Naibu Waziri wa Mambo ya ndani asitisha Uraia wa Warundi 162,000

sagamawe

Senior Member
Aug 3, 2012
148
36
Nimesikia majuzi kuwa Naibu waziri wa mambo ya ndani amesitisha utoaji wa uraia wa watu 162,000 ambao hapo awali Lawrence Masha alikuwa ametangaza kuwapatia uraia wakati akiwa bado waziri. Mwenye habari zaidi naomba anijuze. Aksante
 
Hili suala la utoaji wa uraia kwa wageni yafaa litafutiwe utarabu mzuri katika katiba mpya,utaratibu wa sasa unawapa wanasiasa mwanya wa kutuchezea namna watakavyo.
 
wiki chache zilizopita niliona watu zaidi ya 100 (website ya uhamiaji) wenye majina ya kisomali wamefutiwa uraia wa tz kwasababu walijipatia uraia kwa njia zisizo halali na ninavyofahamu anayeidhinisha uraia ni waziri pekee... ni swala la kuhoji ilikuwa vipi mpaka waziri kutoa uraia kwa watu wasiostaili?
 
Amesimamisha zoezi la utoaji uraia(baadhi walishapatiwa) ili kupata maoni ya wanaodaiwa kuwa wadau ambao inatamkwa kuwa hawakushirikishwa ktk mchakato huo.Hata hvyo kama wewe ni mmoja wao au jamaa yako yumo,usiwe na hofu kabisa.Makambi yote ya wakimbizi yalishafungwa(mwezi wa nane tumefunga kambi ya mwisho) na kwa mjibu wa mapatano ya TZ na UNHCR,tanzania hakuna mkimbizi tena.Wakimbizi waliochaguwa kubaki tz( 162,000) ni lazima watambuliwe kama jamii ya tz lkn utaratibu wa kuwatambua ndio bado unajadiliwa upya.Leo kuna kikao cha wawakilishi wao(vijana wasomi),ujumbe wa wizara na mwakilishi wa UNHCR.Nikirudi ofsini after a week ninaweza kukuhabarisha kama maamuzi yao hayatakuwa confidential!
 
Amesimamisha zoezi la utoaji uraia(baadhi walishapatiwa) ili kupata maoni ya wanaodaiwa kuwa wadau ambao inatamkwa kuwa hawakushirikishwa ktk mchakato huo.Hata hvyo kama wewe ni mmoja wao au jamaa yako yumo,usiwe na hofu kabisa.Makambi yote ya wakimbizi yalishafungwa(mwezi wa nane tumefunga kambi ya mwisho) na kwa mjibu wa mapatano ya TZ na UNHCR,tanzania hakuna mkimbizi tena.Wakimbizi waliochaguwa kubaki tz( 162,000) ni lazima watambuliwe kama jamii ya tz lkn utaratibu wa kuwatambua ndio bado unajadiliwa upya.Leo kuna kikao cha wawakilishi wao(vijana wasomi),ujumbe wa wizara na mwakilishi wa UNHCR.Nikirudi ofsini after a week ninaweza kukuhabarisha kama maamuzi yao hayatakuwa confidential!


Kambi ya mtabila itafungwa mwishoni mwa mwaka huu na ya Nyarugusu bado haijafungwa. Kambi ipi ya mwisho iliyofungwa?
 
Kambi ya mtabila itafungwa mwishoni mwa mwaka huu na ya Nyarugusu bado haijafungwa. Kambi ipi ya mwisho iliyofungwa?

Mwezi wa nane ulikuwa mwezi wa mwisho kutambua uwepo wa kambi ya Nyarugusu.Kama bado kuna wakimbizi hawajaondolewa ni matokeo ya udhaifu ktk utaratibu wa kuwasafirisha.
 
Mwezi wa nane ulikuwa mwezi wa mwisho kutambua uwepo wa kambi ya Nyarugusu.Kama bado kuna wakimbizi hawajaondolewa ni matokeo ya udhaifu ktk utaratibu wa kuwasafirisha.

unamaanisha Mtabila? Maana wakimbizi wa kutoka Burundi waliokuwa wakiishi mtabila ndio walioondolewa hadhi ya ukimbizi mwezi wa nane, na si wakimbizi wa kutoka DRC waliopo kambo ya Nyarugusu.
 
Naomba mwenye kujual hili atufafanulie; kisheria nani mwenye mamlaka ya 'kusitisha' au kutoa uraia? waziri au naibu waziri, au katibu au nani?
 
Amesimamisha zoezi la utoaji uraia(baadhi walishapatiwa) ili kupata maoni ya wanaodaiwa kuwa wadau ambao inatamkwa kuwa hawakushirikishwa ktk mchakato huo.Hata hvyo kama wewe ni mmoja wao au jamaa yako yumo,usiwe na hofu kabisa.Makambi yote ya wakimbizi yalishafungwa(mwezi wa nane tumefunga kambi ya mwisho) na kwa mjibu wa mapatano ya TZ na UNHCR,tanzania hakuna mkimbizi tena.Wakimbizi waliochaguwa kubaki tz( 162,000) ni lazima watambuliwe kama jamii ya tz lkn utaratibu wa kuwatambua ndio bado unajadiliwa upya.Leo kuna kikao cha wawakilishi wao(vijana wasomi),ujumbe wa wizara na mwakilishi wa UNHCR.Nikirudi ofsini after a week ninaweza kukuhabarisha kama maamuzi yao hayatakuwa confidential!

Mkuu uko ofisi gani wewe?

Nakubaliana na wewe kuhusu kutoa uraia lakini sikubaliani na wewe kuhusu kufungwa makambi kwamba mwezi wa nane mmefunga kambi ya mwisho. Siyo kweli mkuu! Kambi iliyofungwa ni ile ya Warundi (Mtabila) lakini bado tuna kambi moja ilyobaki ambayo ina wakimbizi zaidi ya 60,000 (Nyarugusu) ambayo inahifadhi wakimbizi wa kutoka Congo. Hivyo kwa wale wa Mtabila ambao wameonekana sababu zao ni za msingi kuendelea na ukimbizi (hii inatokana na mambo ya usalama) watahamishiwa Nyarugusu, hayo ndo makubaliano yaliyopo kwenye Tripartite Commision (Burundi, Tanzania na UNHCR).

Kwa wale 162,000 siyo rahisi kuwafutia uraia maana yalikuwa makubaliano ya hayo makundi matatu. Hapo wakuu tulishaumia lazima tukubali kwamba imeshakula kwetu!
 
Mwezi wa nane ulikuwa mwezi wa mwisho kutambua uwepo wa kambi ya Nyarugusu.Kama bado kuna wakimbizi hawajaondolewa ni matokeo ya udhaifu ktk utaratibu wa kuwasafirisha.

Mkuu usichanganye madawa!

Naona hapa unataka kutuchanganyia taarifa. Kambi ya Nyarugusu bado inatambuliwa kama kambi rasmi, hii ni kutokana na hali ilivyo DRC kwa sasa. Kati ya 2010 na 2011 kulikuwa na exchange visits nyingi zilizokuwa zinafanyika ili kuona kama hali ni shwari lakini ilikuja kuonekana kwamba isingekuwa busara kuwarudisha kwao wakati bado kuna mapigano kule kwao. Hivyo zoezi la kuwarudisha likawa limekwamba. Kwa hiyo Nyarugusu itaendelea kuwepo na baadhi ya wakimbizi wa Mtabila (wenye matatizo ya kiusalama), haya nia maamuzi yaliyotolewa baada ya indepth interview iliyofanyika kati ya Oktoba na Novemba 2011, watahamishiwa huko mara tu Mtabila itakapofungwa rasmi mwishoni mwa Disemba 2012.
 
Amesimamisha zoezi la utoaji uraia(baadhi walishapatiwa) ili kupata maoni ya wanaodaiwa kuwa wadau ambao inatamkwa kuwa hawakushirikishwa ktk mchakato huo.Hata hvyo kama wewe ni mmoja wao au jamaa yako yumo,usiwe na hofu kabisa.Makambi yote ya wakimbizi yalishafungwa(mwezi wa nane tumefunga kambi ya mwisho) na kwa mjibu wa mapatano ya TZ na UNHCR,tanzania hakuna mkimbizi tena.Wakimbizi waliochaguwa kubaki tz( 162,000) ni lazima watambuliwe kama jamii ya tz lkn utaratibu wa kuwatambua ndio bado unajadiliwa upya.Leo kuna kikao cha wawakilishi wao(vijana wasomi),ujumbe wa wizara na mwakilishi wa UNHCR.Nikirudi ofsini after a week ninaweza kukuhabarisha kama maamuzi yao hayatakuwa confidential!


Strongly kwa sababu za kiusalama warundii warwanda wote waliopewa uraia na watakaopewa uraia ....wewe relocated Hadi maeneo yenye Nafasi Kati Kati mwa nchi ....au kusini hata kaskazini ...,historian imeonyesha kuwa kawaacha hawa maeneo Yetu ya magharibi au ziwa ...lake zone miaka 20 ijayo watamega Eneo Letu kuwa nchi Hizo ambazo zinawatumia Hao waliambizi kimkakati ili kumega Eneo Letu ...na kutuletea usumbufu Kama wa Banyamulenge wanaompaa Kabila sasa Ambapo Eneo la mashariki limegeuka kama Jimbo la Rwanda....
Kwa walio serekalini hasa usalama wa Taifa na usalama wa Jeshi (MI) ...wanaujuwa Huu mikakati wa majirani zetu wa kujitwalia Kagera,Kigoma na sehemu ya Rukwa....Wazo la kuwahamishia maeneo Mbali na mpaka warundii na warwanda wanaopewa uraia lilianza toka Enzi ya utawaka wa Mwalimu ,,,ambapo aliwapa vijiji mkoani Tabora waliambizi wa mwanzo wa Rwanda wa miaka ya 60 ......
karibuni makosa yanacanyika kawaacha hawa tunaowapa uraia mikoa ya mipakanii tutakuja kuwaachia watoto wetu matatizo ......hivi karibuni Mkuu wa mkoa wa Kagera amelalamika kitendo cha majirani zetu kujipenyeza na wengine hata kupata uongozi wa mitaaa...na Kashiria uchaguzi Ujao kwa wingi wao wanaweza hata Kuamua Mbunge.......Ameomba pesa za kuwahamisha wahamiaji haramu kuwarudisha makwao....ni vema akapewa.....
pia inashaauriwa ianzishwe security strip Kuanzia Kagera ...Hadi Kigoma usawa wa mipakanii tuweke mashamba ..makubwa ya kilimo yamilikiwe na Jeshi ..JkT ...hata Kama wataweka wawekezaji ....but this area is vulnerable need to be owned by defence..hawa raia wanarubuniwa wanauzia wageni maeneo ya mipakanii ni hatari...na wanaonunua wanfadhiliwa na agencies za majirani ...Kama sehemu ya mikakati
 
Kuna wakimbizii wa Somalia wamepewa Eneo Soni ,Tanga...hawa inasadikika kuwa hawa Hilo lilikuwa eneo Lao la Asili na walihamia Somalia miaka 150 iliyopita ....na wanatambulika Kama jamii ya waswahili Somali .....at least Somali ni Mbali but strongly tutafute vijiji Mbali na mikoa ya pembezoni tuwahamiashie hawa wakimbizii 162'000 ....kwani hawa miaka 20 ..ijayo watafikia hata millions 5.....na wanafanya Ukanda wote huo uungane na Hao majirani....na mwisho wataanza kuchukua maagizo ya kiutawala toka huko....time bomb!!!!
 
Escherichia Coli jamaa yangu msije mkatutia hasira bure humu yaani wote 162,000 mnataka kuwapa Uraia wakati Zanzibar wameahidi kutoa vitambulisho vya ufanyaji kazi tu kwa wanaotoka Bara na sio vya Uraia au makazi na ina maana wafanyabiashara hawatatambuliwa Ninyi mnataka kutuingizia wengine kwanini wasipewe vya ukimbizi?
Kumbuka walikuwepo tele maofisini lakini baada ya ile ndege ya Rais wao (Habyarimana na Kagame kuchukua Nchi) walirudisha uraia na kukimbilia kwao (kuna afisa wa MAPATO enzi hizo alioa msukuma alimuacha na leo yuko kwao na Cheo kikubwa tu na kaoa Mtutsi mwenzake
Acheni kujipendekeza nampa Hongera huyo Naibu Waziri km kavifutilia mbali
 
Last edited by a moderator:
Mwezi wa nane ulikuwa mwezi wa mwisho kutambua uwepo wa kambi ya Nyarugusu.Kama bado kuna wakimbizi hawajaondolewa ni matokeo ya udhaifu ktk utaratibu wa kuwasafirisha.
Nyarugusu na Mtabila zote waliongeza muda.Mtabila sasa ni official mwisho mwezi wa 12.Nyarugusu Bado kwani wengi wanatoka East Kongo na huko bado kuna mcharuko.
 
Mkuu uko ofisi gani wewe?

Nakubaliana na wewe kuhusu kutoa uraia lakini sikubaliani na wewe kuhusu kufungwa makambi kwamba mwezi wa nane mmefunga kambi ya mwisho. Siyo kweli mkuu! Kambi iliyofungwa ni ile ya Warundi (Mtabila) lakini bado tuna kambi moja ilyobaki ambayo ina wakimbizi zaidi ya 60,000 (Nyarugusu) ambayo inahifadhi wakimbizi wa kutoka Congo. Hivyo kwa wale wa Mtabila ambao wameonekana sababu zao ni za msingi kuendelea na ukimbizi (hii inatokana na mambo ya usalama) watahamishiwa Nyarugusu, hayo ndo makubaliano yaliyopo kwenye Tripartite Commision (Burundi, Tanzania na UNHCR).

Kwa wale 162,000 siyo rahisi kuwafutia uraia maana yalikuwa makubaliano ya hayo makundi matatu. Hapo wakuu tulishaumia lazima tukubali kwamba imeshakula kwetu!
You are damn right!
 
Amesimamisha zoezi la utoaji uraia(baadhi walishapatiwa) ili kupata maoni ya wanaodaiwa kuwa wadau ambao inatamkwa kuwa hawakushirikishwa ktk mchakato huo.Hata hvyo kama wewe ni mmoja wao au jamaa yako yumo,usiwe na hofu kabisa.Makambi yote ya wakimbizi yalishafungwa(mwezi wa nane tumefunga kambi ya mwisho) na kwa mjibu wa mapatano ya TZ na UNHCR,tanzania hakuna mkimbizi tena.Wakimbizi waliochaguwa kubaki tz( 162,000) ni lazima watambuliwe kama jamii ya tz lkn utaratibu wa kuwatambua ndio bado unajadiliwa upya.Leo kuna kikao cha wawakilishi wao(vijana wasomi),ujumbe wa wizara na mwakilishi wa UNHCR.Nikirudi ofsini after a week ninaweza kukuhabarisha kama maamuzi yao hayatakuwa confidential!

Hivi Maagizo ya Waziri aliemaliza muda wake huweza kutenguliwa na Naibu Waziri Mpya? Nadhani hapa tunarudi katika siasa zetu uchwara (kama alivyosema mheshimiwa mmoja aliejiuzulu nafasi yake). Taratibu na kanuni za msingi za kutoa uraia zipo tena kwa mujibu wa sheria, na endapo suala litaonekana si la kawaida (kwa mfano kutoa uraia kwa watu 162,000 +++) mijadala ya wazi iwepo na kuwajumuisha wadau mbalimbali kabla ya kufikia hitimisho la kuutangazia Umma. Hili suala limekuwepo tokea 2007, leo ni 2012 na bado linapelekwa kwa wadau (what for?) ina maana ikikataliwa watu hao watanyang'anywa uraia ambao tayari wameshapewa? Ikikubalika uanzishwe tena mchakato wa kukusanya maoni ya wadau kwamba wasambazwe nchi nzima au la? Itakuwa mwaka gani?
 
Back
Top Bottom