structuralist
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,231
- 905
Wakati serikali ilipopeleka hoja (muswaada) bungeni kuhusu kuzuia fao la kujitoa wabunge wengi walikuwa wakali kupinga hoja hiyo.
Muasisi wa upingaji hoja alikuwa Mh Suleimani Jafo mbunge wa Kisarawe. Alitetea hoja yake na ukweli serikali nadhani ililegeza kamba kwenye hilo na watu wakafanikiwa kuendelea kupata withdraw benefits zao.
Leo hii serikali inaonekana kutaka kurejesha (kama bado haijafanya hivyo rasmi) utaratibu wa kuzuia fao hilo.
Kwa bahati nzuri aliyekuwa akilipinga wakati ule leo hii ni Naibu Waziri TAMISEMI mh Suleiman Jafo. Swali kwa Jafo ni kama kweli alikuwa na nia wakati ule ya kuwatetea watanzania je uko wapi msimamo wake leo hii?
Inawezekana jana alikuwa na msimamo lakini leo akageuka?
Kwa utaratibu wowote ule (najua unalinda pia kitumbua chako) ni ipi kauli yako na unafanya nini kupigania kile ulichokiamini kuwa hakikuwa sahihi toka mwaka jana?
Na kwa wale wabunge wengine walokuwawakipinga katazo lile ni nini kimetokea hatusikii tena wakiwa na misimamo ile?
Muasisi wa upingaji hoja alikuwa Mh Suleimani Jafo mbunge wa Kisarawe. Alitetea hoja yake na ukweli serikali nadhani ililegeza kamba kwenye hilo na watu wakafanikiwa kuendelea kupata withdraw benefits zao.
Leo hii serikali inaonekana kutaka kurejesha (kama bado haijafanya hivyo rasmi) utaratibu wa kuzuia fao hilo.
Kwa bahati nzuri aliyekuwa akilipinga wakati ule leo hii ni Naibu Waziri TAMISEMI mh Suleiman Jafo. Swali kwa Jafo ni kama kweli alikuwa na nia wakati ule ya kuwatetea watanzania je uko wapi msimamo wake leo hii?
Inawezekana jana alikuwa na msimamo lakini leo akageuka?
Kwa utaratibu wowote ule (najua unalinda pia kitumbua chako) ni ipi kauli yako na unafanya nini kupigania kile ulichokiamini kuwa hakikuwa sahihi toka mwaka jana?
Na kwa wale wabunge wengine walokuwawakipinga katazo lile ni nini kimetokea hatusikii tena wakiwa na misimamo ile?