nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
JUMAMOSI, OCTOBA 06, 2012 08:23 NA MWANDISHI MAALUMU, OTTAWA
RAIS Jakaya Kikwete amesema, anashangazwa na jitihada za upotoshaji wa makusudi wa ukweli kuhusu miradi ya maendeleo, inayobuniwa na kuanzishwa na Serikali yake.
Hata hivyo, Rais Kikwete amesema upotoshaji huo, hautaifanya Serikali yake ibadili uwamuzi wake kuhusu miradi ya maendeleo ya wananchi, ama kuacha kubuni miradi mipya.
Rais Kikwete, alitoa kauli hiyo juzi wakati alipohojiwa na mwandishi wa habari mwandamizi wa Gazeti maarufu la Canada la Globe & Mail, Michael Posner.
Katika shughuli ya kwanza, Rais Kikwete alizungumzia masuala mbalimbali yakiwemo jitihada za Serikali kuendeleza kilimo na mipango ya kujenga barabara kupitia Loliondo.
"Kamwe hatujapata kuwa na mipango ya kujenga barabara ya lami kukatisha Mbunga ya Serengeti. Huu ni upotoshaji wa kushangaza. Najua ni upotoshaji wa makusudi, hata kama sijui unaanzia wapi. Nadhani watu hawa wanataka kunihujumu tu,
…tumesema na kusema tena kuwa, tunalo jukumu la maendeleo kwa wananchi wote, wakiwemo wa Loliondo na Mugumu, ambao tumesema tutawajengea barabara ya lami."
"Tunajenga barabara za lami zenye urefu wa kilomita 11,000 ili kuunganisha nchi nzima. Hivyo, wananchi wa Lolindo na Mugumu, nao watakuwa sehemu ya maendeleo haya makubwa ya barabara. Hakuna mtu atakayepitisha barabara ya lami ndani ya Serengeti.
Kwa hakika, kwa upande wa Loliondo, barabara ya lami itaishia kiasi cha kilomita 80 kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti."
Alipoulizwa kwa nini Serikali yake haionyeshi uchangamfu mkubwa kuhusu ujenzi wa barabara ya lami kupitia Kusini mwa Serengeti, badala ya barabara hiyo kupita Kaskazini ndani ya mbunga, kama inavyopendekezwa na baadhi ya wafadhili, Rais alisema, "Tunakaribisha wazo na ujenzi wa barabara kusini mwa Serengeti, lakini barabara hiyo haitakuwa jibu la matatizo ya usafiri kwa wakazi wa kaskazini. Barabara ya kusini itahudumia watu wa kusini na wala siyo watu wa kaskazini."
Kuhusu suala jingine ambalo linachochewa kwa njia nyingi na kwa kila namna kuwa, Serikali inapora ardhi ya wakulima wadogo na kuitoa kwa wakulima wakubwa, ili kufanikisha mageuzi ya kilimo nchini, Rais alisema:
"Huu ni upotoshaji mwingine wa mipango yetu ya maendeleo. Sijui upumbavu huu unatoka wapi? Tunchofanya sisi chini ya mipango yetu ya kuleta mageuzi katika kilimo cha Tanzania, ni kumsaidia mkulima mdogo kwa kulinda na kuiendeleza ardhi yake, ili kumwokoa na njaa, kumpunguzia umasikini na kuongeza usalama wake wa chakula.
Hakuna mkulima mdogo ambaye atanyang'anywa ardhi yake, katika mipango yetu ili apewe mkulima mkubwa."
Hata hivyo, Rais Kikwete amemwambia mwandishi huyo kuwa upotoshaji huo, hautaifanya Serikali yake kuogopa na kushindwa kutelekeza majukumu yake ya maendeleo kwa wananchi kama ilivyoahidi kwenye Ilani yake ya uchaguzi Mkuu.
Hata hivyo, Rais Kikwete amesema upotoshaji huo, hautaifanya Serikali yake ibadili uwamuzi wake kuhusu miradi ya maendeleo ya wananchi, ama kuacha kubuni miradi mipya.
Rais Kikwete, alitoa kauli hiyo juzi wakati alipohojiwa na mwandishi wa habari mwandamizi wa Gazeti maarufu la Canada la Globe & Mail, Michael Posner.
Katika shughuli ya kwanza, Rais Kikwete alizungumzia masuala mbalimbali yakiwemo jitihada za Serikali kuendeleza kilimo na mipango ya kujenga barabara kupitia Loliondo.
"Kamwe hatujapata kuwa na mipango ya kujenga barabara ya lami kukatisha Mbunga ya Serengeti. Huu ni upotoshaji wa kushangaza. Najua ni upotoshaji wa makusudi, hata kama sijui unaanzia wapi. Nadhani watu hawa wanataka kunihujumu tu,
…tumesema na kusema tena kuwa, tunalo jukumu la maendeleo kwa wananchi wote, wakiwemo wa Loliondo na Mugumu, ambao tumesema tutawajengea barabara ya lami."
"Tunajenga barabara za lami zenye urefu wa kilomita 11,000 ili kuunganisha nchi nzima. Hivyo, wananchi wa Lolindo na Mugumu, nao watakuwa sehemu ya maendeleo haya makubwa ya barabara. Hakuna mtu atakayepitisha barabara ya lami ndani ya Serengeti.
Kwa hakika, kwa upande wa Loliondo, barabara ya lami itaishia kiasi cha kilomita 80 kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti."
Alipoulizwa kwa nini Serikali yake haionyeshi uchangamfu mkubwa kuhusu ujenzi wa barabara ya lami kupitia Kusini mwa Serengeti, badala ya barabara hiyo kupita Kaskazini ndani ya mbunga, kama inavyopendekezwa na baadhi ya wafadhili, Rais alisema, "Tunakaribisha wazo na ujenzi wa barabara kusini mwa Serengeti, lakini barabara hiyo haitakuwa jibu la matatizo ya usafiri kwa wakazi wa kaskazini. Barabara ya kusini itahudumia watu wa kusini na wala siyo watu wa kaskazini."
Kuhusu suala jingine ambalo linachochewa kwa njia nyingi na kwa kila namna kuwa, Serikali inapora ardhi ya wakulima wadogo na kuitoa kwa wakulima wakubwa, ili kufanikisha mageuzi ya kilimo nchini, Rais alisema:
"Huu ni upotoshaji mwingine wa mipango yetu ya maendeleo. Sijui upumbavu huu unatoka wapi? Tunchofanya sisi chini ya mipango yetu ya kuleta mageuzi katika kilimo cha Tanzania, ni kumsaidia mkulima mdogo kwa kulinda na kuiendeleza ardhi yake, ili kumwokoa na njaa, kumpunguzia umasikini na kuongeza usalama wake wa chakula.
Hakuna mkulima mdogo ambaye atanyang'anywa ardhi yake, katika mipango yetu ili apewe mkulima mkubwa."
Hata hivyo, Rais Kikwete amemwambia mwandishi huyo kuwa upotoshaji huo, hautaifanya Serikali yake kuogopa na kushindwa kutelekeza majukumu yake ya maendeleo kwa wananchi kama ilivyoahidi kwenye Ilani yake ya uchaguzi Mkuu.