Mzee wa Upako ampinga Prof. Shivji suala la Muswada Katiba Mpya

huyo lusekelo naye ni gamba. hawa ni wale wachungaji matumbo mbele wanatumiwa na magamba.
hawa wachungaji wa uchochoroni wanatabu sana.

Mchungaji ambae akisafiri waumini wanakuwa likizo mpaka akirudi
 
My hairs!
Hivi amewahi kuisoma katiba huyu mchungaji!
Hawa ndio wale wanaenjoy mazingira wanayoandaliwa na waumini na fedha za sadaka, wanachojua wao ni kuwa nchi hii ni ya maziwa na asali!

Sidhani hata kama kava la kitabu cha katiba kama analijua
 
Lusekero wewe fukuza mashetani ndani ya mioyo ya wanakondoo; lakini uchambuzi wa mambo ya Siasa na Uchumi waachie wenyewe walibobea kaka yangu. upeo na karama anagawa mwenyezi sasa wewe umepewa hiyo na wengine wamepewa nyinginezo...

Labda anataka kutuambia kapewa zote
 
Hana sifs za kumpinga Prof SHIVJI maana hata istoria yake haifahamiki katika mchango wa taifa,siyo kila kiongozi wa dini anamaono juu ya taifa la msingi ni kumpuuza na kusifu jitihada za mzee shvji ambaye siku zote analitakia taifa hili maendeleo

Nadhani kama anania njema na taifa hili na anamtumikia Mungu kweli amwombee Jk abadilike na awe msikivu asiyekumbatia wizi unaofanya na magamba wanaomtumia hapo atakuwa amefanya jambo ambalo hata Mungu mwenyewe atatabasam
 
huyo lusekelo naye ni gamba. hawa ni wale wachungaji matumbo mbele wanatumiwa na magamba.
hawa wachungaji wa uchochoroni wanatabu sana.
Anapalilia ombi lake la kutambuliwa kama akina Mhashamu Pengo anaposafiri etinaye ahesabiwe kama VIP asikaguliwe uwanja wa ndege. yeye anaona KUTOKUKAGULIWA ni la maana sana. sijui anataka kuficha nini?
 
Prof Isa Shivji yuko sahihi, Mchg ama hajui asemalo au ametumwa na ccm ya JK.

Dalili za kutumwa hizo,ila siku si nyingi naye ataumbuka,wapi kina Lwakatare na wengine?

Hawezi kutumikia mabwana wawili yaani pesa na mungu kwa muda mrefu
 
Hawa wachungaji wa makanisa ya kilokole wengi wao ni wawekezaji na ndo maana hawaishi migogoro mchungaji ukiwa kampeni manager wa mgombea wa kisiasa utawhubiria nini waumini wako ambao ni wanavyama tofauti?
 
Huyu jamaa kingereza tu kinamsumbua sasa ana ubavu gani wa kufanya analysis ya muswaada?yeye aendelee na uchambuzi wa mambo ya kiroho na siasa awaachie wenyewe
 
Mzee wa Upako aka Mch Antony Lusekelo amesema kwa kuwa Rais Kikwete amesha saini mswaada wa katiba mpya kinachotakiwa sasa ni kuaminiana tu hakuna haja ya kuupinga!.Amewataka wananch na wadau mbalimbali kujitokeza na kuunga mkono Mswaada huo kwa kuchangia mawazo.Amesema Katiba iliyopo sasa haina makosa mengi ya kurekebisha! Source :gzt Mwananch leo

Moja la tatizo kubwa la huyu jamaa anayejihita mchungaji mara mzee wa upako ni njaa na kujipendekeza...ni huyu huyu mchungaji aliyekataa vitabu vyake vya pesa kupitiwa...ni huyu mchungaji aliyekuwa anawataka watu wachangie kanisa lake kupitia account binafsi yenye jina lake....ni huyu mchungaji aliyetamka kuwa pale kanisani kwake yeye ndie anaruhusiwa kuhubiri maana ndio baba hakuna mwingine..ni huyu mchungaji anayewataka waumini wake waamini kuwa huo upako anaojifanya kuwa anao hakuna mtu mwingine anayeweza kuupata zaidi yake...

Kwa hali kama hii sitegemei chema kutoka kwa huyu fisadi na anayetumiwa na serikali ya JK kutupotosha watanzania..huyu jamaa ni kati ya matapeli wakubwa sana pale DSM..anatumia jina la Yesu kuficha uovu wake....
 
Huyu jamaa kingereza tu kinamsumbua sasa ana ubavu gani wa kufanya analysis ya muswaada?yeye aendelee na uchambuzi wa mambo ya kiroho na siasa awaachie wenyewe

Hata kiroho bado anatudanganya tu...huyu ni mfanyabiashara na usije kuta yupo kwenye orodha ya maaskofu wanaouza madawa ya kulevya...
 
Hv lusekelo Ana upeo gani wa kufikiri? Amewahi kutabili mambo kibao hamna hata moja limetokea kuhusiana na chaguz pamoja na uongoz kitaifa, hafai hata kwa Akiba!
 
I miss bishop kakobe for sure...sjui yuko wapi,kimyaaaah! Hata vipindi vya tv hana sku izi..back in those days,he would have also spoken a thing or two kuhusu hizi big issues
 
Nimesikia mzee wa Upako akikemea siasa za Chuki ndani ya CCM wakati yeye alijitangaza kuwa Kampeni manaja wa Jk 2010.Hata hivyo yeye Mzee wa Upako anachuki kubwa na Askof Mwasata katibu mkuu PCT.Askof Mwasota ndiye aliye mchukua mzee wa Upako Mby baada ya maombi ya mama yake .Mwasota alimfundisha Mzee wa upako kozi ya Uchungaji na kufungua tawi la Kibangu.Baada ya kupata sadaka nyingi Mch.Lusekelo akampindua Askof Mwasota na kujiita Mzee wa upako na kusajili upya.Hadi leo Mzee wa Upako haelewani na Askof Mwasota.Mwaka 2010 Mzee Upako akiwa kampenia Jk alifanya njama na kumuweka ndani Askof Mwasota kwa kisingizio kuwa amemuibia Tsh20m, Kwa kutuma majambazi.RPC alituma watu wake na kufanya uchunguzi ikabainika kuwa ni chuki
Za kidini na Madaraka yalitokana yalitokana


Mkuu nakubaliana nawe kabisa.

Lusekelo ameonesha kuwa ni mtu wa chuki, hasira na kisasi. Vilevile ni muongo, mroho wa pesa na Tapeli kwa waumini wake. Hivi vyote viko kinyume na UPAKO!

He is not clean at all, na amejileta mwenyewe kwenye darubini achambuliwe.


Rejeeni makala hii:


1 Oktoba 2011

TUKIO la hivi karibuni la kuvamiwa kwa Mchungaji wa Kanisa la Maombezi Utashinda, Anthony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako (pichani) na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi limechukuwa sura mpya baada ya watumishi wawili wa Mungu kuhojiwa.

Waliohojiwa katika tuhuma hizo nzito za kuvamiwa kwa Mzee wa Upako na kuibiwa mamilioni ya shilingi ni Askofu David Mwasota na Mchungaji Frank Chacha ambao wanatoa huduma kwenye kanisa la Naioth Gospel Assembly lililopo Ubungo Kibangu jijini Dar es Salaam.

Vyanzo vyetu vya habari vilidai kwamba Mchungaji David Mwasota alikamatwa na polisi na kuhojiwa kwa zaidi ya saa 6 katika Kituo cha Mbezi jijini Dar es Salaam kuhusiana na tukio hilo na kutakiwa kumfikisha katika kituo hicho Mchungaji wake Frank Chacha.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, inadaiwa kuwa mara baada ya Askofu Mwasota kumfikisha kituoni hapo, Mchungaji Chacha alihojiwa kwa siku mbili mfululizo bila kupata dhamana kwa madai kwamba kama angeachiwa haraka angevuruga upelelezi wa polisi.


“Baada ya Askofu Mwasota kumfikisha Chacha kituoni hapo, Mchungaji huyo alishikiliwa kwa muda wa siku mbili akihojiwa,” kimoja cha chanzo chetu ambacho tunakihifadhi jina lake kilisema.

Iliendelea kudaiwa kwamba Mzee wa Upako alihisi kuwa Mchungaji Chacha alihusika na tukio hilo kutokana na ujumbe mfupi wa maneno (SMS) aliomtumia, hivyo akaamua kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.

Inadaiwa kwamba ujumbe uliotumwa kwenda kwa Mzee wa Upako ulikuwa ni wa kumpa pole kuhusiana na tukio la kuvamiwa na majambazi kisha kuporwa mamilioni ya pesa usiku wa kuamkia Septemba 27, mwaka huu.

Hata hivyo, vyanzo hivyo vilisema kwamba ujumbe aliotumiwa Lusekelo haukuwa na nia mbaya ila aliutilia mashaka kwa kuwa ulimuuliza kama alimkosea Mungu kutokana na kukumbwa na balaa hilo.

“Hilo la kuambiwa kwamba amemkosea Mungu ndilo lililomfanya mtumishi huyo kuona kama vile alikuwa akifanyiwa dhihaka katika tukio hilo la kuibiwa pesa,” kilidai chanzo chetu.

Inadaiwa kuwa Mzee wa Upako alishindwa kuelewa maana ya ujumbe huo na kuhisi kufanyiwa dhihaka na mtumishi mwenzake Chacha ambaye hakuwa na lengo baya.

Aidha, chanzo hicho kilisema kwamba hii ni mara ya pili kwa Mzee wa Upako kumtuhumu Mchungaji Chacha ambaye zamani alikuwa anatoa huduma katika kanisa lake kabla ya kutokea hali ya kutoelewana ambapo alihamia kwa mlezi wake Askofu Mwasota.

“Inawezekana ana bifu na Mchungaji Chacha kutokana na kuondoka katika huduma yake ndiyo maana ameamua kufanya hivyo, ni jambo la kusikitisha watumishi kupelekana polisi na haya siyo maadili ya kitumishi kabisa,” kiliendelea kusema chanzo hicho.

Kwa upande wa Askofu Mwasota alisema kwamba baada ya kutoka kituoni kesho yake (Jumanne) alimfuata Mchungaji Chacha na kumpeleka Kituo cha Polisi Mbezi ambapo alikaa kwa muda wa siku mbili ndipo alimtoa kwa dhamana.

“Mzee wa Upako ni mwanangu na sijagombana naye na sina matatizo naye, ila sijui kwa yeye na Mchungaji Chacha wana matatizo gani kwa sababu walikuwa watu wa karibu, nitaongea naye vizuri nijue tofauti zao,” alisema Askofu Mwasota.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga alipopigiwa simu siku ya Jumapili kuzungumzia sakata hilo alisema bado analifuatilia na tulipomtafuta kabla ya gazeti hili kuingia mitamboni simu zake zote hazikupatikana.
 
Lusekelo Anthony,
Nina wasiwasi na elimu yake ya kidunia, huyu poti
Maneno yake kwenye mambo ya siasa yanajichanganya, kama mtakumbuka aliwahi kumsifia sana JK, baada ya wiki chache akamponda mbaya kabisa!
Hivi hizo dosari chache kwenye katiba alizosema anaweza kuziainisha na kuelezea impact zake kwa jamii?
 
Huyu hana upako wowote ni pumba tu, Jana nilimsikia akisema atazuia na anazo nguvu ya kuzuia yale mafuriko yaliyotabiriwa na hali ya hewa. Nilimsikitikia yy lakini niliwasikitikia zaidi wauumini wake kuwa na mchungaji kama yule, ati anadai hakuwepo dsm yale mafuriko yalipotokea vinginevyo yasingetokea, Angekuwa na uwezo huo angeyazuia kulekule alipo ndio maana ya uwezo kiroho. Sipendi hta kusikia
 
Back
Top Bottom