Nauliza hivi,ni sawa kikatiba kwa naibu waziri kutanguliwa na ving'ora na pikipiki na watu kutakiwa kupisha barabara ili apite? Jana ijumaa 31.10.08 saa 9 mchana barabara ya morogoro karibu na fire magari yalitakiwa kukaa pembeni kwa ving'ora nikadhani anapita Raisi au waziri mkuu cha kushangaza akapita naibu waziri NW FU na msafara wa magari 6 watu wote wakashikwa na butwaa.Sasa kama viongozi wetu wote wa juu na sasa mawaziri na manaibu wao watapitishwa kwenye foleni kwa staili hii si itakua vurugu tupu?