MzalendoHalisi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2007
- 4,519
- 1,367
Mzalendohalisi:
Wewe sio educator na sababu unazotoa zinaboronga. Kwa maendeleo ya automation yaliopo sasa vyuo vya ufundi wa kati havina tena mpango.
Hata hayo mapinduzi ya kilimo unachosema wewe hayaji kwa kuanziswa shule za VETA. Kumbuka kuwa kila wilaya ilikuwa na shule ya sekondari ya kilimo na vyuo kibao vya maafisa kilimo wa ngazi mbalimbali na bado output ya mavuno kwa heka moja kwa Tanzania ni ndogo sana hata kwa kulinganisha na nchi za kiAfrika.
Nchi zinazoendelea zimehamua kufuata R&D (Research and Development) approach. Vichwa vinafanya kazi (R&D) na baadaye instructions zinapewa kwa watu wanaofanya production kufuatwa. Mtu yoyote mwenye akili timamu akipewa masharti ya kupanda mpunga atafuata na hakuna sababu ya kumpeleka chuo miaka mingi.
Kwa mtaji wa niliyoyasema vyuo vikuu ni muhimu. Na kama tunataka middle level, hicho ni kitu rahisi sana. Tuanzishe system ya entry level. Mtu yoyote anayemaliza chuo kikuu basi afanze kazi kama entry level kwa muda wa zaidi ya miaka miwili. Na kutokana na juhudi zake za kazi basi middle na senior level zifuate.
Hule utaratibu wa kuwa mtu ametoka chuo kikuu basi anakuwa Injinia umeharibu sana ufanisi wa makazi. Watu wengi wana akili za kufaulu mitihani lakini ni mabox kwenye kazi.
Papa Zakumi!
Ahsante! Je dawa ni kuachia free market? 80% wasome Ngiwini???
Siafikiani na hili!