apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Ni Waziri Mkuu mwenye huruma na upendo kuliko wote waliopita,amewahi kulia juu ya mauaji ya Albino, ni mtoto wa Mkulima anayejua kijiji na kilimo kwanza nini. Pinda amekaa Ikulu muda mrefu kama mwana usalama toka enzi za Mwalim hivyo anamjua Mwalim vizuri ingawa hakuwa gwiji la siasa.
Amekuwa akijibainisha kama mfuasi wa sera za Mwalim hasa katika falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea,ni mkubwa sasa katika nafasi ya tatu kutoka kwa Rais huku bara.Nafasi yake inawagusa wote walioko ndani ya Nchi,hivyo lolote analolifanya ama tenda ni taarifa kwa umma.
Pinda toka ateuliwe baada ya Lowassa inasemekana hajawahi kuzuru katika kaburi la Baba wa Taifa wala kutoa pole akiwa Waziri Mkuu. Tunajua si lazima kufanya hivyo kwani hili ni suala la kibinadamu zaidi ndio maana kuna watu hawakosi katika misiba na wengine misiba ni kituo cha polisi.
Pinda amefika mkoani Mara mara nyingi tu, hasa Tarime na kwingineko,hivi ni kweli hakujua ama hajui Mwalimu amelala pale Butiama na watu wanatoka mataifa ya mbali kuzuru pale. Binafsi nashangaa na nimeshitushwa na kauli ya Familia ya Mwalim yenye uchungu juu ya Binadamu huyu Kayanza.
Pengine nadhani aidha alipitiwa ama amezidiwa na msongo wa mawazo ya Kitaifa na kusahau historia ya Taifa hili. Pinda anaendeshaje Nchi bila kujua historia wakati ilikuwa sehemu ya Masomo yake yaani HGL mpaka kuwa Mwanasheria.
Pinda rudisha utu kwani death is an innevitable destiny,usije ukaipa shida familia yako pindi nawe utakapo kick the moon (pass away). Uzalendo ni pamoja na kujaliana katika shida na simanzi. Haiwezekani mtoto wa Idd Amin, adui mkubwa wa Taifa hili na Mwalim pia kuzuru kabuli na kutoa pole,wewe kiongozi Mkuu unapita tu Butiama.
Pinda bila Mwalim usingekuwepo wewe,shule umesoma bure,madaraka umepata, pesa unayo,ulinzi unao,usafiri upo,muda unao leo unashindwa kuitembelea familia ya Mwalimu? Msiba hauozi na hata kama ukioza historia haifutiki. Haya yamejitokeza baada ya Madiwani wa Mkoa wako wa zamani kutembelea Shule ya Mwalimu na kuikuta iko katika hali mbaya na isiyo na historia tena. Swali liliulizwa kama Waziri Mkuu anajua hali hii,ikabainika hajawahi kutia mguu si katika shule bali hata katika Kaburi.
Pinda hata kama hu-anti-social ama una aleji na misiba au makaburi, ukiwa kiongozi wa kitaifa ni muhimu uka-declare interest kwa hayo Wananchi tukakujua na si kuacha tu-feel gap na matokeo yake ni grapevines.
Panga safari uende na uombe radhi kwa hilo acha mambo ya kujitenga na jamii,umepata yote hayo kwa njia nyoofu aliyojenga Mwalimu. Shame on u Pinda.
Amekuwa akijibainisha kama mfuasi wa sera za Mwalim hasa katika falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea,ni mkubwa sasa katika nafasi ya tatu kutoka kwa Rais huku bara.Nafasi yake inawagusa wote walioko ndani ya Nchi,hivyo lolote analolifanya ama tenda ni taarifa kwa umma.
Pinda toka ateuliwe baada ya Lowassa inasemekana hajawahi kuzuru katika kaburi la Baba wa Taifa wala kutoa pole akiwa Waziri Mkuu. Tunajua si lazima kufanya hivyo kwani hili ni suala la kibinadamu zaidi ndio maana kuna watu hawakosi katika misiba na wengine misiba ni kituo cha polisi.
Pinda amefika mkoani Mara mara nyingi tu, hasa Tarime na kwingineko,hivi ni kweli hakujua ama hajui Mwalimu amelala pale Butiama na watu wanatoka mataifa ya mbali kuzuru pale. Binafsi nashangaa na nimeshitushwa na kauli ya Familia ya Mwalim yenye uchungu juu ya Binadamu huyu Kayanza.
Pengine nadhani aidha alipitiwa ama amezidiwa na msongo wa mawazo ya Kitaifa na kusahau historia ya Taifa hili. Pinda anaendeshaje Nchi bila kujua historia wakati ilikuwa sehemu ya Masomo yake yaani HGL mpaka kuwa Mwanasheria.
Pinda rudisha utu kwani death is an innevitable destiny,usije ukaipa shida familia yako pindi nawe utakapo kick the moon (pass away). Uzalendo ni pamoja na kujaliana katika shida na simanzi. Haiwezekani mtoto wa Idd Amin, adui mkubwa wa Taifa hili na Mwalim pia kuzuru kabuli na kutoa pole,wewe kiongozi Mkuu unapita tu Butiama.
Pinda bila Mwalim usingekuwepo wewe,shule umesoma bure,madaraka umepata, pesa unayo,ulinzi unao,usafiri upo,muda unao leo unashindwa kuitembelea familia ya Mwalimu? Msiba hauozi na hata kama ukioza historia haifutiki. Haya yamejitokeza baada ya Madiwani wa Mkoa wako wa zamani kutembelea Shule ya Mwalimu na kuikuta iko katika hali mbaya na isiyo na historia tena. Swali liliulizwa kama Waziri Mkuu anajua hali hii,ikabainika hajawahi kutia mguu si katika shule bali hata katika Kaburi.
Pinda hata kama hu-anti-social ama una aleji na misiba au makaburi, ukiwa kiongozi wa kitaifa ni muhimu uka-declare interest kwa hayo Wananchi tukakujua na si kuacha tu-feel gap na matokeo yake ni grapevines.
Panga safari uende na uombe radhi kwa hilo acha mambo ya kujitenga na jamii,umepata yote hayo kwa njia nyoofu aliyojenga Mwalimu. Shame on u Pinda.