Najihisi nina tatizo nisaidieni

cheusimangala

JF-Expert Member
Feb 27, 2010
2,585
497
As salam aleykum wapendwa wangu.
Natumai pasaka imekua yenye furaha kwenu.

Wapendwa kwa asili mim ni mtu mwenye kupenda utani na mtu ambaye ni vigumu saaana kukasirika.Hakuna binadamu asiyekasirika lakini kwa kweli mimi Cheusie nikikasirika lazima hilo jambo litakuwa kubwa mara nyingi mim ni mtu wakufurahi na mwingi wa tabasamu usoni mwangu.

Lakini wapendwa sijui ni nini kimenipata siku za hivi karibuni,yaani ninaweza kuamka nikiwa nimejawa na hasira bila hata kuudhiwa na mtu yeyote.Yaani siku hiyo shemeji yenu nimpendae kupita maelezo kila atakaloongea nitaona linanitibua,akijaribu kujitetea kuwa hajamaanisha kitu kibaya ndio anakua kaharibu kila kitu.Yaani siku za kuamka na hasira na kuwa sijisikii kuongea na mtu yeyote.Siku kama hizi hata JF siingii sababu nikiingia naweza kujibizana na mtu vibaya nikaishia kuwa banned.

Ajabu ni kwamba kuna siku nyingine tena naamka moyo wangu unakua umejaa furaha ya ajabu,furaha ambayo sijui hata inatokea wapi.

Kuna siku naweza nikaamka nikiwa nina huzuni ya ajabu,huzuni ambayo siwezi kuelezea imesababishwa na nini.Siku hiyo naweza kujikuta najisikia kulia,kama niko nyumbani nitajitupa zangu kitandan machozi yatanitoka nitalia wee huku nikisikia huzuni kubwa moyoni mwangu.

Shemeji yenu,marafiki,wanafunzi na wafanyakazi wenzangu nahisi wamegundua kuwa siku hizi siko normal,naona wanakua kama wananisoma kwanza kuona kama leo Cheusie kaamka na mood gani,nikiwa na mood ya furaha basi wataongea na mim kama tulivyozoea siku zote,nikiwa na mood ya hasira au huzuni naona wanakua makini wakati wakuongea na mimi.

Kiukweli nahisi something is not right with me,sijui ni nini kinanisumbua,lakini najijua mimi hii sio kawaida yangu.
Je hii ndio Depression au ndio dalili za stress? Au hii ni nini jamani..

Niko serious,naombeni kama kuna mpendwa yeyote humu ndani ameshawahi kutokewa na kitu kama hiki aniambie au kama kuna wataalam mnaojua hii inasababishwa na nini mnisaidie.

Natanguliza shukrani zangu kwa mtakaonichukulia serious na kujaribu kunisaidia.
Asante.

Cheusie.
 
umeanza kuwa misllaneous na ni jambo baya mtu ambaye anakuwa hivi anakera na inakuwa vigumu kumdetermine atakuwa katika hali gani.
Inawezekana labda una msongo wa mawazo au tatizo flani linalo kusumbua ambalo hujalipatia ufumbuzi.
Sitaki ongea mengi kwakuwa mimi si mwana psychology(ia)
 
sasa nimekuelewa, kuna ziku huwa unanshangaza tu.

sea Cliff hotel, kuna wataalam wa ushauri wa mambo hayo, ni wellness program.

Au AAR head quater pale Chato Street/ally Hassan Mwinyi.

Kama uko serious utaniPM nikupe namba ya mhusika wa program hiyo.
 
kwa waafrika unaweza kuwa na tatizo la 'kutokwenda kutambika' kwenu kwa mda mrefu....

but kizungu nashauri utazame afya yako kiujumla
hebu kapime 'hormones zako' ina sound kama
kuna mvurugiko wa homones au depression au 'mzunguko wa siku zako'
au dalili ya ugonjwa mwingine
 
mie nahisi ni bipolar disorder hio,ndio inakuwaga hivyo highs and lows...muone mtaalamu..lol
 
Pole kwa hali hiyo.
ila kama uko katika hali hiyo katika avatar yako(mjamzito) hiyo ni hali ya kawaida.
Inasababishwa na mabadiliko/ongezeko la hormones katika mwili wako.
Pia sio ajabu kwa wajawazito(nisamehe kama sio mjamzito) kuwa na depression.
Hata hivyo ni vuzuri ukawaona wataalam ili wajue kiini cha hali hii hasa kama huna ujauzito.
Kama wewe ni mjamzito jitahidi usiwe unakasirika kasirika sana maana utamstress mtoto wako aliye tumboni.
Mungu ni mwema atakusaidia urudie katika ile hali yako ya zamani uliyoielezea.
 
Ohhhh kumbe ndio maana ulikuja vile juzi?

Nwy kama wewe ni mtarajiwa kama avatar yako inavyoonyeshaga(pole kama nimekuchanganya na mwingine) basi waambie wakuvumilie tu maana hizo mood swings hua.zinawasumbua kweli baadhi ya watu wenye ujauzito. Kama sio tafuta msaada wa kisaikolojia na kifizikia maana inawezekana kinachokosumbua kikawa kichwani au mwilini kwa ujumla (stress/hormones/depression n.k). Ila zaidi jitahidi kutoruhusu hisia zako hizo zinyime watu wengine raha.
 
Sorry lakini naomba kuuliza!

Hiyo Avatar yako inaonyesha kama uko mjamzito ... je kwa sasa ni mjamzito? ... kama ndio basi nafikiri hizi mood swings zitakuwa zinatokana na hiyo hali.

If you are pregnant or are supporting someone through pregnancy, you probably have had some experience with mood swings. You are not alone; mood swings are common during pregnancy. You may be excited about being pregnant, but you can also be stressed or overwhelmed.

Mood changes during pregnancy can be caused by physical stresses, fatigue, changes in your metabolism, or by the hormones estrogen and progesterone.

Significant changes in your hormone levels can affect your level of neurotransmitters, which are brain chemicals that regulate mood. Mood swings are mostly experienced during the first trimester between 6 to 10 weeks and then again in the third trimester as your body prepares for birth.
 
hiyo avatar ni miaka miwili now
sio ujauzito itakuwa some disease...for sure

ushauri wangu muone dokta fasta
 
sasa nimekuelewa, kuna ziku huwa unanshangaza tu.

sea Cliff hotel, kuna wataalam wa ushauri wa mambo hayo, ni wellness program.

Au AAR head quater pale Chato Street/ally Hassan Mwinyi.

Kama uko serious utaniPM nikupe namba ya mhusika wa program hiyo.

thanx kongosho,ila siko Dar ila nitatafuta wataalam huku nilipo.
 
kwa waafrika unaweza kuwa na tatizo la 'kutokwenda kutambika' kwenu kwa mda mrefu....

but kizungu nashauri utazame afya yako kiujumla
hebu kapime 'hormones zako' ina sound kama
kuna mvurugiko wa homones au depression au 'mzunguko wa siku zako'
au dalili ya ugonjwa mwingine

Thanx kwa ushauri,kwetu ninakwenda bila shida ila siamini katika matambiko.
Ila hayo mengine uliyonishauri nitayazingatia.
 
mie nahisi ni bipolar disorder hio,ndio inakuwaga hivyo highs and lows...muone mtaalamu..lol

namshukuru Mungu leo nimemka moyo wangu umejaa furaha maana...
Ila labda mwaya maana hata hao wenye bipolar hawakuomba kuwa hivyo na yeyote anaweza kuwa hivyo au kuzaa mtoto wa hivyo(God forbid).
 
Ohhhh kumbe ndio maana ulikuja vile juzi?

Nwy kama wewe ni mtarajiwa kama avatar yako inavyoonyeshaga(pole kama nimekuchanganya na mwingine) basi waambie wakuvumilie tu maana hizo mood swings hua.zinawasumbua kweli baadhi ya watu wenye ujauzito. Kama sio tafuta msaada wa kisaikolojia na kifizikia maana inawezekana kinachokosumbua kikawa kichwani au mwilini kwa ujumla (stress/hormones/depression n.k). Ila zaidi jitahidi kutoruhusu hisia zako hizo zinyime watu wengine raha.

Juzi nilikua kawaida tu sikua na shida yeyote,nilitoa tu mtizamo wangu.

Asante kwa ushauri mzuri,nitautendea kazi.
Kusema kweli huwa sometimes nashindwa kuact normal japo najua kwa mfano ninapoamua kutoongea na mtu, huyo mtu anajisikia vibaya.
 
hiyo avatar ni miaka miwili now
sio ujauzito itakuwa some disease...for sure

ushauri wangu muone dokta fasta

ushauri wa kumuona dokta naupokea ila hayo mengine mmmh.
Boss sijui kwa nini unanichukia lol
 
Juzi nilikua kawaida tu sikua na shida yeyote,nilitoa tu mtizamo wangu.

Asante kwa ushauri mzuri,nitautendea kazi.
Kusema kweli huwa sometimes nashindwa kuact normal japo najua kwa mfano ninapoamua kutoongea na mtu, huyo mtu anajisikia vibaya.
Mtizamo mtizamo haswa!!!

Nwy. . .Kila la kheri...angalia watu wasije wakakukimbia.
 
Mtizamo mtizamo haswa!!!

Nwy. . .Kila la kheri...angalia watu wasije wakakukimbia.

kwani mbona ni vitu vingi naandika lakini sielewi kwanini ile ya juzi imekugusa namna hiyo.
anyway my dear,watu hawatanikimbia,huwezi kuamini huko mtaani watu wananipenda sana,sema tu nikinuna wanamiss ucheshi wangu.Na mtu ukishagundua una tatizo basi ni mwanzo wa tiba wa hilo tatizo.Ushauri mnaonipatia mpaka dakika umenisaidia kwa kiasi kikubwa tu na Mungu awabariki kwa hilo na ninashukuru.
 
Back
Top Bottom