TaiJike
JF-Expert Member
- Dec 14, 2011
- 1,483
- 666
Nyumba ninayoishi ni apartment ya family mbili, nimeishi nyumba hiyo kwa muda mrefu sasa. Mwezi wa kumi 2011 alihamia mpangaji mwenzangu ktk sehemu iliyokuwa imeachwa wazi na mtu ambaye alihama. Jirani huyu ni mwanaume na anaishi hapa bila mke ingawa mke anaye anadai mkewe huyo yuko mbali naye kwa sababu za kifamilia naye hapa yupo kikazi tu.
Toka alivyohamia hapa ninapoishi naye kama jirani kesha badili wasichana wa kazi za ndani wanne aliepo sasa ni wa tano. Msichana wa pili kabla hajaondoka alinifata na kunilalamikia tabia chafu za mbaba huyu za kumlazimsha amtimizie haja zake za zinaa, nikamshauri aondoke akatafute kazi sehemu nyingine. Jana msichana wa tano mwenye umri wa miaka 17 akiwa ana siku mbili tu alinifata na kunitolea malalamiko kama Dada na mwanamke mwenzie, kuwa mbaba yule anamlazimisha mapenzi kwa kumtisha na Bastola. Nilichomshauri binti huyo ni kwamba tutaweka mtego wa kumuadhirisha ili kuikomesha tabia yake chafu ya kuchezea watoto wadogo. Sasa ndugu zangu hapa ndipo ninapoomba msaada wa ushauri wenu nitumie polisi, majirani, ama mapaparazi?
Toka alivyohamia hapa ninapoishi naye kama jirani kesha badili wasichana wa kazi za ndani wanne aliepo sasa ni wa tano. Msichana wa pili kabla hajaondoka alinifata na kunilalamikia tabia chafu za mbaba huyu za kumlazimsha amtimizie haja zake za zinaa, nikamshauri aondoke akatafute kazi sehemu nyingine. Jana msichana wa tano mwenye umri wa miaka 17 akiwa ana siku mbili tu alinifata na kunitolea malalamiko kama Dada na mwanamke mwenzie, kuwa mbaba yule anamlazimisha mapenzi kwa kumtisha na Bastola. Nilichomshauri binti huyo ni kwamba tutaweka mtego wa kumuadhirisha ili kuikomesha tabia yake chafu ya kuchezea watoto wadogo. Sasa ndugu zangu hapa ndipo ninapoomba msaada wa ushauri wenu nitumie polisi, majirani, ama mapaparazi?