Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
- Thread starter
- #21
Sababu za kutosoma Uhuru nishazisemaNingekushauri ujiunge na gazeti la UHURU. Kwani hata JF umeonekana hufai kuwa mwanchama.
Sababu za kutosoma Uhuru nishazisemaNingekushauri ujiunge na gazeti la UHURU. Kwani hata JF umeonekana hufai kuwa mwanchama.
Uhuru, Mzalendo, Jambo Leo, Tazama, Habari Leo, Mtanzania n.k. ndiyo magazeti yanayoharibu nchi yote. Usilete utani.Soma uhuru, mzalendo na jambo leo.
Sidhani kuwa ni sahihi. Kama Njozi ya Mwanakijiji ingekuwa kinyume cha sera yao wasingetoa matoleo zaidi ya saba ya Njozi hiyo. Na kama sera yao imebadilika ghafla na inakinzana na wasomaji basi ndiyo wengine tunajiengua kulisoma na kulinunua.Kila gazeti na sera zake, labda alipitiliza malengo ya gazeti
Ningekushauri ujiunge na gazeti la UHURU. Kwani hata JF umeonekana hufai kuwa mwanchama.
Soma uhuru, mzalendo na jambo leo.
Hivi kuandika kote huku ni kutaka hiyo njozi isiyoisha iendelee kubandikwa? Unanchekesha, si umwambie akutumie nakala ya hiyo njozi?
Mbona hamsemi Mohamed Said anapoleta makala yake humu JF asubuhi, mchana inaondolewa?
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/179304-kwa-hili-rostam-aziz-hutasameheka-8.htmlNimeamua kuandika habari hii baada ya kujishauri tangu nikiwa Igunga!
Rostam Aziz amekuwa Mbunge wa Igunga tangu mwaka 1994 ambapo mpaka sasa ni takribani miaka 17 chini ya uongozi wake. Nilikuwa sijawahi kufika Igunga kabla hivyo sikuifahamu ilivyo.Siku Rostam anajiuzulu alieleza mafanikio mengi aliyoyafanya Igunga nikadhani Igunga hali ni shwari na watu wanamaendeleo mazuri,nilivyofika sikuamini nilichokiona. Rostam alitudanganya. Katika tembea yangu yote hapa nchini sijawahi kuona Wananchi wanashida kama wa Igunga.
Mambo yafuatayo nimeyagundua katika jimbo la Igunga;
1. Wananchi wengi wa Jimbo la Igunga hawajui kusoma na kuandika mpaka vijana wadogo
2. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 13 kufuata maji kwenye Makomero tena maji yenyewe sio safi wala salama
3. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 10 kufuata shule,wengine wanaenda hadi 20
4. Kwenye kata nilizopita hawaelewi wala kuzijua shule za awali.
5. Wananchi wengi wanatembea umbalimrefu kufuata Zahanati na hayo majengo yenyewe ya Zahanati unaweza kulia.
6. Hakuna barabara za kuunganisha kijiji kimoja na kingine,njia zilizopo ni mapitio ya ng'ombe.
7. Wananchi wengi hawana vyoo wala hawana mpango wa Kujenga vyoo,wao wajenga mabafu tu yanayotumika kuogea na kujisadia haja ndogo,haja kubwa utajua mwenyewe.
8. Zipo Kata ambazo hazing mawasiliano ya simu
9. Lipo Kabila mpaka leo wanatembea uchi kama kwa King Muswati.
10. Wapo wanaotembea karibu Kilomita 13 kufuata TV waone taarifa ya habari na mambo mengine. Hii ni Kata anayotoka Dr. Kafumu
11. Na mengine mengi madogo madogo.
Rostam alikuwa na uwezo wa kupunguza hayo niliyoyataja kwasababu zifuatazo
1. Alikuwa ni Mbunge hivyo alikuwa na fursa ya kupiga kelele ndani na nje ya Bunge na akasililizwa.
2. Alikuwa Mbunge mwenye ushawishi ndani ya chama chake hivyo angeweza kushawishi Mawaziri ili miradi iende Jimboni kwake.
3. Alikuwa Mbunge tajiri sana,kama aliweza kuipa CCM,Mabilioni ya shillingi,Kama aliweza kuhonga watu mbalimbali mamilioni ya shilingi alishindwaje kusaidia Jimboni kwake? aliishia kuwanunulia tu simu Mabalozi wa Nyumba Kumi ili wamfanyie Kampeni.
4. Alikuwa anafahamiana na wafadhili wengi tu wa Maendeleo wa ndani na nje ya nchi alishindwaje kuwashawishi wawekeze kwake?
Rostam aliyaweza haya yote lakini hakujali kwakuwa hakuwa na lengo la kuwatumikia Wananchi wa Igunga. Kwasababu hizo basi nashawishika kusema kuwa Rostam ni zaidi ya DUBWANA ni mtu anayeongoza kwa roho mbaya hapa nchini. Hana huruma hata kidogo, anajali maslahi yake tu.. Bora ulivyojiuzulu, ungejiuzulu na utanzania kabisa, ukaombe uraia wa nchi nyingine huko ughaibuni sio Afrika!
Nawasilisha!
Ndugu huu siyo muda wa utani, ni wakati wa kurejesha utaifa unapokwa na CCM. Nilichosema ndicho sahihi, Mwanakijiji alishasema amefika mbali sana na Njozi yake bali hajui kwa nini haitoki. Hakuna sababu ya kudanganya ili kiwe nini?
Nilisoma Njozi zake kuanzia mwanzo hadi mwisho, nikaridhika kuwa ilikuwa na mawazo mazuri sana na hoja za kupambana na wanaoharibu utaifa wetu. Nishasema awali mwanakijiji alishasema wazi kuwa yeye ameendelea kuandika njozi yake kama kawaida lakini Tanzania Daima hawazichapishi.
Haya ni magazeti hovyo kabisa, ndiyo haya yanayosambaza siasa chafu za kuwagawa Watanzania kibaguzi. Hayafai yalipaswa kuwa yamefungiwa na wizara hisika siku nyingi. Lakini kwa kuwa wizara ni CCM na CCM ndiyo inayoongoza kubomoa misingi ya nchi yetu ndiyo maana yanaachwa tu.
Asante kwa ushauri, ila sijui nitayasomea wapi, manake nachelea kuwaharibu wajukuu.mdogo wangu wazo lako zuri sana ila usijari unaweza kusoma kama uwazi,ijumaa,sani,amani,na kiu yatakufaa wakati ukisubili uzalendo wa tanzania daima.
Huwa nalisoma ila sijui kama ni la CDMSoma Mwanahalisi, gazeti la CDM
Nilishamwomba anitumie, lakini hata nikiisoma peke yangu lengo la kukuza uzalendo miongoni mwa watanzania walio wengi halitatimia. Kama nilivyosema awali Tanzania Daima kama lilivyo jina lake linatakiwa litambue habari zinazojenga mawazo na hoja za kuinganisha nchi kuliko kuibomoa kama wanavyofanya CCM hivi sasa katika siasa zao uchwara. Hivi ilikuwa ni jambo zuri kuchapisha njozi ile hadi hitimisho la ujumbe uliokusudiwa linafikiwa. Lakii sasa hoja zilikuwa zinaendelea na hitimisho bado wao wameacha kuchapisha.Mwambie mwanakijiji akutumie basi hizo njozi uzosome.
Au kwenye Tanzania Daima ulikuwa unasoma njozi tu? Kama ndivyo, basi wewe sio msomaji wa Tanzania Daima.
Mimi sikuona marudio, kila sehemu ilikuwa na ujumbe mpya. Habari ya kitabu ni wazo zuri pia, lakini kukuza uzalendo katika nchi yetu unauliwa na CCM tunahitaji mbinu mbalimbali za kuurejesha ikiwemo kuchapisha katika magazeti na baadaye kitabu.yawezekana wameona kuna marudio mengi humo. Isitoshe ni njozi. Mwambie atunge kitabu mkuu upate nakala yako ya kudumu