1800
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 2,215
- 603
- Thread starter
- #61
Riot inaweza kuwa hata ya mtu mmoja au wawil, funguka. Watu wanasombwa na magari na wengine wametoka toka Mbeya na Iringa mjini halafu unasema kikukndi kidogo? hivi unayaandika haswa haya kwa nia safi kabisa na wala sio kwa kubishana mradi kubisha tu?
Ukatazwe kufanya mkutano, ukafanye kwa nguvu, uambiwe sambaratika ukatae na uanzishe fujo, ukitupiwa vibomu vya machozi na wewe unashambulia kwa mawe kwa dakika 30 halafu useme hiyo siyo riot? Isitoshe wakati huohuo atoke mmoja kwa kujiona yeye ni hodari sana akamvae mkuu wa kikosi? hiyo kama si suicide ni nini?
Ukweli unabaki kuwa ukweli hauchakachuliki!
Mkuu unaweka ushabiki na hisia zako zaidi kuliko hualisia,kwanza haujanijibu kua je sheria yetu inaruhusu police kutumia risasi za moto na mabomu ya kutoa uhai katika kudhibiti riot?pili riots uwa ina involve vandalism,properties destruction je ilo ndilo lililotokea Iringa au ni police ndio walio amua kutumia nguvu za kijinga kwa watu waliokua wako katika uzinduzi wa tawi la chama chao ambapo awali waliwaruhusu lakini Rpc kwa utashi wake na maboss wake akaamua kubatilisha baada ya kufika eneo la tukio??simama kwenye fact usilete porojo Zomba