CPU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 3,863
- 686
Mzungu mmoja ambaye sikuweza kufahamu jina lake aliamua kuvua nguo zake zote akiacha ya ndani tu baada ya wakaguzi wa uwanja wa ndege Dar kuwa na wasiwasi nae.
Katika tukio hilo la aina yake leo Jan 28 asubuhi, mzungu huyo aliona ni bora achukue hatua hiyo baada ya kila akipita ktk zile mashine za kukagulia wasafiri wa ndege hapo uwanjani kupiga kelele. Cha ajabu zaid hata pale alipovua nguo na kupita bado mashine ilitoa mlio, ambapo iliwalazimu wakaguzi kwenda kumkagua kwa undani ktk vyumba vya ndani hapo airport, ambapo hakugundulika na kitu chochote cha hatari badala yake ikagundulika mashine ya ukaguzi ilikuwa mbovu.
Watu wengi waliokuwa karibu na eneo hilo walishtushwa na hatua ya huyo mzungu lakin wakatoa lawama kwa uongozi wa airport.
Baadae mzungu huyo aliruhusiwa kuendelea na safari yake na ametishia lazima akaushitaki uwanja kwa Baraza la Viwanja vya ndege Duniani
Habari hii nimeikusanya mimi mwenyewe CPU nilipokuwa ktk eneo la tukio
Katika tukio hilo la aina yake leo Jan 28 asubuhi, mzungu huyo aliona ni bora achukue hatua hiyo baada ya kila akipita ktk zile mashine za kukagulia wasafiri wa ndege hapo uwanjani kupiga kelele. Cha ajabu zaid hata pale alipovua nguo na kupita bado mashine ilitoa mlio, ambapo iliwalazimu wakaguzi kwenda kumkagua kwa undani ktk vyumba vya ndani hapo airport, ambapo hakugundulika na kitu chochote cha hatari badala yake ikagundulika mashine ya ukaguzi ilikuwa mbovu.
Watu wengi waliokuwa karibu na eneo hilo walishtushwa na hatua ya huyo mzungu lakin wakatoa lawama kwa uongozi wa airport.
Baadae mzungu huyo aliruhusiwa kuendelea na safari yake na ametishia lazima akaushitaki uwanja kwa Baraza la Viwanja vya ndege Duniani
Habari hii nimeikusanya mimi mwenyewe CPU nilipokuwa ktk eneo la tukio