tzjamani
JF-Expert Member
- Oct 9, 2010
- 995
- 30
Mzee wangu simuelewi kabisaaaaa. Mwaka wa 4 huu amekuwa akinisisitiza nitafute mwanamke mwenye sifa zifuatazo :-
- Awe na elimu isiyopungua form six, na kama ana six awe na mpango wa kusoma zaid ya hapo
- Asiwe mzungu, mhindi wala mchina
- Awe anaingiza kipato kama kazi au biashara
- Asiwe "mtoto wa mjini"
Na mbaya zaidi atataka amu-interview kama ana uwezo wa kujieleza, kabla hajaamua kumkubali. Ninacho shangaa, hajawahi kunieleza kama mapenzi ni muhimu au sio muhimu. Na kali zaidi mke wake mwenyewe (maza) kaishia la 7. Naona kama kuna mbinu za kunitafutia mke hivi . . . .
Mkuu baba kuna mambo amejifunza katika maisha yake. Hilo la mama kuishia la 7 inawezeka ndio maana anakuambia umchague mwenye elimu ilimsaidia kwenye maisha.
Huyo ni baba yako naamini anataka kukupa samaki wala siyo joka.
Una bahati ya kuelekezwa na baba, Hebu kaa naye chini akupe busara zake nawe umshirikishe mawazo na matamanio yako.
Zungumzeni kwa hisa ya TZ.