ktk jamii zote duniani tunaamini uwepo wa mizimu na madhara yake iwapo mzimu huo utakuwa na ujumbe wa kutoa na usisikilizwe. ndipo, kwa dalili zinazojitokeza wahusika huenda kwa wajuzi wakajuzwa nini kifanyike ili kuepukana na majanga yanayoikuta jamii husika. Basi mwaka jana nilisoma ktk gazeti kuwa kuna mama mmoja huko kusini mwa Tanzania anateseka na mzimu wa Mwl. Nyerere na alikuwa na ujumbe kwa Rais wetu kutoka kwa Hayati Baba wa Taifa letu. Kwa tabia ya viongozi wetu kujifanya mambo hayo hawajui huku kukicha wanayafanya naweza amini kabisa kuwa mama huyu maskini hajaweza kusikilizwa. Ushauri; wahusika hakikisheni mama huyu anakutana na rais, rais si Mungu hata aogopwe, kwanza ni mpenda watu tumeona kule Iringa amekaa chini akiongea na mama mwenye ulemavu. Huenda matatizo ya nchi hii yakapungua kama huyo mama akisikilizwa. kisha rais awaite viongozi wa dini kama Laizer, shehe mkuu, Pengo, viongozi wa waasia(inangawa hawakukumbukwa ktk kumuapisha rais) na kiongozi wa wapagani na butiama awepo kiongozi wao, asiwepo Malasusa.Kisha wa 'discuss' jambo hilo kiimani ambalo huyo mama atamwambia rais. Ikumbukwe Mwl. alikuwa na nia kuona kusini mwa Tz kunaendelea kuliko. Asanteni.