Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Dada huyu anaitwa Amina(siyo jina halisi) aliolewa miaka 2 iliyopita,mumewe bwana Rajabu(siyo jina halisi)ni mfanyakazi kwenye kampuni moja ya uchimbaji wa madini.Tatizo ni hili:Amina na mumewe mwanzoni mwa ndoa yao ilikua njema sana kabla ya mumewe bwana Rajabu kupata jimama lililosababisha Rajabu kuisahau kabisa familia yake.Rajabu alianza vituko wakati mkewe ana ujauzito wa miezi 7,alikua akimpiga,hela ya matumizi akawa anatoa kidogo na wakati mwingine hatoi.Amina ikabidi amwite mama yake kutoka Tabora,nae mama hakusita,akaja lakini akashindwa kumweka sawa mkwe,yaani ndo akawa halali nyumbani.Akawa anarudi asubuhi kubadili nguo na kuondoka.Hali ikawa mbaya nyumbani,ndugu zake mume wa Amina walijaribu kumweka sawa ndugu yao bila mafanikio ndipo mdogo wake wa kiume mumewe Amina akawa anamhudumia shemejie kwa matumizi,wala mumewe Amina hakujali.Hata alipopelekwa kujifungua hostl ya Bugando,mumewe hakwenda,na alijifungua kwa upasuaji na bahati mbaya mtoto alifariki.Shemejie Amina ndo aligharamia kila kitu na alipotoka kodi ya nyumba aliyokua anaishi iliisha na shemejie alilipa.Mama wa Amina alishuhudia yote haya.Mumewe Amina alianza kumtuhumu mkewe kujihusisha kimapenzi na shemejie,eti kama hawana uhusiano mdogo wake asingemhudumia namna ile,jambo hilo lilisababisha mpaka mumewe Amina kukorofishana na mdogo wake,ilipofikia hapo Amina alitengana na mumewe na kwa msaada wa shemeji yake alipata kazi kiwanda cha bia Serengeti(Mwanza)Sasa imepita miezi 5,mumewe Amina anataka warudiane,Amina anadai hana hisia kabisa na mumewe.Yeye Amina kwa muda sasa amekua na hisia zaidi kwa mdogo wake mumewe,amejizuia lakini kila akikumbuka shemeji yake alivyokua anamjali na kuhangaika anazidi kutamani kuwa karibu nae,huwa wanawasiliana na wakati mwingine shemejie Amina humtembelea anakoishi Amina na Amina hajawahi kumwambia shemeji yake anavyojisikia.Amina hajui afanye nini,hataki hata kumuona mumewe na hisia juu ya shemejie zinamsumbua.Hebu funguka,afanyeje?Mumewe huwa mpaka analia kumsihi warudiane,lakini mkewe hataki,kumbuka shemejie Amina hajaoa,je inawezekana Amina na shemejie wakaoana?Nataka mtazamo wako,mimi wangu ninao,hebu nione wako!