Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Aliingia madarakani kwa kauli mbiu ya Ari Mpya Nguvu Mpya. Kasi Mpya wengine walimuona kweli Chaguo la Mungu Kaulimbiu iliyogeuka kuwa janga la taifa na chama chetu tukufu CCM. Katika kipindi chake cha uongozi, Rais Kikwete amegeuka kuwa mzigo na aibu kwa taifa; amekumbatia udini, amejenga makundi ndani ya chama chetu.
Ametumia cheo chake kukifedhehesha taifa. Amekuwa rais wa kwanza kuongwa suti nchini Tanzania. Rais wetu hajui kwa nini watanzania maskini, na wala hajui Ikulu anafanya nini. Hii ni kwa sababu meli za Iran zinasajiliwa akiwa safarini marekani bila yeye kujua
Ameifanya CCM kuchukiwa kila kona ya nchi. Amekuwa rais wa kwanza kupigwa mawe na wananchi. Hivi kweli tunaelekea wapi? Mh. RAIS. Utakosa nini ukiyaacha madaraka kukinusuru chama na Taifa!
Rais Kikwete amekumbatia ufisadi na mafisadi. Hapa namaanisha EPA, Richmond, mabillioni uswisi nk. Katika uongozi wake, uonevu wa polisi umepitiliza. Raia wanatekwa na kuuwawa kinyama. Mahakama zetu zimekuwa za kulinda maslahi ya viongozi. Urasimu, rushwa, kugawana vyeo vimezidi.rasilmali za nchi zinayeyuka, umasikini umekithiri huku huduma za jamii zote zinatoweka. Aibu kwa CCM.
Ili kukinusuru chama chetu mama (CCM) N.E.C lazima ifanye mpango wa kumuondoa Kikwete haraka iwezekanavyo. Hatuwezi tena kujidanganya kwamba chama chetu kinapendwa. Vinginevyo tusubiri kihama 2015 huku mkiyaweka kwenye kumbukumbu huu waraka wangu
MTOTO WA CCM
Ametumia cheo chake kukifedhehesha taifa. Amekuwa rais wa kwanza kuongwa suti nchini Tanzania. Rais wetu hajui kwa nini watanzania maskini, na wala hajui Ikulu anafanya nini. Hii ni kwa sababu meli za Iran zinasajiliwa akiwa safarini marekani bila yeye kujua
Ameifanya CCM kuchukiwa kila kona ya nchi. Amekuwa rais wa kwanza kupigwa mawe na wananchi. Hivi kweli tunaelekea wapi? Mh. RAIS. Utakosa nini ukiyaacha madaraka kukinusuru chama na Taifa!
Rais Kikwete amekumbatia ufisadi na mafisadi. Hapa namaanisha EPA, Richmond, mabillioni uswisi nk. Katika uongozi wake, uonevu wa polisi umepitiliza. Raia wanatekwa na kuuwawa kinyama. Mahakama zetu zimekuwa za kulinda maslahi ya viongozi. Urasimu, rushwa, kugawana vyeo vimezidi.rasilmali za nchi zinayeyuka, umasikini umekithiri huku huduma za jamii zote zinatoweka. Aibu kwa CCM.
Ili kukinusuru chama chetu mama (CCM) N.E.C lazima ifanye mpango wa kumuondoa Kikwete haraka iwezekanavyo. Hatuwezi tena kujidanganya kwamba chama chetu kinapendwa. Vinginevyo tusubiri kihama 2015 huku mkiyaweka kwenye kumbukumbu huu waraka wangu
MTOTO WA CCM