BADILI TABIA
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 32,772
- 23,160
asipogsikiliza ushauri huu basi tena....huyo jamaa anakutumia tu. Hana mapenzi na wewe. Tayari ameshakwambia ana mchumba/mkewe. Hiyo ni alama tosha move on with your life. Kukwambia uwe 2nd wife/nyumba ndogo ina maana jikubalishe uwe Door mat! Yaani wewe ni utatumika iwapo nyumba kubwa kutakuwa kuna kasoro mbili tatu, zaidi ya hivyo, utabakia unahesabu boriti usiku kucha. Ni mapenzi gani hayo ya muda maalumu? Yaani kati ka kumi jioni na nne usikju tu ndio atakuwa na muda na wewe? huhitaji kuwa na wako wa maisha? Mbaya kuliko yote, huyo jamaa hakupi pumzi wala muda wa kutafakari nini unataka maishani. Kwanini unampa nafasi akupigie kila wakati, aje kwako wakati wowote, halafu mwisho wa yote anapoondoka ndipo nawe reality ina kick in kwamba unachezewa shere? Weye sio msukule bana, hebu badilika! Watuchukia waume bure ilhali maamuzi ya kuchezewa maisha umejikubalisha mwenyewe.