Stanley.
JF-Expert Member
- Sep 6, 2011
- 660
- 298
Mh Naibu spika Ndugai hivi punde akijibu Muongozo ulioombwa na Mh Lukuvi kufuatia maoni ya kambi ya upinzani yanayosomwa mh mchungaji Msigwa ameitaka serikali kuwaonesha wapinzani kuwa wao sio dhaifu. Mh Lukuvi aliomba muongozo kufuatia mfululizo wa maneno serikali ya CCM dhaifu na shutuma dhidi ya mwenyekiti mmoja wa CCM wilaya kuwa ni jangili. Mh Ndugai kasema 'mimi sio sehemu ya serikali lakini nadhani serikali mngewaonesha kidogo kuwa nyie sio dhaifu'. Anaonekana ni kama anaimbia serikali itumie nguvu kwa upinzani..