MZEE WA UPAKO AJIKOMBA KWA jk

Naomba kukumbushwa majina ya wachungaji, maaskofu, watume wote waliopigia dabe kampeni za JK 2010
 
1 - kanisa la huyu bwana linaitwa GRC, kirefu chake na maana yake ni nini?

2- Itifaki ya kumwona rais kama anavyodai, zamani ilikuwaje na sasa ikoje?
 
Akimsifia kwa upuuzi tutamnanga pia. Hapa hatuangalii jina au sura ya mtu
 
Mchungaji huyu namheshimu sana lakini nadhani yeye haoni hali halisi jinsi ilivyo mtaani. Amesahau jinsi watu wanavyofanya madudu kupitia cheo cha urais, namkumbusha mzee wa upako kuwa aache kuingia kwenye siasa inaweza kumshusha hadhi haraka sana na si yeye tu bali viongozi wote wa dini.

Atajuaje shida ukimcheki mwilini ana suti ya dola 300, Prado,anakusanya mipesa pasipo kutumia nguvu.
 
Swala sio kusifia au kumsema mtu! Badala ya kupambana na wanaomsema raisi ni bora kama kiongozi wa dini akamsifia kama utashi wake unavyomtuma badala ya kuwashambulia wanaomsema. Mwisho wa siku jamii itaamua siyo individual for reasons best known to himself anakurupuka.
 
Mchungaji huyu namheshimu sana lakini nadhani yeye haoni hali halisi jinsi ilivyo mtaani. Amesahau jinsi watu wanavyofanya madudu kupitia cheo cha urais, namkumbusha mzee wa upako kuwa aache kuingia kwenye siasa inaweza kumshusha hadhi haraka sana na si yeye tu bali viongozi wote wa dini.

Njaa ya mtaani ataionaje wakati sadaka zinajileta zenyewe madhabahuni?
 
>>"Unapojenga afya ya kitu chochote ni lazima ujue misingi ya nchi ni lazima tuheshimu na kuwapenda viongozi wetu tuliochagua na kuwapigia kura. Hata katika maandiko kiongozi anatakiwa aonywe kwa hadhari, heshima na hekima na si kwa makelele.

"Utawala ni mamlaka inayowekwa Mungu lakini inaashiria wazi kuwa tumeanza kuondoka katika misingi hiyo na sasa mtu yeyote anasimama na kumsema Rais Jakaya Kikwete anavyotaka. Hapana. Hili jambo halipendezi mbele ya Mungu," alisema Mchungaji Lusekelo.

Alisema imejengeka tabia kuwa ukimsema Rais Kikwete ndiyo unaonekana kuwa jasiri na mzalendo, utamaduni ambao ni mbaya.

"Hatupo tayari kumpongeza kiongozi akiwa hai, watu wanasifu maiti kuliko mtu akiwa hai hizi ni fikra za kishetani na hazipaswi kunyamaziwa.

"Mfano Mwalimu alipokuwa hai hakuwa na sifa hizi tunazoziona sasa, walisema wazi wamechoka na 'unyerere' leo hii tunamasifu kwa kila nderemo. Watu wamebadilika wanasifu viongozi wanapotoka ndani ya madaraka.

"Inakuwaje Rais Kikwete tunayemfahamu aliingia madarakani akiitwa Masia na chaguo la Mungu leo ni adui wa kwanza. Hili linatokana na wachache wanaomsaidia rais kukiacha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA):hug:kuwa na nguvu na kikaacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa dhaifu. Hivi sasa kukitokea tatizo kama la kutonyesha mvua basi lawama atatupiwa rais," alisema

Alisema kuwa ana imani kuwa rais atakayekumbukwa maishani ni Rais Kikwete hivyo aachwe atekeleleze mchakato wa katiba kupunguza mfumko wa bei na kujenga barabara za hewani.<<
 
Bila kujijua amekinadi na kupigia chapuo cdm, kwa kuainisha kuwa kimekuwa na NGUVU kuliko CCM.
Aksante Mchungaji...naamini uliongea bila hila!
 
Kikwete ni kama Yuda Eskarioti alivyogeuka msaliti kwa Yesu. Huyu ameugeuka umma wa Tanzania ili awatumikie akina Rostam na washikaji zake. Ni ajabu kwangu kuona Rais akishangaa ghala la mahindi lilivyosheheni wakati wananchi wanalalamikia bei kupanda. Hivi akiwa hapo ikulu huwa anafanya nini kama hawezi kuwasiliana na wasaidizi wake wampe taarifa na kumshauri jinsi ya kuendesha nchi
 
>>"Unapojenga afya ya kitu chochote ni lazima ujue misingi ya nchi ni lazima tuheshimu na kuwapenda viongozi wetu tuliochagua na kuwapigia kura. Hata katika maandiko kiongozi anatakiwa aonywe kwa hadhari, heshima na hekima na si kwa makelele.

"Utawala ni mamlaka inayowekwa Mungu lakini inaashiria wazi kuwa tumeanza kuondoka katika misingi hiyo na sasa mtu yeyote anasimama na kumsema Rais Jakaya Kikwete anavyotaka. Hapana. Hili jambo halipendezi mbele ya Mungu," alisema Mchungaji Lusekelo.

Alisema imejengeka tabia kuwa ukimsema Rais Kikwete ndiyo unaonekana kuwa jasiri na mzalendo, utamaduni ambao ni mbaya.

"Hatupo tayari kumpongeza kiongozi akiwa hai, watu wanasifu maiti kuliko mtu akiwa hai hizi ni fikra za kishetani na hazipaswi kunyamaziwa.

"Mfano Mwalimu alipokuwa hai hakuwa na sifa hizi tunazoziona sasa, walisema wazi wamechoka na 'unyerere' leo hii tunamasifu kwa kila nderemo. Watu wamebadilika wanasifu viongozi wanapotoka ndani ya madaraka.

"Inakuwaje Rais Kikwete tunayemfahamu aliingia madarakani akiitwa Masia na chaguo la Mungu leo ni adui wa kwanza. Hili linatokana na wachache wanaomsaidia rais kukiacha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA):hug:kuwa na nguvu na kikaacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa dhaifu. Hivi sasa kukitokea tatizo kama la kutonyesha mvua basi lawama atatupiwa rais," alisema

Alisema kuwa ana imani kuwa rais atakayekumbukwa maishani ni Rais Kikwete hivyo aachwe atekeleleze mchakato wa katiba kupunguza mfumko wa bei na kujenga barabara za hewani.<<

Kwanza, naona huyu mchungaji ni kibaraka! Kuheshimu mamlaka ni pamoja na kuikosoa (kuisaidia) mamlaka ili uwazi na uwajibikaji uongezeke. Kuna njia nyingi za kuwajibisha mamlaka. Njia mojawapo ni kupitia kura na nyingine ni kukosoa (constructive criticism) - kusema namna gani kitu fulani kingeweza kufanywa kwa namna bora zaidi. Yohana Mbatizaji alifanya hivyo kwa watu mbalimbali. Mafundisho ya Yesu nayo yalilenga hayo mamlaka - kubadilisha/kuboresha mfumo wa utawala ili haki itendeke zaidi kwa watu wa kawaida. Sasa huyo mchungaji yeye mafundisho yake anayatoa wapi kama siyo kwa Yesu?

Pili, huyo mchungaji uwezo wake wa kuchambua maandiko matakatifu unatia shaka! Kwa nini Musa alutumwa kuwakomboa Waisrael Misri kutoka kwa utawala dhalimu kama kutii mamlaka ni kukaa kimya na kukubali uovu wa wawatawala uendelee?

Tatu, kama anachokisema kina 'logic' basi kwa nini watu ambao Mungu aliwaumbwa "na tazama kila alichoumba ni chema" leo kuna magenge ya mafisaidi, wauaji, wabakaji, wachakachuaji... nk? Si tungeamini tu kuwa kila alichoumba Mungu ni chema na hivyo hakuna maovu duniani? Watu wanaweza kuchaguliwa na Mungu lakini Mungu huyohuyo kawapa utashi wa kuchagua mema na mabaya. Mtu akichagua kutenda mema tutamsifia. Akichagua vibaya, tutamkosoa. Hii yote ni kutaka tusonge mbele. Kwa mawazo ya huyo mchungaji kwa vile mtu ameumbwa na Mungu, kwa hiyo hakuna namna anayoweza kutenda mabaya. Sasa yeye huwa anawahubiria watu walioumbwa na nani kama siyo Mungu?
 
Niliwahi kumsikia mtaalamu mmoja wa afya ya akili akisema karibu watu wote tuna matatizo vichwani, isipokuwa kiwango cha matatizo ya akili ndicho kinafanya wenzetu kuwehuka na sisi kujiona wazima. Huyu mchungaji nahisi kiwango kinaongezeka kwa kasi.........
 
Tatizo la watu wengi ni kufikiri kuwa mtu akiitwa Mchungaji au Askofu au Nabii basi ni mtakatifu na anjua kila kitu. Maandiko yanasema hakuna aliye msafi isipokuwa Mungu na wote wamefanya dhambi. Kwa hivyo tubadili mind set zetu kuwaona hawa watu kuwa ni sawa na watu wengine wowote wale tofauti ni roles zao ktk jamii.

Having said that anachosema Mchungaji Lusekelo ni sawa na mtu mwingine yeyote yule asiyekuwa na weledi ktk anachokisema. Kwa sababu ya sifa uchungaji anakuwa blinded kuwa anafahamu kila kitu.
 
Niliwahi kumsikia mtaalamu mmoja wa afya ya akili akisema karibu watu wote tuna matatizo vichwani, isipokuwa kiwango cha matatizo ya akili ndicho kinafanya wenzetu kuwehuka na sisi kujiona wazima. Huyu mchungaji nahisi kiwango kinaongezeka kwa kasi.........
Teh teh hata mimi nilisikia juu ya hili ila sikujua kama wapakwa mafuta wa bwana nao wamo , teh inapungua na kupanda kama CD4?
 
Watu wengine bwana wakishajifanya watumishi wa Mungu basi wanadhania kila watakalosema litakuwa na maana kwa watu wote. Sijui hayo aliyasema kanisani kwake au kwenye media. Kama ameyasema nje ya kanisa lake amekosea kwa kuwa yeye ni ''mchungaji na mhubiri'' tu wa kikundi fulani cha watu wasiozidi elfu tano pale Dar es Salaam. Hana mamlaka yoyote kujiaminisha kwamba anastahili kuhubiri siasa kwa watanzania wote. Na kama alihisi anastahili kachemsha vibaya: "Alisema kuwa ana imani kuwa rais atakayekumbukwa maishani ni Rais Kikwete hivyo aachwe atekeleleze mchakato wa katiba kupunguza mfumko wa bei na kujenga barabara za hewani.'' Huwezi kumchukulia serious mtu anyesema hivyo hata kama anjiita mchungaji.
 
Kwanza, naona huyu mchungaji ni kibaraka! Kuheshimu mamlaka ni pamoja na kuikosoa (kuisaidia) mamlaka ili uwazi na uwajibikaji uongezeke. Kuna njia nyingi za kuwajibisha mamlaka. Njia mojawapo ni kupitia kura na nyingine ni kukosoa (constructive criticism) - kusema namna gani kitu fulani kingeweza kufanywa kwa namna bora zaidi. Yohana Mbatizaji alifanya hivyo kwa watu mbalimbali. Mafundisho ya Yesu nayo yalilenga hayo mamlaka - kubadilisha/kuboresha mfumo wa utawala ili haki itendeke zaidi kwa watu wa kawaida. Sasa huyo mchungaji yeye mafundisho yake anayatoa wapi kama siyo kwa Yesu?

Pili, huyo mchungaji uwezo wake wa kuchambua maandiko matakatifu unatia shaka! Kwa nini Musa alutumwa kuwakomboa Waisrael Misri kutoka kwa utawala dhalimu kama kutii mamlaka ni kukaa kimya na kukubali uovu wa wawatawala uendelee?

Tatu, kama anachokisema kina 'logic' basi kwa nini watu ambao Mungu aliwaumbwa "na tazama kila alichoumba ni chema" leo kuna magenge ya mafisaidi, wauaji, wabakaji, wachakachuaji... nk? Si tungeamini tu kuwa kila alichoumba Mungu ni chema na hivyo hakuna maovu duniani? Watu wanaweza kuchaguliwa na Mungu lakini Mungu huyohuyo kawapa utashi wa kuchagua mema na mabaya. Mtu akichagua kutenda mema tutamsifia. Akichagua vibaya, tutamkosoa. Hii yote ni kutaka tusonge mbele. Kwa mawazo ya huyo mchungaji kwa vile mtu ameumbwa na Mungu, kwa hiyo hakuna namna anayoweza kutenda mabaya. Sasa yeye huwa anawahubiria watu walioumbwa na nani kama siyo Mungu?

Laiti huyu mchungaji angekua anapitia jf angechukua huu ushauri. Napenda kuona Watz tunajibu kwa hoja na sio kwa kurupuka. Kwa mfano, najiuliza huyu mchungaji anavyokua mnafiki ana maana gani. Hivi kweli mtu akikosea asirekebishwe? Kikwete ni binadam anakosolewa pale alipokosea ili yeye binafsi na serikali yake wajirekebishe. Na pale atakapofanya vizuri tutamsifu pia.. Hatutasubiri mpaka afe kama anavyodai huyu mchungaji. Pia hakuna Mtanzania aliemlaum Kikwete kwa kukosekana mvua, labda hii atakuwa ameitoa kwa waumini wake. Kuna hoja za msingi ambazo watu wanazizunguzia kama katiba mpya., kulipwa kwa dowans n.k. Kwa nini Lusekelo hakumsihi Kikwete awe wazi na atoe mcmamo wake. Huu ni unafiki na kufilisika kifikra.
 
Hizo ni changamoto kwa rais,yaani mzee wa upako anataka watu waitikie Aaamen kwa kila kitu,haiwezekani.
 
Waommbewa hawafiki tena kwenye maombezi wote wameamia Loliondo,sadaka zimepungua naona sasa anabadilika kuwa katibu mwenezi wa CCM kama sio msemaji wa JK.Yeye na Kakobe babu alisema wakanywe dawa. FASTAA...Wanaumwa...!!
 
Back
Top Bottom