Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,844
- 2,665
Kwanza nawaonea huruma ccm.Mwanasiasa mkongwe na kada wa CCM, Chrisant Mzindakaya amekitaka chama cha Mapinduzi CCM kujibu hoja za Chadema kwa kuwatumia viongozi wa mikoa ambayo Chadema wanafanya mikutano badala ya kumsubiri Waziri Mkuu au rais kujibu hoja.
"Viongozi wa CCM katika mikoa ambayo Chadema wanapita na kutoa hoja zao, wajibu kwa kuponda hoja hizo ili wananchi waelewe hali halisi na siyo kumsubiri Waziri Mkuu au Rais kujibu hoja," alisema Mzindakaya.
Amehoji iweje Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kuwa kimya muda wote kama iko likizo na kuiachia Serikali kazi ya kisiasa hasa katika kipindi hiki?
Source: HabariLeo
Wana mzigo wa kukisafisha chama kutokana na mavuvuzela kama Makamba Sr.
Pili wana kazi ya kujibu hoja toka kwa chadema
Wana kazi ya kujisafisha mbele ya watazania utokana na yale wanayoshutumiwa
Wana kazi ya kutekeleza ahadi lukuki walizoahidi 2005-2010
n.k, n.k, n.k..............................................
Mwacheni JK akonde......