumba. Kutokana na ufahamu mkubwa wa wanawake wa kichaga kabla ya kuzama kwenye mapenzi lazima wawe na uhakika kama kweli unaweza kukabiliana na niliyoyaeleza hapo juu.