Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,510
- 28,416
Mahakama kama moja ya mihimili mitatu ya serikali ina nafasi sawa kikatiba kama ilivyo BUNGE na UTAWALA(EXECUTIVE). lakini hili halidhihiriki kama linavyotakiwa katika nchi yetu.Kitendo cha mahakama kuwa chini ya wizara ya sheria na katiba ni kuifanya iwe chini ya mhimili mwingine wa serikali ambao unasimamiwa na waziri mkuu na mawaziri wake.. Hoja yangu hapa si kupunguza uingiliaji wa rais katika uteuzi wa majaji ila ni kuiondoa mahakama chini ya wizara na kiufanya iwe huyu kama lilivyo bunge
Bunge la jamhuri hii haliko chini ya wizara yoyote na wala hakuna waziri(na hata waziri mkuu) aliye na dhamana ya kuangalia uendeshaji wake wa siku kwa siku sasa iweje kwa mahakama iwe chini ya kiongozi wa kisiasa ambaye anatoka katika mhimili mwingine wa utawala
Juzi juzi nilimsikia waziri wa sheria akiipa mahakama maagizo ya kuharakisha kesi za mahabusu ili kuwapa watu haki zao hasa wale ambao wanasota na vijikesi vyao havieleweki eleweki ,japo jambo hili si baya lakini kama waziri mbaye yuko chini ya waziri mkuu anaweza kutoa maagizo haya kwa mhimili mwingine inaonekana hata waziri mkuu wa nchi hii yuko juu ya mahakama japo katiba hailitamki hili wazi wazi
MY OPINOIN
moja ya mambo ya msingi ambayo wanasheria wa nchi hii wanabidi wayatolee maoni katika katiba mpya ni hli la kuiondoa mahakama chini ya wizara na kiwe chombo huru chenye government struture yake na jaji mkuu inabidi ndio awe TOP kama alivyo SPIKA katika bunge japo rais anweza kuendelea kuwa na mamlaka kama aliyo nayo
Mimi si mwanasheria ila nadhani wanasheria wanaweza kulitolea hili ufafanuzi mzuri wa kina
naomba kuwasilisha
Bunge la jamhuri hii haliko chini ya wizara yoyote na wala hakuna waziri(na hata waziri mkuu) aliye na dhamana ya kuangalia uendeshaji wake wa siku kwa siku sasa iweje kwa mahakama iwe chini ya kiongozi wa kisiasa ambaye anatoka katika mhimili mwingine wa utawala
Juzi juzi nilimsikia waziri wa sheria akiipa mahakama maagizo ya kuharakisha kesi za mahabusu ili kuwapa watu haki zao hasa wale ambao wanasota na vijikesi vyao havieleweki eleweki ,japo jambo hili si baya lakini kama waziri mbaye yuko chini ya waziri mkuu anaweza kutoa maagizo haya kwa mhimili mwingine inaonekana hata waziri mkuu wa nchi hii yuko juu ya mahakama japo katiba hailitamki hili wazi wazi
MY OPINOIN
moja ya mambo ya msingi ambayo wanasheria wa nchi hii wanabidi wayatolee maoni katika katiba mpya ni hli la kuiondoa mahakama chini ya wizara na kiwe chombo huru chenye government struture yake na jaji mkuu inabidi ndio awe TOP kama alivyo SPIKA katika bunge japo rais anweza kuendelea kuwa na mamlaka kama aliyo nayo
Mimi si mwanasheria ila nadhani wanasheria wanaweza kulitolea hili ufafanuzi mzuri wa kina
naomba kuwasilisha