Naibu Spika Ndugai apinga pendekezo la CAG

Bulesi

Platinum Member
May 14, 2008
14,210
13,723
Controller and Auditor General kwenye ripoti yake ya bunge amesisitiza umuhimu wa wabunge kutokuwa wajumbe wa mabodi ya mashirika ya umma kwani kwa kufanya hivyo kunawapunguzia dhamana ya kuyasimamia hayo mashirika kwa sababu ya conflict of interest!!

Jambo la kushangaza ni kuwa leo baada ya wenyeviti wa kamati za mahesabu kutoa hoja zao na kabla ya kuahilisha kikao huyu bwana akatoa angalizo kuwa kwavile hata hesabu za bunge ni lazima zipelekwe kwa kamati za bunge, haoni sababbu ya wabunge wasiwe wajumbe kwenye bodi za mashirika!!

What shallow thinking kutoka kwa naibu Spika kwani ni wazi haelewi concept nzima ya conflict of interest simply because kabla ya kupata huo wadhifa alionao alikuwa mjumbe wa bodi ya TANAPA kwa miaka kumi na kufaidi malupuplupu yaliyomfanya yeye na wenzie washindwe kuwathibiti watendaji na kusababisha nchi kukosa fedha nyingi za kigeni kutoka kwa watalii sababu ya maamuzi mabovu!!!

Naamini kuwa Zitto atasimama kidete kupinga upuuzi huu unaopunguza kasi ya maendeleo ya nchi kwasababu ya ubinafsi wa watu wachache.

Ni muhimu kwa bunge kuheshimu maelekezo ya CAG ili nchi iweze kuwa na utawala bora.
 
aaagh tumechoka na haya matapishi ya li CCm na watu wake....
 
Now I believe even more that the so called "common sense" is not common to everyone.

Because if this were true, then my class 6 child could be a Deputy Speaker bcoz I guess he can argue better that.
 
Nashawishika kuamini kwamba Naibu Spika ni mgeni sana ktk masuala ya Bunge.

Naibu Spika hakujipa nafasi ya kutosha kuelewa mantiki ya kutoshirikisha wabunge kwenye Bodi za mashirika yaliyo chini ya serikali. Maelezo ya ripoti yanajitosheleza kwa yeyote mwenye fikra sahihi. Mbunge ataiwajibisha vipi taasisi ya serikali iwapo yeye ni mmoja wa watoa uamuzi ktk taasisi hiyo??

Poleni sana CCM maana safari hii mlichagua wabunge vilaza haswaaa.

Labda kwa sababu mwenyekiti wa Kamati ni kutoka Upinzani?? Anasahau kwamba huo ulikuwa ni ushauri ulioridhiwa na Mabunge yaliyopita??
 
Sawa kijana mwenzetu Ndungai lakini kubwa zaidi tunapenda kusikia sauti yako ukikumbusha Bunge, Executive pamoja na Mbunge mmoja mmoja kwamba nyinyi nyote hapo ni waajiriwa wa Katiba hivyo kujitafutia kuhodhi shughuli za usimamizi na uendeshaji wa muswada wa kuanzisha Baraza la Taifa kuratibu mchakato mzima wa Katiba Mpya ni kule kujitafutia tu balaa na Umma wa Tanzania; Bara na Visiwani.

Never waste your precious time any further on sheer periferal issues that are daily going the wrong way under the watch of CCM government and ultimately settling on our misery at group and individuals; all the suitable answears would far easily be available and accessible with Katiba Mpya in place.
 
Inawezekana na yeye ni mmoja wa wale jamaa wanaofikiri kwa kutumia matumbo yao huku wakiacha bongo zao zipumpzike bila kufanya kazi stahili ya kufikiri critically! Lakini pia sio ajabu kwani leo hii wengi wao wako hivyo humo kwenye Chama chao!
 
Huyu bwana si kwamba anafanya makusudi bali haelewi. Kwetu sisi ile kamati ya bunge ikiwa inakagua taarifa au matumizi ya bunge wao ni km internal auditors au board of directors. Kwahiyo bado ni issue ya ndani. Yaani kukaa na kulinganisha kamati ya bunge kulikagua bunge na taasisi nyingine ni mapungufu makubwa sn. Angekuwa na busara km angeomba na wao wakaguliwe na muhimili mwingine. Kule bungeni tutasikia mengi saana.
 
Controller and Auditor General kwenye ripoti yake ya bunge amesisitiza umuhimu wa wabunge kutokuwa wajumbe wa mabodi ya mashirika ya umma kwani kwa kufanya hivyo kunawapunguzia dhamana ya kuyasimamia hayo mashirika kwa sababu ya conflict of interest!! Jambo la kushangaza ni kuwa leo baada ya wenyeviti wa kamati za mahesabu kutoa hoja zao na kabla ya kuahilisha kikao huyu bwana akatoa angalizo kuwa kwavile hata hesabu za bunge ni lazima zipelekwe kwa kamati za bunge, haoni sababbu ya wabunge wasiwe wajumbe kwenye bodi za mashirika!! What shallow thinking kutoka kwa naibu Spika kwani ni wazi haelewi concept nzima ya conflict of interest simply because kabla ya kupata huo wadhifa alionao alikuwa mjumbe wa bodi ya TANAPA kwa miaka kumi na kufaidi malupuplupu yaliyomfanya yeye na wenzie washindwe kuwathibiti watendaji na kusababisha nchi kukosa fedha nyingi za kigeni kutoka kwa watalii sababu ya maamuzi mabovu!!! Naamini kuwa Zitto atasimama kidete kupinga upuuzi huu unaopunguza kasi ya maendeleo ya nchi kwasababu ya ubinafsi wa watu wachache. Ni muhimu kwa bunge kuheshimu maelekezo ya CAG ili nchi iweze kuwa na utawala bora.
Hii kitu mbona ya zamani sana. Bila shaka itakua imetekelezwa maana ni jambo la msingi kabisa kuondoa wanasiasa na hasa wabunge kwenye bodi za mashirika ya umma. Wengi hawaelewi wajibu wao wanajua ni ulaji tu. Ukizungumzia conflict of interest wanaona ni kuwanyima ulaji kitu ambacho ndio lengo lao kwenye uongozi.
 
Back
Top Bottom