Nahitaji mwanamke wa kumlipa anizalie mtoto kwa mkataba.

Utoto unakusumbua. Wewe ni mwanafunzi, soma umalize shule kwanza.Mzazi haji kuishi na wewe kwa maisha yako au kukutunzia familia yako baadaye.Unaoa ili uwe na familia yako mwenyewe.Epuka watoto wanaolelewa na wazazi ambao hawaishi pamoja,usijifikirie nafsi yako au kufanya jambo fulani ili kumfurahisha mzazi wako bila kufikiria upweke atakaokuja kuishi mwanao bila mama mzazi baada ya wewe kuoa mwanamke mwingine na kuachana na huyo wa mwanzo,Nafikiri unawaona watoto wa mtaani wengi wao utakuta wamekimbia nyumbani kutokana na manyanyaso ya kina mama wa Kambo na wengine wametoka kwenye familia bora tu.Kwa mtizamo wangu nakuona wewe hufai katika jamii,wewe ni mtu mbinafsi na ni kati ya wanaotaka kuchangia ongezeko la watoto wa mitaani.

ni mawazo yako na ninashukuru kwa mda wako
1."utuuzima sio pale tunapoanza kuongea vitu vikubwa ila ni pale tunapoanza kuelewa mambo madogo"
2.kuhusu kusoma ninajitambua
3.kuhusu mtoto kuwa wa mtaani hicho kitu hakipo coz mtoto m1 hanishind kumhudumia
anyway,naheshim mawazo yako
 
hapo kwenye red kuweni makini huu ni utoto uliopitiliza msipoteze nguvu wakuu

hujui kutoa mawazo angalia ukiitwa kwenye press conf ujibu hoja za watu utashindwa

hoja haijibiwi kwa kejeli hoja inajibiwa na hoja

utoto!?eleza kvp
ok,ni sawa labda ndo uwezo wako wa kufikiri
huwa nakubali challenges
 
hujui kutoa mawazo angalia ukiitwa kwenye press conf ujibu hoja za watu utashindwa

hoja haijibiwi kwa kejeli hoja inajibiwa na hoja

utoto!?eleza kvp
ok,ni sawa labda ndo uwezo wako wa kufikiri
huwa nakubali challenges
naomba unieleze maana halisi ya neno kejeli maana hata MAMODS wa JF hawajui kutofautisha kejeli na ukweli
 
pimeni kwanza akili sio kutiririka tu wakuu

toa hoja kupinga hoja
eleza ni kwa jinsi gani hoja niyoiandika haina mashiko,sio unakurupuka
kweli walimu wanakaz kufundisha watu kama nyie
labda nimekosea spelling lakini those ar human errors
tumia muda vizur
 
Poor you!!!! Huyo mama yako anaumwa ugonjwa ambao doctor amemhakikishia hatashi miaka michache ijayo au ni kitu gani? Kama ni mzazi na anataka usome na ufaulu upate maisha basi akuache umalize shule ndipo uoe kabisa. Kwa nini azalwe mtoto aishi na mzazi mmoja na msipooa basi aishi na mama wa kambo? Kwa hakika kwa tunavyoona si vema kabisa mtoto kuishi na mama au baba wa kambo, inasumbua sana kimalezi na saikolojia ya mtoto. Pinga hiyo na mueleweshe mama yako.
 
this is beyond my wildest imaginations, sikutegemea kama kuna watu wana mawaza ya hivi, yani we unashindwa kumpa mimba demu wako kijanja, yani wewe ni MTOTO WA MAMA nambari moja
 
Endelea kutafuta utampata...si kuna binti msanii anatoa hiyo huduma ya kuzalia watu watoto.

Mtafute aisee anaweza kukusaidia.
 
ni mawazo yako na ninashukuru kwa mda wako
1."utuuzima sio pale tunapoanza kuongea vitu vikubwa ila ni pale tunapoanza kuelewa mambo madogo"
2.kuhusu kusoma ninajitambua
3.kuhusu mtoto kuwa wa mtaani hicho kitu hakipo coz mtoto m1 hanishind kumhudumia
anyway,naheshim mawazo yako

Tatizo sio kushindwa kumlea.Je huyo mwanamke utakayekuja kufunga naye ndoa atakuja kuwa tayari kumjali na kumtunza huyo mtoto kama mwanaye wa kumzaa.Maana tuna mifano hai ya baadhi ya watoto wanaolelewa na baadhi ya Mama wa Kambo wanavyowanyayasa hao watoto.
 
naomba unieleze maana halisi ya neno kejeli maana hata MAMODS wa JF hawajui kutofautisha kejeli na ukweli

unaona ni jinsi gan unashindwa kupambanua mambo
katika kanuni za kuuliza na kupinga hoja ya mtu huwa hatumuulizi mtu maana ya neno mojamoja unachukua maana ya text nzima na kuijengea hoja yakupinga kile kilichoandikwa coz kila neno linamaana tofauti katika kila sentensi
duh,nimegeuka mwalim
 
hapo ndg umeanza kutoka nje ya maadili ya kawaida kabisa!!! hivi unajua kuwa mtoto akizaliwa ana haki ya kupata upendo na malezi toka kwa Baba na Mama hadi akijakuwa mtu mzima, asomeshwe na ahudumiwe nanyi kwa pamoja? ukifanya hivyo unavyotaka kufanya ni kuwadhalilisha wanawake, huku ni kuwafanya wanawake kama "chombo" cha wewe kutimizia malengo yako na hitaji la mama yako. Namwonea huruma mwanamke yule atakayekuwa tayari kudhalilishwa eti kwa kigezo cha kulipwa!!!! kumtii mama si maana yake "kukubaliana naye kila kitu". Kumbuka wewe unajukumu kubwa la kujenga maisha yako na heshima yako mbele ya jamii kwa kuonesha kuwa huendeshwi kwa matakwa ya mzazi hususani katika jambo kubwa kama hili. Usijiingize kwenye tatizo la kumleta duniani mtoto atakayekosa "upendo wa baba na mama". Na kwa yule binti au mwanamke atakayekubaliana na "dili" hili narudia tena atakuwa anajidhalilisha kwani atakuwa amejifanya kuwa chombo au kitega uchumi. ama kweli duniani kuna mambo, sijajua ni dini gani hasa inaruhusu hizi ndoa za mikataba? au ni kwa utamaduni wa kabila gani hapa TZ, mambo haya yanapokeleka. Tuache mtindo wa "copy and paste" wa tamaduni za wenzetu huko Ulaya. Yawezekana nikaonekana mshamba lakini kwa vile hapa tunaelimishana na kushauriana, basi nashauri kuwa jenga staha yako mbele ya mama yako kwa kumweleza kuwa yule unayetarajia aje kuwa mtoto wako ana haki ya kuja kufurahia malezi na upendo wa Baba na Mama, na hivyo akusubiri hadi pale utakapofikia hatua ya kupata mtoto kwa ustaarabu murua wa kijamii na kwa imani yako. Kama ni kufa mama, usihofu hilo litakuja kutokea tu siku moja na kama ni mapenzi yake Mola inawezekana ukafa hata kabla mpango huo anaoutaka mama hujautekeleza. Tusipotoshe maadili kwa visingizio kama hivi. Naomba kuwasilisha.
 
kama umesoma maelezo vizur nimeandika
1.nitaihudumia hiyo mimba mpaka wakati nitakapo mchukua mtoto baada ya kumaliza kunyonya
2.mwanamke nitamhudumia mahitaj yanayoendana na ujauzito wangu
3.kuhusu uwepo wangu inategemea huyo mwanamke atakua mkoa gan coz mda mrefu nipo chuo na field

Source ya kipato chako ni wapi maana kwa umri wako wa miaka 23 kwa mazingira ya Tanzania jeuri ya mpaka kumtafuta mwanamke akuzalie umpe hela maana yake una hela nyingi na kama unazo uhakika wa fedha zako ukoje maana mimba isije ikafika miezi 6 ela baba imekata ghafla au akaunt yako imefungwa kwa kuwa ndugu wameenda kufungua kesi labda ni ela za urithi hivyo hawajaridhika na mgawanyo alafu mwanadada anabaki hoi, unless kama unalipa advance kwanza ambayo itaonyesha upo serious
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom