Habari wana JF?Mimi huwa najiuliza swali moja, Watanzania tunafanya kazi saaana na tunakatwa Michango ya mifuko ya jamii kila mwezi. Hivi hatuwezi kuitumia fedha inayoingia kwenye hii mifuko ya jamii kama amana kukopa Mfano PPF, PSPF, NSSF, LAPF na n.k?Nauliza hivi kwa sababu kuna mgeni (mzungu) nilikuwa nastorisha nae (ni mwekezaji mkubwa sana) nikamuuliza jinsi yeye alivyoweza kupata mtaji mkubwa kiasi hiki (takriban milioni 200Tshs) akanijibu alikopa kupitia amana ya fedha zake zilizokuwa mfuko wa jamii aliokuwa anauchangia baada ya kufanya kazi kwa kama miaka kumi na ushee.Ndipo nikajiuliza hivi na sisi kwa nini tusitumie akaunti zetu za mifuko ya jamii kama amana ili tuweze kukopa mitaji mirefu ili kuwekeza kiukweli kuliko kukopeshana vijisenti vya kununulia radio na tv kwa kutegemea mishahara finyu? Ye mwenzetu kaniambia kwao mfanyakazi ni mtu aliyefanikiwa saaana hata kama salary ni ndogo kwani michango ya jamii huweza kuwainua sana licha ya kuwasaidia uzeeni kwani wanaweza kukopa na michango yao ikiwa ni amana na kuondokana na habari za hadi uwe na hati za nyumba/ardhi na mali isiyohamishika ambayo ni ngumu mno kuwa navyo.Sasa oneni mzungu huyu, kaanzisha kampuni huku kapanua mtaji taratiibu anaihamishia kwao baada ya kuwa na mtaji wa kutosha na kuona anaweza kushindana na wenzie huko.All in all, michango yangu kule PPF, NSSF, PSPF au kwingineko haiwezi kunidhamini nikakopa benki? Mbona kuna fwedha nyingi tuu kuliko hata hati ya nyumba au ardhi?Kwa nini sisi tushindwe????????