Naangamia mwenzenu nisaidieni pls!

Pole mwanangu.
Ninakushauri uandike barua kwa ufupi tu ya kuomba kazi. Tengeneza CV yako safi kabisa na usisahau kuweka referees wakuaminika watatu. Ambatanisha na vyeti vyako (IV, VI na chuo). Jitahidi upate address za mabenki yafuatayo: CRDB, NMB, NBC, AKIBA COMMERCIAL BANK, STANBIC, STANDARD CHARTERED BANK, EXIM.
Hakikisha unapeleka barua, CV na vyeti kwa mabenki yote haya. Kisha potezea kabisa na uendelee na shughuli nyingine. Utashitukia unaitwa kwenye Interview hata kama ni baada ya mwaka mmoja. Hakikisha unaweka contacts zako ambazo hazina utata haswa simu. Mara nyingi hawatumi barua, bali wanakupigia simu ya mkononi. Hizi Bank hawatangazi nafasi za kazi hata siku moja. Wanaita wale walioomba ambao tayari wana docs zao nilizotaja hapo juu.
Binti zangu wawili wamepata kazi CRDB kwa mtindo huu. Infact CRDB walikuwa na Interview ya watu almost 300 wiki mbili zilizopita na wameajiriwa wengi tu bila upendeleo hata chembe, including mabinti zangu. Nasikia Interview nyingine itakuwa mwezi wa saba. Nakutakia kila la heri na Mungu akutangulie mwanangu.

Mabenki na taasisi nyingi za fedha na za kimataifa huwa hawaajiri direct..wanatumia recruiting agencies..cha msingi ni yeye kuweza kutuma CV yake kwa agency mbali mbali kama Erolink, Proffesional Approach etc..hilo ndio litakalo mtoa kutoka kijiweni..otherwise itaendelea kula kwake.
 
Mabenki na taasisi nyingi za fedha na za kimataifa huwa hawaajiri direct..wanatumia recruiting agencies..cha msingi ni yeye kuweza kutuma CV yake kwa agency mbali mbali kama Erolink, Proffesional Approach etc..hilo ndio litakalo mtoa kutoka kijiweni..otherwise itaendelea kula kwake.


Hizo recruiting agencies nyingine ni utapeli mtupu. Wengi ya waliofanya CRDB walipeleka Interview zao Direct na wote waliitwa kwenye Interview. Ninamshauri kitu ambacho nina uhakika nacho. Hawa mabinti zangu waliitwa kufanya Interview kwenye several bank, lakini walichagua kufa na CRDB na kuacha kwenda kule kwingine. Hawakutumia recruiting agencies yoyote zaidi ya kumuomba Mungu. Wewe kijana peleka CV zako na utulie usubiri kuitwa. Mradi uwe na subira na usiwe na haraka. Achana na hao matapeli wanaojiita recruiting agencies. Labda kama unataka kufanya kazi customer care za vodacom, Airtel etc ambao hawajali Taaluma yako, wao mradi uwe na degree na ujue mshahara mtagawana nusu kwa nusu kila mwezi.
 
Pole sana...kazi zinasumbua uchumi unakua kwa kasi ndogo ya kuweza kuajiri kila mtu anayetafuta kazi. We have to start planning and think outside the box
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom