nadhani sasa nifanye maamuzi mepesi!!!!

msani

JF-Expert Member
Jun 13, 2011
1,801
1,191
kuna siku nilikuja na thread yenye kickwa hiki nisaidieni-nifanyeje-kuhusu-gf-wangu
kwa ufupi nilikuwa napewa taarifa na mdogo yake ambaye ni rafiki yangu sana kuwa dada yake sio mwaminifu kwangu na hata kudhani huenda ananitaka lkn inawezekana pia.
Sasa kilichonifanya kurudisha humu mmu hili suala ni kuwa wiki iliyopita alinipigia kuwa anaenda moro kumuona mgonjwa na ameagizwa huko na mama,alifika moro saa 4 usiku na wkt nawasiliana nae akaniambia kuwa amepigiwa simu kuwa ameambiwa mgonjwa kahamishiwa mkoa huu niliopo kwa hiyo ikabidi aunganishe safari na kwa kuwa kutoka hapa mjini mpaka alipotakiwa kwenda ni mbali aliniomba nimtafutie chumba cha kulala na sio nyumbani kwangu ambapo kwa sababu alizotoa nilizikubali,nikamtafutia na asbh nikamsindikiza akaenda alipotakiwa kwenda na kuahidiana kuwa siku hiyo angekuja nyumbani kulala kwani kesho yake ilikuwa arudi.Mchana yake tuwasiliana nae na kuniambia saa 12 atakuja lakini hakuja na simu zote zilikuwa haziptikani na nishindwa kujua km aliondoka kuja na njiani akapata mkasa au hakuondoka kabisa siku hiyo ikapita nikiwa na mawazo sana,siku iliyokuwa ya safari nikawasiliana na mdogo wake naye akasema hampati na hajui kwa nini ila kuna namba moja ya alikuwa anaitumia yenyewe ilikuwa hewani lkn haipokelewi.
nikamtafuta siku hiyo mpaka saa 5 ucku namba ikiwa haipokelewi na hatimaye ikapokelewa na dada yake mkubwa na kuniambia kuwa gf wangu aliiacha ile line wakati anasafiri na huyo dada ndo alikuwa anaitumia,kesho yake asbh akanipigia kwahiyohiyo namba na kuniambia kuwa dada yake amemwambia kuwa nimepiga sana kwenye hiyo namba na kuniambia kuwa yaliyojiri kuwa aliibiwa simu zote 2 alipokuwa ameenda mjini na aliporudi alikuta tiketi tayari imekatwa akashindwa kuaga kuja huku,.
siku ile nilipoona mambo yamekuwa magumu niliamua kumshirikisha bianmu yake ambaye tuko naye hapa karibu na kumueleza mkasa mzima kwani safari hiyo ilikuwa siri kwetu wawili na nikahisi kama aliondoka na akapata tatizo njiani na mie ndo nilikuwa najua anakuja kwangu je ndg zake wakijua kuwa mie nilikuwa najua si itakuwa msala ikabidi niseme.sasa jana wkt tumekana na huyo binamu tukaanza kuongelea hilo sula ila akaniambia kuwa yule dada lkn hajatulia na hapo alikuwepo mtoto wa baba yake mkubwa akadakia hivi huyu binti pamoja na kuwa na mtoto bado anatamani kurukaruka?!Dah nilisikia km nimewekewa kaa la moto moyoni ndipo nilipoulizia na kuambiwa kuwa ana mtoto mmoja na alizaa akiwa f2 lkn mie nilikuwa nafichwa sku zote jamani na leo tumeongea nae lkn sijamwambia kuhusiana na hilo ila ndo nafikia maamuzi mepesi jamani maana kesho 19/11/11 nadhani nitakuwa single kwani nimechoka maana nimedanganywa siku nyingi sana ila kwa kuwa nilikuwa nampenda niliamini ktk mabadiliko.
hata hawa ndg zake kwa ni marafiki zangu sana wamenishauri nitafute mtu wakuwa naye na sio huyo kwani haendani na mie na ukizingatia sasa nakimbilia 30 yrs na ninahitaji kuwa na mtu ambaye anamwelekeo wa kuwa mke!!!!!!!!!
nimechoka ila nashukuruni kwa ushauri wenu hapo awali
 
watakao jibu hii thread naomba msiiquote kwa sababu ni ndefu sana.ukiiquote ntajua wewe ni masaburi.
Mukuu huyo hafai kuwa mke.ana uongo wa maudhi kama unakaa nae nyumba moja unaweza kuua.mia
 
Duh move on mkuu
Haya mambo ya mapenzi yanahitaji uaminifu sana na kama unamtafuta mke sio jambo la kuchagua kama unachagua nyanya sokoni
tafuta mtu ambaye kweli anafaa kuwa mke
Kama ana mtoto muda mrefu hivyo hata kukupa taarifa hajawahi au kugusia ni mangapi mengine anakuficha
Hata hilo la kuibiwa simu inawezekana anakudanganya tuu may be alikuwa kwa jamaa yake akaona haina haja
 
pole sana kaka yangu
ni maamuzi mazuri koz hujui kilikomfanya azime 4n zote mbili nn nn zaidi na kama huyo dda yake mkubwa alikua na cm kwann asipokee na kilikomfanya asipikee mchana kutw ana kuja kupokea ucku ni nn wakati ni namba hiyo hiyo ilikua inatoa call loh! zinduka kaka yangu
amua kumuliza mwizi au piga chini na chapa lapa ndefuuuuuuuuuuuuu
 
Daaah!Pole sana mkuu,haya mambo yanahitaji sana hekima ya kutosha ndugu yangu!Kuwa mvumilivu!
 
acha ujinga wewe! Sasa hivi hakuna mapenzi we uwe unakula halafu unasepa huo ndio mpango mzima! Ukijifanya kupenda utaumia hio ndio kanuni!
 
watakao jibu hii thread naomba msiiquote kwa sababu ni ndefu sana.ukiiquote ntajua wewe ni masaburi.
Mukuu huyo hafai kuwa mke.ana uongo wa maudhi kama unakaa nae nyumba moja unaweza kuua.mia
nami niliwaza km watu wakii-quote mbona itakuwa kero ila sikuwa na jinsi,asante kwa ushauri ila atakayei-quote sio masaburi huenda hajasoma comment yako
 
Daaah!Pole sana mkuu,haya mambo yanahitaji sana hekima ya kutosha ndugu yangu!Kuwa mvumilivu!
yaani mpaka nimefikia hii hatua nimevumilia sana na hata ndg zake walikuwa wananishangaa kwa jinsi nilivyokuwa na huyo ndg yako nikiamini atabadilika...kumbe kunguru hafug.......i
 
acha ujinga wewe! Sasa hivi hakuna mapenzi we uwe unakula halafu unasepa huo ndio mpango mzima! Ukijifanya kupenda utaumia hio ndio kanuni!
sio ujinga mkuu ila sikutaka kukimbikimbia huku na kule nikiamini yeye ananifaa na hata nitakayempata nitampenda pia huenda akapendeka maana wote hawafanani.
usile na kusepa,weka ndani kabisa au umri wako bado unaruhusu hako kamchezo nini?
 
Dalili ya mvua ni MANYUNYU!
hii yangu kweli imeanzia kwenye manyunyu badala ya mawingu,huenda nilikuwa ndani ndo maana sikuona mawingu ila imenyesha mpaka imekatika sasa naweza toka nje na kuendelea na safari.thanks
 
mchukue mdogo mtu maisha yaendelee..
hapo nitakuwa nimeharibu mkuu kwani kwa muda wote ambao nimekuwa naye hata familia yao ilikuwa ni rafiki kwangu sana hata sasa nitaachana naye lkn watabaki kuwa marafiki kwangu ila nikichukua mzigo tu nitakuwa nimesababisha soo
 
pole sana kaka yangu
ni maamuzi mazuri koz hujui kilikomfanya azime 4n zote mbili nn nn zaidi na kama huyo dda yake mkubwa alikua na cm kwann asipokee na kilikomfanya asipikee mchana kutw ana kuja kupokea ucku ni nn wakati ni namba hiyo hiyo ilikua inatoa call loh! zinduka kaka yangu
amua kumuliza mwizi au piga chini na chapa lapa ndefuuuuuuuuuuuuu
asante AMINATA,ila hapo ndo nilikuwa nachanganyikiwa zaidi lakini nimetulia na sasa naona shughuli zangu zinaenda safi
 
Pole woiyeee,njoo kwangu nikupooze
je wewe ni me au ke ngoja mwenye mali aje ikifika kesho hajatoa comment hapo halfu ukiwa ni ke nitafikilia ofa yako ila km ni me utanitaka radhi hapa,asante
 
Back
Top Bottom