Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,720
- 155,326
View attachment 11955RAIS Jakaya Kikwete ameushangaza umma wa Watanzania baada ya kuanza kukiuka misingi iliyokiunda Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kuwaheshimu Wakulima na Wafanyakazi pale alipokutana na wazee wa MSkoa wa Dar es Salaam na kutoa hotuba kali akiwashutumu viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafabnyakazi Nchini (Tucta) kuwa ni wanafiki kwa kuendelea kushinikiza mgomo wa wafanyakazi licha ya mazungumzo yanayoendelea kati yao na Serikali.
Hawa viongozi wa Tucta walisema sisi serikali ni watu wasioambilika hawa viongozi wa Tucta ni waongo, alisema Rais Kikwete akisisitiza kuwa hii ni moja ya sababu iliyomfanya jana awajibike kujibu.
Sasa iweje tunakubaliana hili, kesho yake asubuhi unazungumza kama hatujakubaliana, alisema Rais na kusisitiza: Ninayo kila sababu kuhoji dhamira zao iwapo kweli wana nia thabiti ya kuwabeba wafanyakazi ama wana lao jambo.
Hawa viongozi wa Tucta walisema sisi serikali ni watu wasioambilika hawa viongozi wa Tucta ni waongo, alisema Rais Kikwete akisisitiza kuwa hii ni moja ya sababu iliyomfanya jana awajibike kujibu.
Sasa iweje tunakubaliana hili, kesho yake asubuhi unazungumza kama hatujakubaliana, alisema Rais na kusisitiza: Ninayo kila sababu kuhoji dhamira zao iwapo kweli wana nia thabiti ya kuwabeba wafanyakazi ama wana lao jambo.