Nafikiri Biblia na Qur'an ni project zilizofanywa na wanadamu - Prove me wrong!

Sidhani kama wasomaji wa Biblia wanatafuta ushahidi wa maandiko katika mambo ya dunia. La hasha! Wasomaji wazuri wa Biblia yaani waaminio, wanaiamini Biblia kuwa ni neno la Mungu kwa ushuhuda ulio ndani yao. Tunaleta vilinganishi hivi kwa sababu baadhi yenu mnapinga matukio katika biblia yanayokubaliana na sayansi ama historia ya mwanadamu. Hatuhitaji kuiamini Biblia kwa kusaka matukio duniani yanayoithibitisha ama la. Tunaliamini neno na kulishika basi. Na hapo tunaokoka na kukutana na Yesu mwokozi wa Ulimwengu. Basi. Mambo ya Anga, nyota, sayari Ayubu aliyasema zamani kabla ya hata Galilio Galilieo. Dunia kuwa duara yalisemwa zamani na Biblia. Mikataba ya ushirikiano imefanyika zamani sana katika Biblia. Upembuzi yakinifu umefanyika zamani sana hata enzi za Yusufu Misri. Utawala Bora ulitumika tangu ziku za Sulemani Mfalme. Sema hata Diplomasia ya Kimataifa. Matumizi ya askari wachache katika vita maalum ilitumika na kina Gideon kabla ya Jeshi la Israel kuiasili mbinu hii na kuitumia Uganda na Lebanon. Gideon aliwarejesha nyumbani wanajeshi wa Israeli zaidi ya 22,000 na kubaki na 300 tu na wakashinda vita. Usikipungukie kile ambacho Biblia imekiandika. Ikiwa hukiamini basi ni vizuri kuwaacha wanaokiamini na kukifanyia kazi waendelee maana hutaweza kukizima.

Good. Bora umesema kuwa mfuasi wa Biblia lazima awe closed mind. Ukisema utafute ushahidi na logics hutaelewa.

So, tutaipimaje KWELI katika maandiko? How can we identify the right book kama tunaishi kwa kuambiwa tuamini tu bila kutafuta shahidi za kidunia?
 
Good. Bora umesema kuwa mfuasi wa Biblia lazima awe closed mind. Ukisema utafute ushahidi na logics hutaelewa.

So, tutaipimaje KWELI katika maandiko? How can we identify the right book kama tunaishi kwa kuambiwa tuamini tu bila kutafuta shahidi za kidunia?
Now THAT IS A POINT OF DISCUSSION.

Its what this thread is all about
 
Leta mistari ya bible inayozungumzia mifumo ya jua, uduara wa dunia

Cha ajabu, leo hii watajifanya wanaleta mstari lakini wao wao ndio walifungia Galileo na kuunda council, wakamtishia adhabu ya kifo kwa kumwambia akane kauli kuwa jua sio centre ya Galaxy na dunia si duara.

Kipindi cha Renaissance iliaminika dunia ndio centre of the universe kwa sababu ndio makao makuu ya uumbaji wa mwanadamu na hawakusema ilikuwa duara.

Waliua wanasayansi waliosema before Galileo na Galileo alipokuja na ugunduzu wa Telescope wakamkanisha kauli na kumfungia exile mpaka mauti ilipomfika. Leo hii nyumba yake ya exile imekuwa chuo na museum.
 
My point is here,

"So, tutaipimaje KWELI katika maandiko? How can we identify the right book kama tunaishi kwa kuambiwa tuamini tu bila kutafuta shahidi za kidunia?"
 
My point is here,

"So, tutaipimaje KWELI katika maandiko? How can we identify the right book kama tunaishi kwa kuambiwa tuamini tu bila kutafuta shahidi za kidunia?"

kibaya zaidi theologist wanakwambia usichukulie maandiko ya biblia kama yalivyo, yani neno lilivyoandikwa usilichukulie kama lilivyo, kwa namna hii maanake ni kwamba biblia imeandikwa kimafumbo, na yale matukio yaliyotokea sio ukweli ila kuna maana ndani yake. tatizo la kuandikwa biblia kimafumbo ni kwamba mwisho wa siku kila mtu anakua na tafakari yake, one can be right and one can be wrong.. sasa mtu akisema bible is a confusious book utambishia? hatari sana.
 
Good. Bora umesema kuwa mfuasi wa Biblia lazima awe closed mind. Ukisema utafute ushahidi na logics hutaelewa.

So, tutaipimaje KWELI katika maandiko? How can we identify the right book kama tunaishi kwa kuambiwa tuamini tu bila kutafuta shahidi za kidunia?

Umesema vizuri! Wale wanaotaka kuthibitisha yaliyomo katika Biblia pasipo kuyaamini tu wanao uhuru wa kutafuta vielelezo vya Kihistoria ama vinginevyo. Thomaso alisema nisipomshika ubavu wake sitaamini. Kweli akamshika akaona yake makovu ya Yesu ndipo alipoaamini. Yesu aksema heri waliosadiki kabla ya kuona. Soma Yohana 20:

24Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. * 25Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. *

26Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu. * 27Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye. 28Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! * 29Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. *


Bora kuamini. Na kuamini ni busara zaidi na wala si "closed mind."
 
Umesema vizuri! Wale wanaotaka kuthibitisha yaliyomo katika Biblia pasipo kuyaamini tu wanao uhuru wa kutafuta vielelezo vya Kihistoria ama vinginevyo. Thomaso alisema nisipomshika ubavu wake sitaamini. Kweli akamshika akaona yake makovu ya Yesu ndipo alipoaamini. Yesu aksema heri waliosadiki kabla ya kuona. Soma Yohana 20:

24Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. * 25Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. *

26Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu. * 27Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye. 28Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! * 29Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. *


Bora kuamini. Na kuamini ni busara zaidi na wala si "closed mind."

Okay.

But hujanijibu.

Kuna maandiko mengi duniani. Tutajuaje andiko la kweli?
 
We umewezaje kujua kuwa kuna mungu na ndiyo aliyekuumba?
Nikakujibu kwambaaa, kwa kujiangalia mimi jinsi nilivyo, mikono, miguu, ubongo, utumbo na hata uwezo wa kuongea, kufikiria.. Vyote ivyo hakuna binadamu wa kufanana na mimi anayeweza kuvifanya.

Which means kuna mtu au kitu kilichoratibu kutengenezwa kwangu.

Kwangu huyo/hicho kitu ndio MUNGU.

So naamini kuna Mungu kupitia mimi mwenyewe.
 
Nikakujibu kwambaaa, kwa kujiangalia mimi jinsi nilivyo, mikono, miguu, ubongo, utumbo na hata uwezo wa kuongea, kufikiria.. Vyote ivyo hakuna binadamu wa kufanana na mimi anayeweza kuvifanya.

Which means kuna mtu au kitu kilichoratibu kutengenezwa kwangu.

Kwangu huyo/hicho kitu ndio MUNGU.

So naamini kuna Mungu kupitia mimi mwenyewe.
Mimi naamini kwamba dini ndiyo zilizoleta habari ya kwamba kuna mungu na ndiye muumbaji,na ndiyo maana nikakuuliza wewe huo utambuzi wako kwamba kuna mungu umeupataje?
 
Mimi naamini kwamba dini ndiyo zilizoleta habari ya kwamba kuna mungu na ndiye muumbaji,na ndiyo maana nikakuuliza wewe huo utambuzi wako kwamba kuna mungu umeupataje?
Aisee samahani lakini ingawa nimegundua ninafanya converstation na mtu ambae ni mgumu sana kuelewa.

Soma jibu langu lina majibu yote YA KWANINI NAAMINI KUNA MUNGU.

Katika majibu hayo sijahusisha maandiko hata sehemu moja.

My regards
 
Back
Top Bottom