Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Source: Mange Kimambi Blog: [mods tafadhali msiondoe kama mnawatendea watanzania haki hizi ni picha zao wenyewe]
View attachment 46432View attachment 46433View attachment 46434View attachment 46435View attachment 46436View attachment 46437View attachment 46438View attachment 46439Baada ya tusi la binti mfalme kuturingishia hekalu lake [hisani ya mwandishi wake wa habari] nimeumia sana moyoni kwani nafanya kazi kwa bidii licha ya elimu yangu kubwa ambayo hainisaidii kuwalisha wanangu vizuri. napokea mshahara wa Tsh. 800,000 kwa mwezi. Nina shahada ya uzamili nimeajiriwa na taasisi ya umma, nyumba ninayoishi ni ya kupanga na malipo kwa mwezi ni Tsh 400,000 hapo makato kazini bado hela za chakula bado nauli bado. Sasa nashangaa mtoto wa kiongozi ambaye ameanza kazi nyuma yangu anakuja na jumba la billioni 3 najiuliza ni nini alichokifanya zaidi ya kujianika kwenye viombo vya habari na mablogs ambacho mimi nimeshindwa kukifanya. Mods naomba msitoe post yangu kwa maana ni la kisiasa na sijataja jina la mtu. Waache wana jukwaa walijadili mada yangu. Naomba kujua ni kitu gani wanachokidanya watoto wa viongozi wa CCM ili kupata utajiri wa haraka hivi? Naombeni mchangie mada kwa umakini na pia TAFAKARINI tunakoelekea. Tunawapigia kura alafu wanaturingia mali walizochuma . Mtakaosema wivu poleni siyo wivu. Ni usawa kwa wote. kumbukeni maisha bora kwa kila mtanzania na siyo kwa baadhi